GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
- Psychological Blow baada ya Kuumizwa vibaya kwa Mshambuliaji Salah
- Schoolboy Goalkeeping kutoka kwa Kipa Karius kwa Kujifunga
- Squad Gambling kutoka kwa Kocha Klopp
Zinedine Zidane alifanikiwa akiwa kama Mchezaji na sasa anatuthibitishia kuwa hata katika Kazi / Jukumu la Ukocha bado pia anabakia kuwa Galacha / Nyota hivyo kama inawezekana basi Waandaaji wa michuano ya UEFA Champions League pamoja na FIFA kwa ujumla wafikirie kuandaa Tuzo ya Kocha bora wa Dunia ambayo sidhani kama hiyo Tuzo ikianzia kwa ' Zizou ' kuna Mtu atakayelalamika au kuhoji.
Hongereni sana mlioshinda ila binafsi kwa machungu makubwa niliyonayo sioni dalili zozote kwa Mimi Kuupata Usingizi kwa muda huu hivyo nashindwa kujua itakuwaje leo kwani Jurgen Klopp ametuchanya sana na aina ya Upangaji wake wa Kikosi kwa leo.
Nawasilisha.