Pongezi kwa kubuni mitihani ya mchujo na interview, naiona dalili ya Tanzania yenye weledi (meritocracy)

Pongezi kwa kubuni mitihani ya mchujo na interview, naiona dalili ya Tanzania yenye weledi (meritocracy)

Uhakika Bro

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2022
Posts
3,644
Reaction score
4,315
Naanza na pole kwa watu wa maabara kwa kupewa mitihani ya watoto wa shule wakati ninyi tayari ni watu wazima wa kazini.

Nimeona niandike thread hii kabla sijafanya mtihani hiyo ili nije niisome tena nijicheke baada ya mtihani🤫😁. Bado hayajanikuta.

Inapendeza, sasa badala ya kuchagua mtu kwa kuanzia na sijui jinsia, mara umri na hali ya afya (uzima na ulemavu) kama sifa ya kwanza sasa sifa ya kwanza kabisa imekuwa ni KUFAULU MTIHANI wa nafasi husika ✅✅.

Halafu baada ya kufaulu tukawa na uhakika kwamba hao wanaoenda kushindana kwenye oral ndio 'one of the best men/women for the job' ndio waangalie vigezo vingine. Naona ni kitu nzuri tu.

Hiyo ndio dhana ya weledi (meritocracy) yaani imelenga kuwapata wataalamu wenye weledi kwa kazi husika. Kabla ya kuangalia mambo mengine tunawachukua watu sahihi kabisa kwa kazi kwa kutumia mbinu inayoweza kuleta matokeo sahihi (pragmatic) na mengineyo.

Natamani sana kujua kama kuna takwimu za waliofaulu, wa kike na wa kiume ni wangapi? Sijui hizi data nani anaweza zichakata ukizingatia namba ya mtu ni siri. Kama vipi waitoe takwimu bila namna ya kumjua muhusika (anonymyty) watuwekee tu tulipata madaktari wa kiume watatu (30%) na wa kike saba sawa na asilimia 70%

Nikifanya mtihani alama zangu au za wenzangu zisipotosha kuitwa viva/oral interview basi ntasema tu kama wazungu "may the best man/woman win" 👊. Nakubaliana na ukweli tu kwamba miaka ya kukaa mtaani imesahaulisha mambo ya shule.

Soma Pia: Kimetulamba kwenye written interview😂

Tujitahidi kuona upande chanya wa jambo kila mara.

Mbarikiwe.
 
Watu wamemaliza chuo kitambo sana wamesahau sasa mjue kwanini kada zingine walikuwa wanakosa kazi. Wanesahau, wanatoa maswali tofauti, au yale wasiyotegemewa kabisa.
 
Naanza na pole kwa watu wa maabara kwa kupewa mitihani ya watoto wa shule wakati ninyi tayari ni watu wazima wa kazini...
Unachagua watu wa kwenda kufanya upasuaji kwa kubeti/ tossing coin mkuu hebu kuwa serious
 
Wengi wanachoshindwa kuelewa NI kuwa interview siô njia Sahihi ya kupata Watendaji Bora Ila NI mchujo kama ilivyomitihani mingine.

Imelenga zaidi kwèñye Cognitive domain ya wahusika badala ya utendaji wa wahusika.
Huwezi pima utendaji wa wahusika Kwa interview ya Siku Moja.

Kumbuka interview NI sehemu assesment.

MTU anaweza akapata A lakini kwèñye utendaji akashindwa na aliyepata C
 
Wengi wanachoshindwa kuelewa NI kuwa interview siô njia Sahihi ya kupata Watendaji Bora Ila NI mchujo kama ilivyomitihani mingine.

Imelenga zaidi kwèñye Cognitive domain ya wahusika badala ya utendaji wa wahusika.
Huwezi pima utendaji wa wahusika Kwa interview ya Siku Moja.

Kumbuka interview NI sehemu assesment.

MTU anaweza akapata A lakini kwèñye utendaji akashindwa na aliyepata C
Unashauri wafanyaje sasa?
 
Exactly. Mtu ameajiriwa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kwa zoa zoa. 8 years later anahamia NIMR kama "technical officer". Hakuna merits wala competence.​
 
Watu wamemaliza chuo kitambo sana wamesahau sasa mjue kwanini kada zingine walikuwa wanakosa kazi. Wanesahau, wanatoa maswali tofauti, au yale wasiyotegemewa kabisa.
Sasa jomba interview itakua na maana gani ikiwa utataka upewe kile wewe unakijua ili ufaulu.

Kile ni kipimo, zimo au hazimo, kukaa kwako mtaani na kusahau mambo ya shule hakuwahusu wao.
 
Watu wamemaliza chuo kitambo sana wamesahau sasa mjue kwanini kada zingine walikuwa wanakosa kazi. Wanesahau, wanatoa maswali tofauti, au yale wasiyotegemewa kabisa.
Kwahy ulitaka uletewe maswali unayoyajua?
 
Kuna nini tena humu. Mbona watu wanalalamikia mitihani ya PSRS?
 
Back
Top Bottom