John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Mnamo tarehe 06.03.2022 majira ya saa 18:00 jioni, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilifanya msako huko Mtaa wa Mwanyanje – Uyole, Kata ya Uyole, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya na kufanikiwa kumkamata ABDUL MWAKALINGA [27] Dereva Tax, Mkazi wa Uyole akiwa na bidhaa zilizozuiliwa kuingizwa nchini na zilizokwepa kulipiwa ushuru wa forodha kutoka nchini Zambia ambazo ni:-
1. Vitenge jora 87,
2. Nyavu za kuvulia Samaki matundu madogo viroba 10,
3. Boksi 06 zenye vipodozi vyenye viambata sumu aina ya maji ya citrolight, Ct + Clear therapy, Cocoplus, Miss mimi
4. Kiroba 01 chenye vipodozi aina ya Anti Blacks Spots, Stretch Marks and Pimples.
5. Kiroba 01 chenye vipodozi aina ya Epiderm Crème.
Jumla ya mali yote iliyokamatwa ni zaidi ya milioni tisa. Mtuhumiwa ni msafirishaji na muuzaji wa bidhaa hizo zilizopigwa marufuku nchini na zilizokwepa kulipiwa ushuru wa forodha. Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi wa shauri hili kukamilika.
Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA
1. Vitenge jora 87,
2. Nyavu za kuvulia Samaki matundu madogo viroba 10,
3. Boksi 06 zenye vipodozi vyenye viambata sumu aina ya maji ya citrolight, Ct + Clear therapy, Cocoplus, Miss mimi
4. Kiroba 01 chenye vipodozi aina ya Anti Blacks Spots, Stretch Marks and Pimples.
5. Kiroba 01 chenye vipodozi aina ya Epiderm Crème.
Jumla ya mali yote iliyokamatwa ni zaidi ya milioni tisa. Mtuhumiwa ni msafirishaji na muuzaji wa bidhaa hizo zilizopigwa marufuku nchini na zilizokwepa kulipiwa ushuru wa forodha. Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi wa shauri hili kukamilika.
Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA