Pongezi kwa Serikali kwa kuanzia kutekeleza Ugawaji wa Vishikwambi kwa Walimu

Pongezi kwa Serikali kwa kuanzia kutekeleza Ugawaji wa Vishikwambi kwa Walimu

njwanjwanjwa

Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
8
Reaction score
11
Mapema wiki hii inayoishia, nimefurahi sana kuona Serikali ikigawa bure kwa walimu wa VETA vishikwambi ( tablette) vilivyokuwa vinatumika ktika zoezi la Sensa la mwezi Agasti.

Baada ya zoezi la Sensa kutamatika, Serikali hii tukufu ya Mama Samia iliahidi kugawa vishikwambi vilivyokuwa vikitumika kwa watumishi wa sekta ya Elimu kuanzia vyuo vikuu, vyuo vya kati na hatimae kwa walimu na maofisa wa Elimu sekonsari na msingi.

Nilipoona wakufunzi wa chuo cha ufundi cha Veta iliyokaribu na mimi wamepatiwa vishikwambi, nikajisemea moyoni kuwa basi…hata yule mwaliku wa shule ya Msingi Namtumbo kule Songea nae anaenda kumilikishwa na Serikali mishikwambi muda si mrefu.

Aidha, binafsi hili ni jambo la kupongezwa sana tena sana kwa Serikali si tu kwa kuwakumbuka walimu na kuwapa bishikwambi vilivyokuwa vikitumika wakati wa Sensa la hasha! Bali kuwawezesha nyenzo ya kufundishia kisasa kwa kuendana na mabadiriko ya kasi ya sayansi na Teknologia.

Mimi kama Mwalimu wa Taifa hili pendwa, nasema Asante sana Serikali yangu kwa hili🙏

7E510E92-6ECE-4721-A10D-6C6C928185FD.jpeg
 
Kwa taarifa yako kauri ya Waziri Mkuu aliyoitoa siku anazindua ugawaji wa vishikwambi pale Dodoma Desemba 4, 2022 inapingana na kinachoendelea sasa. Leo asubuhi nilikuwa naongea na rafiki yangu mmoja ambaye yuko idara ya uthibiti ubora halmashauri x , amesema si walimu wote waliopewa . Katika halmashauri yao wamegawa vishikwambi 7 kwa kila shule. Kwa mantiki hiyo walimu wengi wamekosa shikwambi .

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Nyie mmepewa hivyo, sisi kaka nape anatupa simu tujichagulia wenyew
 
Ilitakiwa NECTA iwe na website malaumu ambapo teaching and learning materials yatakuwa humo. Mwalimu anapakua kitabu kwenye website anaprint
Kila shule ilitakiwa waweke
1. Desktop computer 4 au 5 na Laptop 3
2. Printer mashine
3. Photocopying machine
4. Internet access
5. Projector
Hivyo vishikwambi vitageuka kuwa mali ya mtu binafsi.
 
Back
Top Bottom