Polisi wafafanua tukio la Wakili Lusako Alphonce kukikimbizwa na Polisi katika Ofisi za "Reachout Tanzania"

Polisi wafafanua tukio la Wakili Lusako Alphonce kukikimbizwa na Polisi katika Ofisi za "Reachout Tanzania"

View attachment 3169735
TAARIFA KWA UMMA
Taarifa iliyo upande wa kushoto inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Jeshi la Polisi lingependa kuitolea ufafanuzi ili isiendelee kuleta taharuki ambayo si ya lazima.

Ni kweli Askari Polisi walifika eneo hilo kumkamata mtuhumiwa anayejulikana kwa jina la Emmanuel Mweta, ambaye awali alikamatwa na baada ya kudhaminiwa aliruka dhamana kwa muda mrefu.
Leo Desemba 5,2024, Mlalamikaji alitoa taarifa Polisi kuwa, amemuona mtuhumiwa huyo, ikabidi askari wawahi haraka kumkamata.

Tunaendelea na uchunguzi kubaini ni nini kilichomfanya anayetajwa kwa jina la Alphonce Lusako kukimbia kisha kujirekodi video voice na kuirusha kwenye mitandao wakati siyo yeye aliyekuwa anatafutwa na Askari waliofika pale walijitambulisha kwake na kumweleza wamefika pale kwa nia ya kumtafuta Emmanuel Mweta.
Imetolewa na:

David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania

Pia soma ~ Makumbusho: Polisi wadaiwa kuvamia Ofisi za "Reachout Tanzania", wakidai kumtafuta Wakili Lusako Alphonce
Jeshi la polisi haliaminiki tena kwa sasa labda utawala wa ngazi ya juu ubadilike kwa kura za wananchi. Polisi wameshajichafua sana hata kama zoezi wanalolifanya ni la haki bado shaka ni kubwa sana na haiwezi kutengenezwa na ikasafishika kwa kifaa chochote.
Namna ya ukamataji waliyoianzisha kwa siku za hivi karibuni yenye mtindo wa kuteka hakuna wa kuwaamini kwa lolote.
 
Kawashtaki mahakamani maana hata wao huwa wanashtaki watuhumiwa mahakamani kwahiyo kama wamesambaza unaweza kabisa kuwashtaki
Kama tu Mahakama imewaachia huru polisi waliohusika kwenye kupora hela unadhani kuna haki hapo!? Mahakama inaendeshwa na Rais 😃 nchi ya Peru kuna maajabu sana
 
Kama tu Mahakama imewaachia huru polisi waliohusika kwenye kupora hela unadhani kuna haki hapo!? Mahakama inaendeshwa na Rais 😃 nchi ya Peru kuna maajabu sana
Kama imewaachia maana yake hakukua na ukweli
 
View attachment 3169735
TAARIFA KWA UMMA
Taarifa iliyo upande wa kushoto inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Jeshi la Polisi lingependa kuitolea ufafanuzi ili isiendelee kuleta taharuki ambayo si ya lazima.

Ni kweli Askari Polisi walifika eneo hilo kumkamata mtuhumiwa anayejulikana kwa jina la Emmanuel Mweta, ambaye awali alikamatwa na baada ya kudhaminiwa aliruka dhamana kwa muda mrefu.
Leo Desemba 5,2024, Mlalamikaji alitoa taarifa Polisi kuwa, amemuona mtuhumiwa huyo, ikabidi askari wawahi haraka kumkamata.

Tunaendelea na uchunguzi kubaini ni nini kilichomfanya anayetajwa kwa jina la Alphonce Lusako kukimbia kisha kujirekodi video voice na kuirusha kwenye mitandao wakati siyo yeye aliyekuwa anatafutwa na Askari waliofika pale walijitambulisha kwake na kumweleza wamefika pale kwa nia ya kumtafuta Emmanuel Mweta.
Imetolewa na:

David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania

Pia soma ~ Makumbusho: Polisi wadaiwa kuvamia Ofisi za "Reachout Tanzania", wakidai kumtafuta Wakili Lusako Alphonce
 
View attachment 3169772Huyu baba asipotubu dhambi za uongo ulio kubuhu basi siku ya kiama ajiandae kuchomwa moto wake malaika wa adhabu watatumia Chlorine Trifluoride (ClF3). Yaani muende kumkamata mhusika mwingine kisha muondoke na gari ya mtu mwingine?.
Shuhuda kahojiwa na Jambo tv anasema polisi aliyekuwa na kitambulisho alisema wazi kuwa wamekuja kumkamata mtuhumiwa anaitwa Lusako. David Misime tubu mapema kabla hayajakukuta.
Nae wamemuweka chambo tu.
 
View attachment 3169735
TAARIFA KWA UMMA
Taarifa iliyo upande wa kushoto inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Jeshi la Polisi lingependa kuitolea ufafanuzi ili isiendelee kuleta taharuki ambayo si ya lazima.

Ni kweli Askari Polisi walifika eneo hilo kumkamata mtuhumiwa anayejulikana kwa jina la Emmanuel Mweta, ambaye awali alikamatwa na baada ya kudhaminiwa aliruka dhamana kwa muda mrefu.
Leo Desemba 5,2024, Mlalamikaji alitoa taarifa Polisi kuwa, amemuona mtuhumiwa huyo, ikabidi askari wawahi haraka kumkamata.

Tunaendelea na uchunguzi kubaini ni nini kilichomfanya anayetajwa kwa jina la Alphonce Lusako kukimbia kisha kujirekodi video voice na kuirusha kwenye mitandao wakati siyo yeye aliyekuwa anatafutwa na Askari waliofika pale walijitambulisha kwake na kumweleza wamefika pale kwa nia ya kumtafuta Emmanuel Mweta.
Imetolewa na:

David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania

Pia soma ~ Makumbusho: Polisi wadaiwa kuvamia Ofisi za "Reachout Tanzania", wakidai kumtafuta Wakili Lusako Alphonce

Kwa hali ilivyo kwasasa kijana yupo sahihi kukimbia kujiokoa kwan kama walikuja bila kutoa taarifa lazima ujihami
 
Jeshi la polisi nchini limekuwa katika hali ya kutoviamini kwa wananchi, hali ambayo imejikita kwa muda mrefu. Katika mazingira haya, kuna hisia kwamba mabadiliko ya kweli yanaweza kuja tu kupitia utawala mpya utakaopatikana kwa njia ya uchaguzi wa kidemokrasia. Hata ingawa kuna juhudi zinazofanywa na polisi katika kutekeleza majukumu yao, imani ya umma imeporomoka kwa kiasi kikubwa kutokana na matukio mbalimbali ya ukiukwaji wa haki za binadamu na matumizi mabaya ya madaraka.

Moja ya sababu kuu za kutokuwepo kwa imani hii ni tabia ya polisi katika ukamataji. Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na mtindo wa ukamataji ambao unahusisha vitendo vya kuteka watu. Kitendo hiki kimeleta hofu kubwa miongoni mwa wananchi na kuifanya jamii kuwa na shaka kuhusu lengo halisi la jeshi la polisi. Wananchi wanajiuliza: je, polisi wanateka watu kwa sababu ya uhalifu, au kuna sababu nyingine za kisiasa au binafsi? Hali hii inachangia kuhamasisha wasiwasi na kutokuwepo kwa ushirikiano kati ya wananchi na vyombo vya usalama.

Polisi wamejichafua katika macho ya umma kutokana na matukio mengi ya kashfa na ukiukwaji wa sheria. Hii ni pamoja na matumizi ya nguvu kupita kiasi katika kukabiliana na waandamanaji na raia wengine. Watu wengi wamekuwa wakikumbana na ukatili usio wa kawaida, na matukio haya yamekuwa yakirekodiwa na vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, hivyo kueneza picha mbaya kuhusu jeshi la polisi. Iwe ni kwa sababu ya kukosekana kwa mafunzo yafaayo, au kwa sababu ya mfumo wa usimamizi wa polisi, imani ya wananchi imeporomoka kwa kiasi kikubwa.

Wakati polisi wanapojaribu kujenga taswira chanya kupitia kampeni mbalimbali za uhamasishaji, bado wahusika wa ukamataji wanaonekana kuwa na mtazamo wa kibaguzi na wa kikatili. Hii inadhihirisha hitilafu katika mfumo mzima wa uendeshaji wa kazi za polisi. Kwa upande mwingine, wananchi wanaweza kuwa na hofu ya kushirikiana na polisi, wakihofia kuwa ushirikiano wao unaweza kuwapelekea katika matatizo zaidi. Hali hii inaathiri si tu usalama wa raia, bali pia juhudi za polisi za kupambana na uhalifu.

Mabadiliko katika utawala wa polisi yanaweza kuwa muhimu katika kurejesha imani ya umma. Ni dhahiri kuwa bila mabadiliko haya, hali itabaki kuwa mbaya. Wananchi wanahitaji kuona viongozi wa polisi wakifanya kazi kwa uwazi na kwa uwajibikaji. Miongoni mwa hatua zinazoweza kuchukuliwa ni pamoja na kuanzishwa kwa mipango ya mafunzo ya mara kwa mara kwa maafisa wa polisi, ili wangeweza kuelewa umuhimu wa kuheshimu haki za binadamu na taratibu za kisheria.

Aidha, kuna umuhimu wa kuimarisha uhusiano kati ya polisi na jamii. Hii inaweza kufanywa kwa njia ya mikutano ya mara kwa mara kati ya polisi na wananchi, ambapo pande zote zinaweza kujadili masuala yanayowakabili na kutafuta suluhu za pamoja. Uhusiano mzuri kati ya polisi na raia utasaidia kuondoa hofu na kujenga imani mpya, ambayo ni muhimu kwa usalama wa jamii nzima.

Pia, kuna haja ya kuangalia mifumo ya usimamizi wa polisi ili kuhakikisha kuwa kuna uwazi na uwajibikaji. Hii inaweza kujumuisha kuanzishwa kwa mifumo ya ufuatiliaji wa shughuli za polisi, ambapo wananchi wanaweza kutoa taarifa kuhusu ukiukwaji wa haki na matumizi mabaya ya madaraka. Kwa njia hii, polisi wataweza kujifunza kutokana na makosa yao na kuboresha huduma zao.

Kwa ujumla, kutokuwepo kwa imani katika jeshi la polisi ni tatizo kubwa linalohitaji hatua za haraka. Mabadiliko katika utawala, mafunzo ya mara kwa mara, na uhusiano mzuri na jamii ni baadhi ya hatua ambazo zinaweza kusaidia kurejesha imani ya wananchi. Bila hatua hizi, hali itabaki kuwa ngumu, na wananchi wataendelea kuishi katika hofu na kutokuwepo kwa usalama.
 
Emmanuel Mweta,si mtumishi Wala mfanyakazi wa Reachout Tanzania.
Polisi wamekuwa vituko nchini.
Tangu warushe ma helicopter na mandefe kudhibiti maandamano ya UKUTA. Akili hazijakaa sawa.
Ndo kosa la kuajiri watu kwa sifa ya kuwa warefu na wenye mbio kichwani hamna kitu
 
Polisi kila siku ni clarifications. Inatia shaka na wasiwasi. Watanzania wa leo sio wa miaka 10 nyuma, wajitafakari.
 
Bora kumwamini shetani kuliko wale watu ..
 
Back
Top Bottom