Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 8,870
- 14,258
Wananchi wa Palestina eneo la Gaza wameendelea kupata nafuu ya amani wakati wakirudi kwenye maeneo waliyokuwa wakiishi kote Gaza kufuatia usitishwaji wa vita kati yao na Israel vilivyodumu kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Hali hiyo inatokana na kurudi kwa polisi wa Hamas wakiwa wamevalia sare zao maarufu za rangi ya bluu.Wananchi hao wamesema hata wakiwa makambini hawajawahi kukosekana na ndio maana kwenye kambi hizo hakuna wizi na uvunjifu wa amani.
Kuonekana kwa asakari hao kumeendelea mpaka eneo la Jabalia ambalo ndio lililopata athari mbaya zaidi ya vita. Majengo matatu tu ndiyo yaliyobaki wima yakiwa yameporomoshwa ghorofa za juu yake. Zaidi ya hapo huduma zote zinazopelekea uhai wa binadamu zilikatwa kwa zaidi ya miezi 3.
Wananchi waliorudi eneo hilo la kaskazini kabisa mwa Gaza mpakani na Israel walishangaa wakiwa wanaingia kukuta wakikaribishwa na kuongozwa na askari hao wa Hamas.
View: https://www.youtube.com/watch?v=SklZqgPTS00
Hali hiyo inatokana na kurudi kwa polisi wa Hamas wakiwa wamevalia sare zao maarufu za rangi ya bluu.Wananchi hao wamesema hata wakiwa makambini hawajawahi kukosekana na ndio maana kwenye kambi hizo hakuna wizi na uvunjifu wa amani.
Kuonekana kwa asakari hao kumeendelea mpaka eneo la Jabalia ambalo ndio lililopata athari mbaya zaidi ya vita. Majengo matatu tu ndiyo yaliyobaki wima yakiwa yameporomoshwa ghorofa za juu yake. Zaidi ya hapo huduma zote zinazopelekea uhai wa binadamu zilikatwa kwa zaidi ya miezi 3.
Wananchi waliorudi eneo hilo la kaskazini kabisa mwa Gaza mpakani na Israel walishangaa wakiwa wanaingia kukuta wakikaribishwa na kuongozwa na askari hao wa Hamas.
View: https://www.youtube.com/watch?v=SklZqgPTS00