Ponda afungwa mwaka mmoja Jela wengine waachiwa huru

Ponda afungwa mwaka mmoja Jela wengine waachiwa huru

Status
Not open for further replies.
Kumuweka Ponda mahabusu kwa muda wote huo kwa kesi ya ki p u u z i kama hii ni UONEZI MKUBWA NA UVUNJWAJI WA WAZI WA HAKI ZA BINADAM!Kuna kesi zinatajwa kwa mtuhumiwa kunyimwa dhamana lkn sio kesi kama hii!

Akipata mwanasheria mzuri Ponda atashinda kesi ya fidia alipwe mamilion!
 
Me ni mwislam wa msimamo wa wastan nimefurahi sana,chuki zimepozwa sana.bongo ya wote sisi ni ndugu tuvumiliane tuunganishwe na U TZ.
 
LEO MAKAHAKA KUU YA KISUTU IMEMUACHIA SHEKH ISSA PONDA

KWA MADAI YAKE YA MSINGI KUHUSIANA NA KIWANJA CHA WAISLAMU CHANG'OMBE KUUZWA NA TAASISI YA BAKWATA(CCM B),ALIFUNGULIWA MASHTAKA YA UCHOCHEZI, WIZI, KUVAMIA ENEO LA WATU, NA KUTOKANA NA MASHTAKA HAYO ALINYIMWA DHAMANA KWA KIPINDI CHOTE HIKI, LEO KAACHIWA, SUALI LANGU KWA WANASHERIA HUMU,
JE, KUACHIWA KWAKE KUNAMAANISHA MADAI YAKE KWA KIWANJA CHA CHANG'OMBE NI SAHIHI?
KM NI HIVYO,JE WAISLAMU WANAWEZA KUFUNGUA MASHTAKA YA KUDAI KIWANJA CHAO KUTOKA KWA BAKWATA(taasisi ambayo CCM na serikaliyake wanaitumia kisiasa zaidi kuliko dinni,na kufanywa wanaharakati waonekane wakorofi kwa kuipinga bawkata).
JE. PONDA NAEZA KUIFUNGILIA MASHTAKA SERIKALI KWA KUMUWEKA NDANI PASINA KOSA?


Ponda hakuwekwa ndani bila kosa na ndio maana amefungwa kifungo cha nje cha mwaka mmoja.

Usahihi wa madai ya Ponda haumpi haki ya kuvunja sheria nyingine. Ponda kama anayo madai dhidi ya mtu yeyote yule, anachotakiwa kufanya ni kuyapeleka madai yake mahakamani.

BAKWATA kweli ni tatizo lkn sijajua suluhisho lake. Je kuna namna ya kuwaunganisha Shiite, Sunni, Ahmaddiya, Mawahabi, Answar Sunni, Ismailliya na wengineo na kuwapa kiti kimoja?
 
Ee Mungu utajalie amani Tanzania Ameeen



Ponda hakuwekwa ndani bila kosa na ndio maana amefungwa kifungo cha nje cha mwaka mmoja.

Usahihi wa madai ya Ponda haumpi haki ya kuvunja sheria nyingine. Ponda kama anayo madai dhidi ya mtu yeyote yule, anachotakiwa kufanya ni kuyapeleka madai yake mahakamani.

BAKWATA kweli ni tatizo lkn sijajua suluhisho lake. Je kuna namna ya kuwaunganisha Shiite, Sunni, Ahmaddiya, Mawahabi, Answar Sunni, Ismailliya na wengineo na kuwapa kiti kimoja?
 

Attachments

  • 521708_10151715893657355_1015067248_n.jpg
    521708_10151715893657355_1015067248_n.jpg
    37.2 KB · Views: 49
Sawa sawa mkuu, lakini unajua kuwa katika taasisi zinazoongoza kwa rushwa nchini, mahakama ipo juu?

KEBEPA:

Umesema kweli kabisa ndio maana wakamwachia Lwakatare! Mahakama zetu kwa kula rushwa tu! yaani hawaogopi kupokea rushwa hata kwa vyama vya siasa!
 
Mahakama imetenda haki na maamuzi yake yaheshimiwe.

Mahakama haijatenda haki kwa kumnyima dhamana Sheikh Ponda kwa kumshikilia gerezani miezi 9! na pia haijatenda haki kumhukumu kifungo cha nje mwaka 1! Sheikh Ponda ni Kiongozi wa Waislamu wanaodai haki zao kama vile wananchi wa Mtwara wanavyodai Gesi yao isisafirishwe!
Wakati umefika kwa Serikali kufungua sikio na kusikiza madai mazito ya Waislamu! kumfunga Sheikh Ponda au kumuachia huru hakufuti madai ya Mamilioni ya Waislamu wanaodhulumiwa mwenye masikio na asikie!
 
Kila mara nasisitiza Watanzania tupendane,tuheshimiane, na katu mmoja wetu asifurahie mwenzake anapopatwa na janga.Wapo wana jamvi ambao wao huweka mbele zaidi imani zao,tena kwa namna ya kuudhi imani nyingine,wakifiki kwa kufanya hivyo mama yetu Tanzania atadumu na kusimama,nao wapate nafasi ya kufanya wanayoyataka.WANAJIDANGANYA!!!Narudia,tusiposhikamana na kurudi enzi za Juma na Rosa,tunawatengenezea watoto wetu dimbwi kubwa la damu(Mwenyezi Apishie mbali)Mwislam ni lazima aheshimu matukufu ya Mkristu,na Mkristu pia ni lazima aheshimu matukufu ya Mwislam.Sisi sote ni Wana wa Ibrahim(amani iwe juu yake).Inanishangaza sana tunasahau asili yetu.Tukipendana Mwenyezi Mungu Atateremsha baraka Zake na nchi yetu itameremeta.Maadui wanajua Mwenyezi Ametupa mali asili nyingi,hali ya kua wao hawakupewa.Wamejaribu sana kutugawa wameshindwa.Sasa wanatumia dini.Sisi badala ya kushituka,bila kujijua tunashangilia.Tuamke leo maana huenda kesho ikatukuta tumechelewa.Tumsifu Yesu Kristu,Asalaam alaykum

maranduhussein;

Nadhani nia yako ni nzuri ndio maana umejaribu kubalance kila kitu! kuanzia Jina lako umechanganya jina la kibantu na kiarabu! halafu umemalizia kwa salamu za baadhi ya Wakristo na Waislamu lakini umewasahau Wasabato na Walokole kwa salamu za Bwana asifiwe na salamu za kimila za MAWWEEE! haha haha!
Vinginevyo nakubaliana nawe umejieleza vizuri sana hasa umenigusa pale uliposema tukipendana Mwenyeezi Mungu atashusha baraka zake! lakini ili tupendane na kuheshimiana unashauri nini kifanyike kwasasa? maana mapenzi na heshima kwasasa hakuna tena! tumekuwa kama mijibwa inayofoka ndani ya geti la chuma huku kila mmoja anasubiri bwana ake afungue geti ili waparuwane!
 
Hapa kuna walakini na usalama wa wahusika, kwanini wasingesubiri makovu ya Arusha yakauke miongoni mwa wakristu dio hukumu ikatoka? hali kama hii itazidisha maswali miongoni mwetu juu ya juhudi za serikali kuzika mitafaruku ya kidini. siungi hoja mkono kamwe!

MMTEULE;

Kwani Sheikh Ponda anauhusiano gani na milipuko ya Kanisa huko arusha? nijuavyo alikamatwa na kushtakiwa na Serikali kwa uporaji wa kiwanja cha Jumuiya moja ya Serikali inayoitwa Bwakwata! mbona sikuelewi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom