Polisi wafeli kufukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi baada ya Familia kudai kutoshirikishwa

Polisi wafeli kufukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi baada ya Familia kudai kutoshirikishwa

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Polisi wameshindwa kufukua mwili unaodaiwa kuzikwa kimakosa katika kitongoji cha Dungi, Kijiji cha Kibosho Kindi, Wilaya ya Moshi, baada ya ndugu kudai hawana taarifa hiyo na kutaka waonyeshwe kibali cha kuwaruhusu kufanya hivyo.

Mwili huo unaodaiwa kuwa wa Richard Shoo, aliyefariki dunia Juni 19, 2024 ulitakiwa kufukuliwa kwa ajili ya uchunguzi na vipimo vya vinasaba (DNA), baada ya familia moja kuibuka na kudai mwili huo uliozikwa si wa marehemu Shoo bali wa kijana wao.

Baada ya sintofahamu hiyo, inadaiwa Mahakama iliamuru mwili huo ukafukuliwe, ili kufanyika kwa vipimo na taratibu nyingine za kisheria zifuate.

Hata hivyo, Polisi jana Jumapili Septemba Mosi, 2024 wakiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Moshi wakiambatana na madaktari wawili, walifika kwa ajili ya kufukua mwili huo, lakini ilishindikana baada ya familia kudai kutoshirikishwa na kutaka kuonyeshwa kibali cha kufukua mwili huo na polisi hawakuwa nacho.

Soma Pia:
Polisi walilazimika kuomba kutumiwa kibali hicho kwa simu ambacho walieleza walikiacha ofisini, lakini familia hiyo ilikataa na kudai wanahitaji kukiona, hali iliyosababisha kuahirishwa shughuli hiyo.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema kazi ya kufukua mwili huo lilishindikana baada ya upande mmoja kutoridhia na baadhi ya wanafamilia kudai kutoshirikishwa suala hilo.
 
Back
Top Bottom