Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Polisi nchini Uganda wamekanusha madai kwamba kiongozi wa upinzani, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, alipigwa risasi Jumanne jioni, badala yake, wamesema kwamba kiongozi huyo wa National Unity Platform (NUP) alijeruhiwa wakati akijaribu kuingia kwenye gari lake.
Kwa mujibu wa msemaji wa polisi, Kituuma Rusoke, amesema maafisa wa polisi waliokuwepo eneo hilo wanadai kuwa Bobi Wine alijikwaa wakati akijaribu kuingia kwenye gari lake na kupelekea jeraha hilo, ingawa Bobi Wine na timu yake wanasisitiza kuwa alipigwa risasi.
Taarifa ya Polisi inaeleza kuwa Bobi Wine na timu yake walipanga maandamano hadi mji wa Bulindo licha ya polisi kupiga marufuku maandamano hayo, ambapo alipata majeraha wakati wa mvutano na polisi.
Source: Jambo TV Online
Mnadhani nani anasema ukweli? Serikali ya Uganda au Bobi Wine?
Soma: Bobi Wine apigwa risasi ya mguu katika vuta n'kuvute na polisi
Kwa mujibu wa msemaji wa polisi, Kituuma Rusoke, amesema maafisa wa polisi waliokuwepo eneo hilo wanadai kuwa Bobi Wine alijikwaa wakati akijaribu kuingia kwenye gari lake na kupelekea jeraha hilo, ingawa Bobi Wine na timu yake wanasisitiza kuwa alipigwa risasi.
Taarifa ya Polisi inaeleza kuwa Bobi Wine na timu yake walipanga maandamano hadi mji wa Bulindo licha ya polisi kupiga marufuku maandamano hayo, ambapo alipata majeraha wakati wa mvutano na polisi.
Source: Jambo TV Online
Mnadhani nani anasema ukweli? Serikali ya Uganda au Bobi Wine?
Soma: Bobi Wine apigwa risasi ya mguu katika vuta n'kuvute na polisi