Pongezi Rais Magufuli na Awamu Yake ya Tano, Wafanya Maajabu Vita Dhidi ya Umasikini, Tanzania Yaongoza Dunia Kupunguza Umasikini Uliotopea-WB.

Hivi Wanyonge ndio hao hao Masikini, au haya ni Makundi mawili tofauti?
Yes wanyonge ndio hao masikini. Watanzania wengi wana mashamba na mifugo ambazo ni rasilimali, lakini bado wanaishi kinyonge na kwenye umasikini uliotopea kwasababu hizo rasilimali zao, hazijarasimishwa ni assets tuu lakini hawawezi kuzi turn in current assets, TASAF inagawa fedha hard cash kunusuru kaya masikini, wakati MKURABITA, unarasimisha rasilimali na biashara za wanyonge kuwa rasmi kuwaweza kuzi turn in current assets.
P
 
Unadhani watanzania wanapenda kukuona unapanda jukwaani na makaratasi kuwasomea data za uchumi, hiyo ni credit tu kwa Wasomi ambao hata si wapiga kura?

Wao wanataka kuona mkate wa kila siku unapatikana.

Hata kama nchi ingekuwa imetoka kwenye umasikini, ikiwa watu bado hawawezi kula vizuri, hawamudu gharama za matibabu, hawana maji safi huna maana yoyote kwao.

Kitu kikubwa ni lazima viongozi wasiyabane sana maisha ya watu kwa visingizio vya miradi mikubwa. Lazima wabalance na bajeti ili maisha ya kawaida yaendelee

Ni sawa na baba anatumia 90% ya mapato pamoja na mikopo juu kununua gari akitegemea aendeshe mradi biashara isipokuwa ya ufanisi maisha ya familia lazima yatetereke, madeni ndiyo kabisa yatasababisha hata kuuzwa kwa asset

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaka chakula ambacho hujapika hustahili kupewa pongezi kwa kuwa kitamu au ni kama kusifiwa una mtoto mzuri wakati mimba ni ya mwingine. Bro hata kuona huoni kwamba bado miaka 4 mpaka yeye akaingia madarakani? I knew you as a person who will give credit when it is due and criticism when it is also due. Today i think you put all those to rest with on one JF writting. Giving credit for something someone doesn't deserve.
 
Kaka chakula ambacho hujapika hustahili kupewa ppongezi kwa kuwa kitamu
Mgeni anapokuja nyumbani, akala akashiba, anamshukuru mwenyeji. Hata house girl wa Kitanga, akipika mahanjumati kama samaki wa nazi wa kupaka kwenye familia ya Wachagga, mgeni akila na kufurahia chakula pongezi ni kwa mama mwenye nyumba wa Kichagga na sio house girl wa Kitanga.

Hata tulipokaribishwa Ikulu, ile ni nyumba yetu, wafanyakazi tunawalipa sisi, chakula tunanunua sisi, wapishi tunawalipa sisi, bado tukila tukashiba, tunamshukuru mwenyeji wetu.

Any credits kwa Tanzania ya sasa, pongezi ni kwa the current regime.
P
 
Makala zako ndefu hazina mvuto ni Yale Yale tu. Badilisha style ya uandishi
 
Makala zako ndefu hazina mvuto ni Yale Yale tu. Badilisha style ya uandishi
Mkuu Mliberali, nimekusikia, nitabadilisha
Ila nisaidie nitumie styles gani ili makala zangu ziwe na mvuto, niandike kama nani?, Mkuu Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Maalim Mohammed Said, St. Ivuga, Mag3, Mliberali au niandike kama nani ziwe na mvuto?
P
 
Mkuu Masiya, katika mashindano ya kuondoa umasikini uliotopea iliyochapishwa mwaka huu, inaonyesha Tanzania ndio inaongoza duniani!. Hata kama data ni za zamani, data hizo ndizo ime Tanzania uongozi mwa mwaka huu!.
P.
Pascal umetumia hiki kipengele kutueleza ulicho tueleza "Where has extreme poverty declined the most?
Average of total extreme poverty percentage points change over the circa year 2000-15 (start year - end year), top 15 countries". Data hiyo inaonyesha wamelinganisha 2015 misho (end of year) na 2000 mwanzo (start year). Hivyo data hiyo inawaruhusu kuzungumzia mabadiliko kwa wakati huo. Kama ni hivyo hata kama report ni ya 2019 ukweli ni kuwa reporting period ni 2000-2015. Na kwa period hiyo Tanzania imepunguza umasikini kwa 3.2 "best" performance kwa kipindi hicho. Itakuwa ni makosa wewe kusema in 2019 Tanzania ilipunguza kwa 3.2. usahihi ni kuwa kwa report ya 2019 katika kipindi cha 2000-2015 Tanzania imepunguza kwa kiwango cha 3.2 ikipita nchi nyingine ilizolinganishwa nazo. Sasa kana kwamba haitoshi wewe uka ATTRIBUTE hiyo reduction na awamu ya Tano-hili ni kosa kitaaluma. Ukimpongeza JPM umpongeze kwa niaba ya awamu husika. Interpretation yako siyo sahihi kitakwimu.
 
Na hapa ndipo tulipofika.Gone are the days JF ilipokuwa kisima cha maarifa.
 
Mkuu Mliberali, nimekusikia, nitabadilisha
Ila nisaidie nitumie styles gani ili makala zangu ziwe na mvuto, niandike kama nani?, Mkuu Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Maalim Mohammed Said, St. Ivuga, Mag3, Mliberali au niandike kama nani ziwe na mvuto?
P
Soma tena para ya mwisho ya bandiko lako, umeandika mipasho bro.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…