Polisi watoa taarifa kifo cha Ulomi wasema alifariki kwa ajali ya pikipiki

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Hivi mnaona hii pattern ya watu kutekwa sasa hivi pamoja na reporting yake?

Wote (uliondoa wanasiasa mashuhuri) ni wafanyabiashara au wanahusishwa na biashara, na zote bwana Ayo amekuwa mstari wa mbele utafikiri anapewa headsup kuwa hii freshi unaweza kuripoti?!

Halafu tayari kulikuwa na taarifa ya Ulomi kupotea na kutafutwa na polisi, ina maana mifumo haisomani mwili wa mtu asiyetambulika unapopatikana toka tar 11 mpaka leo?🤔

Nawaza tu.... kuna ka kitu kanatengenezwa hapa.

Pia soma: Katibu wa Afya Hospitali ya Mwanyamala: Ulomi alipata ajali, mwili uliletwa December 11, 2024

 
Hii agenda ilianza kipindi cha mzee Reginald mengi hadi akalalamika kwenye tv yake ni ajenda ya raia feki kushika uchumi wote mkuu wa tz na njia zote za uchumi kuu...pia ni agenda ya kushika serikali yote kuwa mali yao binafsi ndiyo maana mnaona mambo ya ajabu yanaendelea nchini.JAMBAZI ROSTAM AZIZI NA GENGE LAKE NI WAHUSIKA WAKUU
 
Sijui kama wengine hamuoni utata kwenye taarifa ya polisi
 
Kuna mtu anasema alimpigia marehemu kuwa anafuatiliwa na Landcruiser
Alipotajiwa namba ikaonekana namba za gari hilo ni za gari la Kahama ila liko Ilala
Hiyo ajali ilitokea eneo gani na mashuhuda ni nani
Nani huyo aisaidie polisi sio unasema kunamtu tu
 
Nani huyo aisaidie polisi sio unasema kunamtu tu
Polisi wasaidiwe wapi tena wakati taarifa yao imekamilika?

Saivi wamehamia hatua ya tatu ya kutafuta chanzo cha ajali ni nini.
Hatua ya kwanza kupokea taarifa, hatua ya pili kutoa mrejesho na ya tatu sasa ni kufuatilia chanzo cha tukio na mwisho kabisa hatua ya nne kama watataka watatoa mrejesho wa chanzo cha ajali.
 
Hili jambo lina utata sana. Ina maana kipindi chote hiki hakuna aliyekumbuka kucheki hosptail?
Labda wasamaria wema, zahanati na hospital wote hawakupata taarifa ya kupotea kwake au hawakumtambua!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…