Ponda inabidi apime kipi muhimu. Kati ya pesa anazopewa na Waarab au utanzania kwanza
Dokta Makende usiki yaho:-
*Asema mkakati wa kukamatwa kwake uliandaliwa
Sheikh Ponda Issa Ponda
SIKU moja baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mjini Dares Salaam, kumwachia na kumweka chini ya uangalizi wa mwaka mmoja Katibu Mkuuwa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda,jana aliibuka na kusema umefika wakati wa Waislamu kufanya uamuzi mzito.
Akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu, baada ya swalaya Ijumaa katika Msikiti wa Mtambani, Dar es Salaam, Sheikh Ponda, alisema hatua ya yeye kuwekwa ndani kamwe haitamkatisha tamaa na kurudi nyuma katika mapambano ya madai ya Waislamu nchini.
Alisema kutokana na hali hiyo, kwa muda mrefu Waislamu wamekuwa wakinyanyaswa kinyume cha sheria, wakati wana madai ya msingi ndani yataifa lao.
Alisema hatua yeye kukamatwa, ni wazi ilikuwa ni mkakati maalum unaoratibiwa na Serikali, wenye lengo la kuwafunga midomo masheikh waKiislamu ili wasiseme jambo lolote ambalo ni manyanyaso kwa jamii yao.
Ni wazi hivi sasa, hawa wenzetu wanapigana nasi kitaalamu kwa kutunyamazisha midomo, kamwe hatuwezi kurudi nyuma. Hali ya Waislamu ni nzitona tunahitaji kufanya maamuzi mazito.
Ni wazi kabisa, ninataka kulisema hili lieleweke kuwaUislamu wetu hauko kwa ajili ya Katiba, wala Utanzania wetu, bali ni kwa ajiliya asili ya dini yetu tu.
Kwa muda mrefu, walikuwa wakifanya mikakati ya kunishughulikia eti sio raia wa Tanzania,niliwajibu wazi pale Mtoni kuwa hakuna mtu yeyote wa kuniweza kuninyanganya.Na sasa wamebadili mfumo wa kutushughulikia masheikh kwa kesi za uongo.
Ninataka kuwaambieni ndugu zangu, Waislamu hatutarudi nyuma, iwe katika amani au mapambano, ili mradi tu tuweze kuisongesha mbeledini ya Allah (Mwenyezi Mungu), alisema Sheikh Ponda.
Maisha yagerezani
Alitumia mkusanyiko huo, kusimulia maisha aliyokumbana nayokatika gereza la Segerea.
Alisema aliweza kushuhudia mambo mengi, yakiwamo ya watu wengi kuwekwa mahabusu bila kesi zao kushughulikiwa.
Walipo nikamata walinipeleka katika gereza la Segerea nakuniweka selo ya watoto, ambapo alikuja mtoto mdogo ambaye nilimuhoji na kusemaana umri wa miaka 10.
Katika hali ya kushangaza, mtoto yule alisema amewekwa ndani kwa sababu ya tuhuma za kuiba pochi iliyokuwa na Sh 40,000.
Kama iliwezekana kwa mtoto huyo kukamatwa, imekuwaje kwa mtoto aliye kojolea Koran pale Mbagala Oktoba 10,mwaka jana, hadi leo hajakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Leo hii, kwa mujibu wa takwimu zetu zinaonyesha magereza mengi na makaburi nchini yamejaa masheikh ambao kila mara wamekuwa wakifikwa namadhila ya kesi za kusingiziwa.
Leo kina Sheikh Farid, Mselem hadi leo hii maskini ya Mungu wamewekwa ndani kwa kesi za kusingizia tu, ila Mbeya yametokea machafuko katiya Wakristo ambao walichoma msikiti, lakini hadi leo hii hakuna hata kiongozi aliyefikishwa mahakamani.
Wakati akiyasema hayo, waumini wa dini ya Kiislam kila marawalikuwa wakikubaliana na maelezo yake kwa kutamka Takbir ... Takbir neno lenye maana kwa lugha ya Kiarabu Mungu mkubwa.
Juzi Mei 9, mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimtia hatiani Sheikh Ponda na wenzake 49, ambao waliachiwa huru katika kesi iliyo kuwa ikiwakabili.
Washtakiwa hao, waliachiwa huru na Hakimu Mkazi wa Mahakamaya Hakimu Mkazi Kisutu, Victoria Nongwa.
Katika kesi hiyo, upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Wakiliwa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka na upande wa utetezi uliwakilishwa naWakili Yahya Njama.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Nongwa alisema: Jamhuri imeshindwa kuthibitisha mashtaka kuanzia shtaka la kwanza, tatu, nne na la tanokwa washtakiwa wote, katika mashtaka hayo washtakiwa wote kuanzia wa kwanzahadi 50 hawana hatia.
Katika shtaka la pili la kuingia kwa nguvu katika Uwanja waMarkaz Changombe, upande wa mashtaka umeweza kuthibitisha kwamba Pondaaliingia kwa nguvu, hivyo anatiwa hatiani kwa kosa hilo.
Shtaka la kuingia kwa nguvu halielezi adhabu inayostahili kutolewa, lakini mahakama inaweza kumpa adhabu ya kifungo cha miaka miwili jela au faini au vyote kwa pamoja.
Kwa mshtakiwa wa kwanza (Ponda) hakuna kumbukumbu kwamba nimkosaji wa makosa mengine
mahakama inazingatia pia mshtakiwa alikaa rumande kwa muda mrefu kuanzia Oktoba 18 mwaka jana hadi leo, hivyo inamwachiwa kwamasharti.
Alisema mahakama inamwachia Ponda kwa masharti ya kulindaamani, awe mwenye tabia njema kwa miezi 12 na endapo atashindwa atarudi mahakamani apewe adhabu nyingine inayostahili.
SOURCE MTANZANIA
Last edited by tunduruboy; Today at 11:11.
Sasa umeng'ng'nia warabu warabu nenda kamuulize!!