Pongezi kwa mdada Mentor Cherry, muathirika wa VVU anayetoa elimu kuhusu masuala yanayohusu VVU

Pongezi kwa mdada Mentor Cherry, muathirika wa VVU anayetoa elimu kuhusu masuala yanayohusu VVU

KJ07

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2021
Posts
2,370
Reaction score
5,381
Salaam Wakuu,

Katika pitapita zangu za hapa na palehuko mjini instagram nimekutana na mdada mmoja ambaye ameni inspire sana kutokana na kitu alichoamua kufanya kwa jamii ya watanzania. Jina lake halisi sijalifahamu bado ika la instagram ni Mentor_Cherry.

Sasa kwa harakaharaka nimegundua kuwa ni muathirika wa VVU na ameamua kuliweka wazi hilo mbele ya jamii na nadhani ni kwa ajili ya kuongeza uelewa kwa jamii hasa juu ya masuala yanayohusu VVU.

Miongoni mwa post zake kuna ambayo anatoa taarifa juu ya uwepo wa tabia ya manesi (CTC) ya kuwanyanyapaa waathirika wa VVU wanapoenda kuchukua madawa ya kupunguza makali ya VVU. Video zake nyingi zina contents hizo na shuhuda mbalimbali za watu wakimtaja kama mtu aliyewabadilisha kimtazamo hasa waathirika wa VVU.

Pia nimeona post moja akiwashauri wadada wa vyuoni kuacha kujirahisisha kwa wababa kisa pesa na mwisho wa siku wanaingiliwa kinyume na maumbile jambo ambalo linachangia maambikizi ya VVU kwa kiasi kikubwa.

Natamani tuwe na watu wengi kama yeye ambao wanachukulia changamoto za kiafya in a positive way ili kupunguza athari zitokanazo na hofu ya magonjwa.

Ni hayo tu wakuu wa JF.

Hii ni moja ya post zake ambayo imeniinspire sana.

 
Amejizima data maisha yanaenda...

Kwenye maisha kuna wakati data lazima uizime ili utoke kimaisha ..

Zama hizi hela ipo kwenye content na umaarufu social media..

Unapopata followers wengi unapata dili za hela nyingi kuliko kuajiriwa ofisini mshahara laki kazaa ama milioni 1

Mwijaku na upuuzi wake kwa mwezi anatengeneza zaidi ya milioni 10

MC garab na content zake za harusi za kishua kwa mwezi anatengeneza zaidi ya milioni 20. Maana kila mpenda show off anataka ampe kazi Garab ili apostiwe kwenye page yake
 
Zama hizi hela ipo kwenye content na umaarufu social media..

Unapopata followers wengi unapata dili za hela nyingi kuliko kuajiriwa ofisini mshahara laki kazaa ama milioni 1
Kuna watu wananunua hadi follower's ili wawe na watu wengi...

Nimeshuhudia mtu kanunua Instagram 10k kwa elfu 40 tu...
 
Kuna watu wananunua hadi follower's ili wawe na watu wengi...

Nimeshuhudia mtu kanunua Instagram 10k kwa elfu 40 tu...

Followers peke yake hawakutoi.

Muhimu ni content zako. Yaani maudhui yako unayopost.. je yanapendwa na watu ?

Maudhui ndio yana ku brand na kukufanya upate dili za matangazo na kupewa dili za ubalozi.

Hata ukinunua account yenye followers milioni 10. Wewe ukawa Huna maudhui yanayopendwa inakula kwako
 
Asanteni moderators kwa marekebisho
 
Back
Top Bottom