Pongezi Mhe. Spika Kuliongoza Vyema Bunge Letu, ila Sio Busara Kutumia Bunge Kujibu Trivia Issues za Mitandaoni, Zina Downplay Hoja Rasmi za Msingi!.

Wachache sana tunaokuelewa mkuu Paskali..nasikitika kuona bado kuna watu wanaendelea kukuhukumu na lile bandiko lako la April mosi..ambalo kimsingi lilisadifu maudhui ya ile siku yenyewe,hata hivyo nikirudi kwenye hoja yako ya msingi ya leo iko wazi bado kuna shida kwenye inshu ya mawasiliano hasa kwa watendaji wa serikali wenye dhamana..na ndio maana hata leo waziri mkuu akachomekea inshu ya kutoa taarifa za corona kienyeji badala ya kutolewa na wenye mamlaka ya kufanya hivyo.
 
Wengi mnaomlaumu paschal kuhusu yote laiti mnngeshudia hata dk 10 za mahojianomahojiano kwenye kamati ya maadili mngenyamaza.

Naona aliandika mahali ni bora kunyamaza kuliko....


Pole mayalla endelea kupambania ubaba wa wanao ndani umma WA watz. Si rahisi lkn vumilia ukishindwa nyamaza najua si rahisi mwanahabari na PGDwa sheria kukubali kunyamaza kirahisi.

For the benefits of ur children nyamaza, kumbuka, karibuni wataanza kusoma jf. Hata kama wako lockdown huko...... Nyamaza labda utaokoa vilivyo na thamani kwako inaweza kuwa ulivyopoteza au unavyokaribia kupoteza.
 
Hakika serikali ya awamu ya tano inastahili pongezi kila uchwao ,hii ni kutokana na mambo mazuri yanayofanywa na government yetu katika kutatua changamoto zinazomkabili mwananchi,JPm for 2020-2025

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii serikali ni kiboko hadi imeweka hewani mitambo ya kufyonza virusi vyote vya corona vinavyoingizwa nchini,awamu ya tano ni fire
 
Ningekuwa na uwezo nisingeruhusu msukuma na mgogo kupewa madaraka makubwa
 
Siweki andiko lolote mpaka niwe na uhakika Job aliongea nini. Maana kama taifa tunachangamoto nyingi sana. Ila kwa ulimwengu wa leo social media ndio reliable source of info. Mimi naishi Nyakagwe lakini nafanaya interaction na dunia nzima na watu wanatoa true info.
Enzi za kupata info toka vijiwe vya kahawa, bar na vilabuni zimepitwa na wakati.
Tujifunze kwa nchi kama China, Us na zinginezo. Na uzuri sasa hivi kila laini imesajiliwa kwa kitambulisho cha Taifa.
Nipo Nyakagwe kuna mtu kachafua baa kwa kreti kama kumi.Mengineyo ni siri.
Kesho.
 
Paskali natambua nafasi yako kama verified user, sihitaji kukulaumu kama ww kwani najua hali halisi. Ila hizo sifa ulizompa Ndugai ni kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa kutokana na ID yako. Unasema huku mitandaoni tunajadili trivial issues, ukweli ni kuwa kwa sasa humu mitandaoni ndio kulikobaki huru, tunapoweza kusikia issue za kweli, huko bungeni ndio hiyo ulisikia wapinzani wamegomewa kusoma hotuba yao, kwa sababu zinazomfurahisha Ndugai na anayemtumikia.

Ndugai ameamua kujibu habari za mitandaoni, sio kwa bahati mbaya, bali huku mitandaoni ndiko anakokutana na hoja za kweli zinazomuumiza, hivyo hana jinsi zaidi ya kuzijibu. Kumbuka huku mitandaoni hawezi kuja maana huku anajua fika atakutana na ukweli mchungu, na yale madaraka anayoyatumia vibaya kule bungeni, huku hana nguvu hizo, zaidi ya kupendekeza jukwaa lifungwe, na hata akipendekeza lifungwe, bado mitandao ni mingi sana na tutahamisha huko hata kwa VPN. Hivyo hayo mafuta unayompaka kwa mgongo wa chupa, ni vyema tu ukamwambia cheo ni dhamana na madaraka yana mwisho.
 
Dah! Hizi njaa hizi.
Hv huyu jamaa na yeye ni mtu mzima, ana mke na watoto wanamuita baba kabisa ndio anakuja kuandika hizi shombo!?
Hv viapo mnasema mmekula kusema na kuandika ukweli huwa mnaapa mbele ya shetani !?
Mambo mengine ni afadhali kukaa kimya kulikoni kuendelea kujidhalilisha kiasi hiki.

Hii nchi inastahili zaidi ya haya tunayoyaona na unayoyasifia.
Nyie mnaojitoa ufahamu na kujikuta mnamsifia mfalme Juha ndio mnaozorotesha hali ya hii nchi. Kama huwezi kuwa mkweli na muwazi, kaa kimya. Njaa zako zisiwe kero kwa wengine, tunahitaji wapambanaji na watafuta mabadiliko na sio waimba ngonjera na wapiga debe.


"I love my country but i'm ashamed of my government"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naamini pascal ana point nzuri sana, tatizo unamuona kama kibaraka... hata aongee mazuri, huji kumuelewa.
 
Nadhani Mh. Ndugai yuko sahihi, kila mmoja ametumia platform yake

 

Ni kweli bora angekaa kimya tu kuliko kuleta sifa za kumsifia mtu asiye na maana yoyote. Kimsingi watu wana uelewa mpana, unapoleta sifa za kijinga bandiko lote linaishia kupuuzwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…