Elections 2010 Poll Watch: Malecela has not lost yet

Status
Not open for further replies.


I see.......noted!
 


Kaka unaijua historia ya Lusinde lakini? Je makubaliano ya 2005? Je network yake sasa CCM? There is no way NEC ikambeba Mzee Malecela.

omarilyas
 
Mijitu bana.

Jana inamcheka Mwakalinga kuwa kashindwa vibaya sana na AIBU KUBWA. Leo hii mijitu iko hapa ikisema na kukiri kuwa CCM wanafanyiana Mchezo Mchafu sana. Na kesho itakuwa inalia kuwa huko Kyela, Dodoma, Dar etc CCM wamecheza mchezo mchafu.

Mkuki kwa nguruwe. Nchi inaendeshwa bila SHERIA yoyote. Rushwa kwa Wapendwa wa Chama tawala zilitawala na zilikuwa zikitolewa waziwazi. Kyela uchafu wa hali ya juu umefanywa na watu wameona waziwazi. Na baadhi yao ni hata member wa JF hapa na sasa wapo wakilaani RUSHWA ingawa na wao wamesaidia kwa hali na mali rushwa kama hizohizo kwenye majimbo ya wapendwa wao.

Bila sheria kali kuwepo na TAKURURU kulinda kwa hali ya juu na sheria kali sana na ikibidi HUKUMU YA KIFO kwa watoa na kupokea rushwa wakati wa uchaguzi, nchi yetu itaendelea KUUZWA na kununuliwa kwa watu wenye pesa zao. Kwa hali iliyopo sasa hivi Tanzania, kitamshinda nini tajiri wa Kimarekani, Kirusi, Kijep, Kichina etc kuja na kununua SERIKALI yetu nzima kwa kuweka wabunge wake? Kama Wananchi wanapenda Tshirt na Pilau, na viongozi ni mfano wetu wenyewe, basi nao wanapenda sana VYA BURE.

Tufurahie tu ndugu zetu wanaposhinda kwa kutumia UMAFIA ila siku tukija kuona nchi inaliwa na Rostam Azziz, basi nisisikie jitu la CCM likilalamika. Mlitoka kwa RUSHWA, mtarudi kwa Rushwa, jina la CCM litukuzwe, Anem.

Kwa sababu CCM imeshindwa kutibu hili GONJWA na watu mwamko bado uko chini, inabidi kupeleka mtu MAGOGONI ili afanye kusafisha kwa kiasi kikubwa RUSHWA. Mtu huyu tujiandikishe na tumsaidie kwa hali na mali na bila kutumia RUSHWA ambayo itakuja kutula tena.

WOTE TUJIANDIKISHE na kuwakumbushe ndugu, jamaa na marafiki ili TUMCHAGUE Dr. Slaa.

UKO NA MAFISADI AU UKO NA Dr. SLAA.
 
ikibidi HUKUMU YA KIFO kwa watoa na kupokea rushwa wakati wa uchaguzi

Mkuu haya maneno ni baada ya Mwakalinga kushindwa au?
 


hehe heheeee!!! babu kaula wachuya! kwishney asubiri mbeleko ya Mafisadi wa NEC sasa
 
Hapana Mkuu. Uchaguzi ndiyo MSINGI wa kila nchi. Unafahamu kwenye nyumba au kila JENGO, msingi ndiyo kitu kikubwa sana na muhimu.

Ukishajenga jengo kwenye MSINGI mbovu, basi kila kitu kitaharibika. Rushwa Tanzania zinaanzia kwenye UCHAGUZI. Ukishapata viongozi walioingia kwa rushwa, basi rushwa itaenda hadi kwa karani wa ofisini. Ukiweza kuvunja RUSHWA wakati wa Uchaguzi, basi kwanza unaanza na BUNGE safi na viongozi wanaofuata sheria. Na kwa sababu wao ndiyo watunga sheria, na baadaye kuja kuwa mawaziri na hata Rais wetu ambaye ndiye huwa kuwa mteuzi wa hawa maboss wa TISS, PCCB, POLICE etc inakuwa ni wazi kuwa atachagua viongozi walio safi. Sasa kama yeye kaingia kwa Hongo na anafahamu kuwa miaka 5 ijayo itakuwa rahisi kwake kuingia kwa Hongo, unafikiri atangaika kufanya kazi? Unafikiri atatunga sheria zitakazombana yeye? Unafikiri atasimama na kukamata wala Rushwa?

Uchaguzi ni MWISHO kabisa wa MNYORORO wa ile hadithi ya KARUMEKENGE. Tukichagua viongozi bila ya rushwa kwa watu kuogopa hukumu ya kifo, basi tutaendela kuwa na Rais asiyependa hongo, Bunge lisilopenda hongo, sheria zisizopendelea rushwa, Mawaziri wasiopenda rushwa, ma DC, Polisi, Takururu, maofisa wa serikali nk nk wasiopenda/wanaoogopa rushwa kwa kufahamu HUKUMU YAKE NI MBAYA SANA.

Kama wewe hilo hulioni na unaona kuwa nimeandika kwa sababu MWAKALINGA kashindwa, nazidi tu kuamini kuwa Tanzania tuna safari ndefu sana kuondoa RUSHWA. Na nitakumbuka hayo maneno yako kila siku. Nikija kuona sehemu unalaani RUSHWA, ntakupa swali kama hilohilo. Nikiona mtu analaani RUSHWA, itabidi nikupe swali kama jamaa na yeye anaandika kwa sababu Mwakalinga kashindwa.

Kesi ya Mwakalinga hapa si muhimu sana. Soma sahihi yangu ndiyo utafahamu lengo langu la mwaka huu ni nini.

UKO na SLAA AU UKO NA MAFISADI. Nyambala, uko wapi??????

Mkuu haya maneno ni baada ya Mwakalinga kushindwa au?
 
Mkuu vipi bana! after october mwenye kuteua wabunge wa jimbo la Ikulu ni Dr, umesahau nini! tehe tehe tehe! Jamaa si apumzike tuu, maana nasikia jamaa hata mshiko anao wa kutosha.
 

.........hayo hapo juu ndio maswali muhimu ya kujiuliza.........na wajuvi wa nyakati huyaona haya hata kabla hayajatokea..........?
 
UKO na SLAA AU UKO NA MAFISADI. Nyambala, uko wapi??????

Msimamo wangu siku zote uko pale pale.............................. i have neva voted for CCM and neva will.
 
'Kenyewe' kamesema bajaji kaangusha tingatinga!

Kwa umahiri wa rafu za kisiasa za Mzee JSM isingewesekana ashindwe kimizengwe; he's so smart for that. Mzee akubali tu kwamba ndiyo hivyo tena. Ambacho anatakiwa ajutie ni kushindwa kusoma alama za nyakati. Angefuata ushauri wa Mzindakaya, haya yasingemkuta. Sasa anaondoka katika siasa disgracefully! Poleni sana wahusika wote
 
Mkuu Fmes, Posts zako zimekuwa zinaleta mwamko mkubwa wa watu kuja hapa jamvini mara kwa mara na hilo lita thihirishwa na siku za karibuni ulipokuwa haupo hapa kumekuwa na mpoozo wa aina fulani.

Naomba usitukimbie hata kama kuna mambo ambayo haya kufuhishi ni vizuri ukayaweka bayana hapa tujaribu kuyatafutia uvumbuzi

Mods, kwenye hile thread ya wana jamiiforum kutinga bunge kuna watu waliongelea kuna mtu alikuwa ana reveal ID za members, majibu yenu hayakuwa NDIYO au HAPANA-kama kuna mtu kafanya hivyo au hakuna kitu kama hicho.Sasa Mkuu wetu naye anaongelea speculating ID za members ingawa kwa upande wangu nimwelewa tofauti alipoendelea "maana kuna siku mtalia kilio cha mbwa mtakaporudi bongo" hii ni zaidi ya kukisia ID z za members.

Ni vizuri kuweka ugonjwa wazi ukatibiwa hata kama utakimbiwa na baadhi ya marafiki kuliko kuficha na bila kusahau "Where We Dare To Talk Openly" au hii dhana inatumika pale tunapojadili watu wengine.

Chonde chonde Mods wekeni hili jambo wazi.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…