Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 16
Polisi watawanya msafara wa Mbowe
Na Mussa Juma
MSAFARA wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana ulivunjwa wa polisi kwa madai kuwa ungesababisha vurugu.
Tukio hilo lilitokea jana saa 12.00 jioni baada ya Mbowe kumaliza kuhutubia mkutano wa kampeni wa kumnadi mgombea wa udiwani wa Kata ya Kati, Seif Simba uliofanyika katika eneo la YMCA.
Mbowe mara baada ya mkutano huo aliamua kutembea kwa miguu kwenda katika ofisi cha Chadema zilizopo karibu na Stendi Kuu ya mabasi mjini hapa.
Mbowe ambaye alikuwa akisindikizwa na wafuasi wengi wa chama hicho mara alipofika katika eneo la Stedi ya mabasi polisi waliokuwa na mabomu ya machozi wakiwa katika magari matatu, waliwaamuru watu waliokuwa katika msafara huo watawanyike na mbowe apande gari lake aondoke.
Hata hivyo, Mbowe alipinga amri hiyo na hivyo polisi walitishia kuwapiga mbomu ya machozi watu hao, hali ambayo iliwafanya watawanyike.
Mbowe naye aliingia katika gari lake na kuanza kuondoka huku akisindikizwa na magari hayo ya Polisi akielekea katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Hata hivyo, Polisi hao walilishikilia kwa muda gari la matangazo la chama hicho aina ya Fuso kuwa lilikuwa likisababisha mikusanyiko ya watu.
Awali akihutubiua mkutano huo aliwataka wanachama wa chama hicho leo kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kwamba mara baada ya kupiga kura wasiondoke kwenye vituo vya kupigia kura kulinda kura zao.
Na Mussa Juma
MSAFARA wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana ulivunjwa wa polisi kwa madai kuwa ungesababisha vurugu.
Tukio hilo lilitokea jana saa 12.00 jioni baada ya Mbowe kumaliza kuhutubia mkutano wa kampeni wa kumnadi mgombea wa udiwani wa Kata ya Kati, Seif Simba uliofanyika katika eneo la YMCA.
Mbowe mara baada ya mkutano huo aliamua kutembea kwa miguu kwenda katika ofisi cha Chadema zilizopo karibu na Stendi Kuu ya mabasi mjini hapa.
Mbowe ambaye alikuwa akisindikizwa na wafuasi wengi wa chama hicho mara alipofika katika eneo la Stedi ya mabasi polisi waliokuwa na mabomu ya machozi wakiwa katika magari matatu, waliwaamuru watu waliokuwa katika msafara huo watawanyike na mbowe apande gari lake aondoke.
Hata hivyo, Mbowe alipinga amri hiyo na hivyo polisi walitishia kuwapiga mbomu ya machozi watu hao, hali ambayo iliwafanya watawanyike.
Mbowe naye aliingia katika gari lake na kuanza kuondoka huku akisindikizwa na magari hayo ya Polisi akielekea katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Hata hivyo, Polisi hao walilishikilia kwa muda gari la matangazo la chama hicho aina ya Fuso kuwa lilikuwa likisababisha mikusanyiko ya watu.
Awali akihutubiua mkutano huo aliwataka wanachama wa chama hicho leo kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kwamba mara baada ya kupiga kura wasiondoke kwenye vituo vya kupigia kura kulinda kura zao.
Last edited by a moderator: