Polisi Trafiki na Ukaguzi wa Leseni hawafanyi kazi kwa weledi!

Polisi Trafiki na Ukaguzi wa Leseni hawafanyi kazi kwa weledi!

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
1681194060398.jpeg

Tumesikia hivi karibuni, tangazo la Polisi Trafiki kupitia kwa Kamanda wa Trafiki Ramadhani Ng'azi kuwa dereva aje na leseni, kitambulisho cha NIDA, kitambulishi cha mlipa kodi TIN, cheti cha afya na shada ya shule aliyisomea udereva!

Kwa hayo masharti tu, unagundua kuwa kitengo chetu kina tatizo kubwa. Kwanza hawakujitayarisha kiutendaji kwa zoezi. Unachohitaji hapo ni namba ya leseni tu iliyosajiliwa na TRA. Ukiacha cheti cha afya, vingine vyote unavipata kwa mtandao.

Zoezi hili linaweza kuwa mtambo wa rushwa kwa Askari wa Trafiki.

Kamanda IGP alitazame hilo kwa makini.
 
Leseni wanatoa wenyewe, kinacho wafanya wakague kitu walichotoa wenyewe Ni nini?
Kama Ni ukaguzi wa leseni Basi ifanywe na taasis nyingine sio polisi.
Kwa kweli zoezi kama hili ni mtambo wa rushwa tu.
Na yamekuwapo mazoezi kama haya zaidi ya matano katika miaka ya karibuni.
Matokeo yake wala hatujulishwi.
 
Tumesikia hivi karibuni, tangazo la Polisi Trafiki kupitia kwa Kamanda wa Trafiki Ramadhani Ng'azi kuwa dereva aje na leseni, kitambulisho cha NIDA, kitambulishi cha mlipa kodi TIN, cheti cha afya na shada ya shule aliyisomea udereva...
Na hiyo leseni ilitokaji TRA bila TIN number. Kwamba mifumo ya leseni haifungamani na TIN number....anyway hawa watu ni basi tu...wengi wao ni zile product za div 4 na ziro
 
Leseni wanatoa wenyewe, kinacho wafanya wakague kitu walichotoa wenyewe Ni nini?

Kama ni ukaguzi wa leseni Basi ifanywe na taasis nyingine sio polisi.
Kwanza,Leseni ya udereva haitolewi na polisi.

Pili,Hizo leseni zina madaraja ambayo yameainisha mtu ataendesha nini.

Unakaguliwa kuona kama leseni yako inaendana na chombo unachoendesha.
 
Polisi wa Tanzania kwa Elimu zetu hizi hizi ila wao wanaweza kutambua kila kitu kuanzia kugagua cheti cha Afya,Bima na matakataka mengine hiyo kazi kama wao na TRA ndio wametoa Leseni iweje tena wao wenyewe ndio wakague kwa nini taasisi ingine au Tume indie kwa ajili hiyo hao jamaa wanatengeneza mazingira ya kupora hela za Wananchi kwa kupitia Rushwa kama wanavyoiba kuhusu Sticker za kwenda kwa usalama hizi CAG hajazizungumzia...wanakusanya hela kwenye mabegi bila hata risiti ya Serikali Nchi hii kiboko baadae wataanza kupiga fine wasiohakikiwa na Leseni wanazo...
 
Kwa gari binafsi ukikutana nao barabarani wanaangalia stika ya nenda kwa usalama tu na tochi zimerudi tena.
 

Tumesikia hivi karibuni, tangazo la Polisi Trafiki kupitia kwa Kamanda wa Trafiki Ramadhani Ng'azi kuwa dereva aje na leseni, kitambulisho cha NIDA, kitambulishi cha mlipa kodi TIN, cheti cha afya na shada ya shule aliyisomea udereva!

Kwa hayo masharti tu, unagundua kuwa kitengo chetu kina tatizo kubwa. Kwanza hawakujitayarisha kiutendaji kwa zoezi. Unachohitaji hapo ni namba ya leseni tu iliyosajiliwa na TRA. Ukiacha cheti cha afya, vingine vyote unavipata kwa mtandao.

Zoezi hili linaweza kuwa mtambo wa rushwa kwa Askari wa Trafiki.

Kamanda IGP alitazame hilo kwa makini.
Tanzania ndo nchi pekee ambayo kila mtu ni mchambuzi wa kila Tasisi na idara.....
 
Leseni ya udereva inatolewa na TRA baada ya recommendation za polisi.
Usidandie treni kwa mbele.
Leseni wanatoa wenyewe, kinacho wafanya wakague kitu walichotoa wenyewe ni nini?

Kama ni ukaguzi wa leseni Basi ifanywe na taasis nyingine sio polisi.
Unajichanganya tu hakuna hata ulijualo.

Kuna Leseni za muda/kujifunzia udereva (Daraja H) zinatolewa na TRA bila hiyo recommendation ya polisi na ndiyo utaratibu na watu wanaendeshea vyombo barabarani.
 
Unajichanganya tu hakuna hata ulijualo.

Kuna Leseni za muda/kujifunzia udereva zinatolewa na TRA bila hiyo recommendation ya polisi na ndiyo utaratibu na watu wanaendeshea vyombo barabarani.
Maneno mengi hayajengi. Tuelimishe jinsi ya mtu kupata leseni ya udereva Tanzania. Chukulia MTU huyo Hana hata hiyo provisional licence.
 
Back
Top Bottom