Pongezi CCM, kwa Ushindi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Pongezi Pia Upinzani kwa kidogo mlichokipata, muwe na shukrani ili 2025 mpatiwe kikubwa!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Makala yangu gazeti la Nipashe ya leo 01/12/2024.

Paskali
 
Wanabodi,
Makala yangu gazeti la Nipashe ya leo 01/12/2024.
View attachment 3166742
Paskali
Nimebaki mdomo wazi kwa namna kaka Paschal ulivyopanga maneno mengi kana kwamba haujui kilichotokea, kuna mtu aliwahi niambie wewe ni kada. Mwanzo nilidhani wewe ni mwandishi wa habari mbobezi unayeweza kusema nyeusi kuwa nyeusi na si vinginevyo. Kwa makala hiyo umejipambanua kuwa wewe ni kada mtiifu. Mwanzoni wakati mwenda zake anaingia ulionesha kaukomavu kidogo, naona sasa umekubali yaishe. Haya Bwana hayo ni maisha na maamuzi yako binafsi, ila umenivunja moyo sana. Kwaheri HAKI karibu dhuluma
 
nimecheka pale unapo sema kwamba 2019 kulikuwa na uchaguzi

we nyooka si 2019 wala 2024 hapakuwa na uchaguzi bali maigizo na upumbavu wa ccm

cha maana umezungumza ni hakuna tume huru bali mabadiriko ya jina tu mengine ni upumbavu tu
 
Kaka Pascal Mayalla itafika kipindi maandiko yako yatatoa majibu wapo wanakusema Ila mara nyingi unaandika fact CCM wanaweza wakawa wanacheza rafu lakini ukweli aina ya Siasa za Upinzani inawafelisha kwa kiasi kikubwa kuchukua madaraka they are not organized, poor team work and poor strategic plans Kama wataendelea kujificha kwenye mgongo wa kusema wanaibiwa kura bila kujitathimini wao kama wataendelea kushindwa uchaguzi miaka yote.
 
Pascal Mayalla uliheshimika sana kwa mijadala ya kina, uchambuzi makini na uandishi wa masuala ya kisiasa na kisheria bila woga. Hukuwa na chembe ya ubabaishaji wala uchawa.

Lkn kwa sasa unaandika maandiko ambayo mtu akisoma kichwa cha habari tu anaona jinsi ulivyoathirika na kupoteza weledi wa uandishi. Umepoteza hata hadhi ya kuitwa mkongwe wa uandishi wa habari.

Unawezaje kutoa pongezi kwa uchaFUzi huu? Unapata wapi nguvu ya kuwataka wapinzani washukuru kwa kidogo walichopata na kusema wawe na shukurani?? Kwamba wewe hukuziona hizo rafu walizochezewa??

Nilitegemea uwe wa kwanza kukosoa mwenendo mzima wa uchaguzi na kuzisulubu mamlaka kwa kuandika ukweli wa mambo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…