Nina wasi wasi na "usomi" wa mtoa mada. Bilashaka ni "postgraduate" ambaye hajajifunza maana na matumizi ya "prospective na retrospective studies".
Nashauri si vizuri kuanzisha mjadala wa somo usilolijua kwasababu unaweza kuishia kupotosha au kujidhalilisha.
Lakini unaposhindwa kuelewa ripoti ya kitaaluma (kisayansi) ni kudhihirisha kuwa "masters" uliyonayo haina msaada kwako kwakuwa mtu wa kiwango hiki anatarajiwa awe amejifunza mbinu za kufanya utafiti (research methods) na kuchambua na kutafsiri takwimu (data analysis and interpretation (statistics)) bila kujali taaluma (profession) uliyosomea.
Report inayongelewa ni Miata 2000 Hadith 2011 lakini pongezi ni za rais wa 2015 ha 2019. Hapa rais Magufuli anapongezwa kwa jambo gani Au ni staili ya sasa ya kupongeza kwa kila kitu. Kwa hili la umasikini tusubiri report ijayo tuone kama umeendelea kupungua au umeongezeka. Kupunguza umasikini ni lazima kuekeza raslimali katika kilimo, ufugaji na uvuvi kwa wakulima, wafugaji na wavuvi wadogo wadogo ambako ndiko umasikini uliko. Sasa
swali la msingi ni raslimali kiasi gani imeelekezwa katika sekta ya Kilimo, na tutegemee umasikini utakuwa unapungua au unaongezeka..
Hahaha hii nchi huwa tunaongoza kila kitu, Juzi nilisikia tunaongoza Uchumi kupanda East, south and central Africa. Leo Tunaongoza Kupunguza umasikini, kesho tutaongoza nchi tajiri afrika, NA UTASIKIA TUNAONGOZA KUWA NA WAGONJWA WENGI WENYE KWASHIORKOR.
Huwa sishangai siku hizi maana takwimu zetu ni kuongoza tu.
Mie amenifurahisha sana! Kawakusanya na kuwakoroga, kisha kawaacha hawaelewi wafurahi, wasikie aibu au wamshambulie Pasco!
Zamani sikuwa ninaelewa neno 'kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa' au hadithi ya joho la mfalme, lakini siku hizi ndio nimeelewa kwa mifano dhahiri.
Ripoti hiyo ni sifa kubwa kwa utawala wa Magufuli. Kweli ni 'jembe'
Nafikiri tunalingalia hili jambo kwa nia tofauti. Huwezi ukampa credits JPM kwa kitu ambacho hakufanya yeye, likewise huwezi kumlaumu kwa kitu ambacho hakufanya yeye. Kwa miaka yote ambayo nimeona maandiko kama haya (ndani na nje ya vyuo) kwa kweli sijaona interpretation na attribution kama yako. Credits zinatakiwa kwenda kwa yule aliyefanya, kiungwana ungesema namuomba raisi wetu afikishe kongole zetu kwa........ Mfano wako wa kitanda hakizai haramu na Tetemeko la Bukoba siyo sahihi. JPM alilaumiwa sio kwa sababu tetemeko lilitokea wakati wake bali kwa sababu (right or wrong) watu walifikiri response yake haikuwa sawa.
Mkuu Masiya, katika bandiko hili, tunsbishania vitu viwili tofauti.
1. Report ya World Bank ya Mwaka 2019 ikionyesha Tanzania ndio inch inayoongoza duniani kwa kupunguza umasikini uliotopea.
2. Date of data collection.
Taarifa yoyote kuhusu jambo lolote inayoihusu Tanzania inahesabiwa kwa siku inapotolewa, the date of release na sio the date of data collection.
Jambo lolote zuri au baya kwa Tanzania, linapotangazwa, credits or blames ni kwa the current regime wakati jambo hilo linapotangazwa na sio data zilikuwa collected lini.
Hii ni World Bank Report ya mwaka huu 2019 imekuwa released December hii 2019, hivyo ni sawa na haki kwa credits kwenda kwa utawala uliopo at the time of publication.
Watu wanaofanya Ph.D by thesis wengine huchukua hata miaka 10 wakifanya research lakini Ph.D zao zinahesabika kuanzia pale wanapo publish kazi zao.
Tanzania tuna tatizo kubwa sana kusoma tafiti za data na kutafsiri. Mfano mzuri ni Ripoti ya CAG ni liripoti limoja likubwa full of data. Media yetu haina uwezo wa uchambuzi wa kutosha kuwatafunia Watanzania kila kilichomo hivyo hufanya cherry picking on few areas of interest ndio wana report.
Wabunge wetu mule wengine ndio hao darasa la 7 unategemea nini kwenye data kama zile.
Mfano kwenye report ya CAG ya 2016, CAG amezungumzia madeni ya nje na the risk associated na kutolipa madeni hayo ni mpaka ndege zetu zilipokamatwa ndipo kuna watu wakajifanya kuanza kushangaa!.
Wanabodi, Hili ni bandiko kuhusu kitu very serious kuhusu mustakabali wa taifa letu na vipaumbele vyetu ambapo CAG Prof. Mussa Asad amekisema!. Kama hii ni kweli, then, this is not right at all, hivyo kama mambo yenyewe ni haya, hala hala huko mbele tusije tukashikana mashati, swali linabaki...
www.jamiiforums.com
Kwenye bandiko hili, nimeiweka report yenyewe, very few or nobody bothered to read the report and understand it but most are very first to criticise!.
Wajameni someni report.
Tanzania ilipata uhuru wake mwaka 1961. Kila sherehe ya uhuru anayepongezwa ni rais aliye Madarakani kwa mwaka huo. Naamini wengi mnasoma salamu mbalimbali za pongezi kwa rais Magufuli kusheherekea Uhuru na Jamhuri, rais Magufuli anapongezewa nini kwani ndiye yeye aliyeleta uhuru?.
Vivyo hivyo japo utafiti umenywa kwa kipindi kilichopita, Tanzania ndio imeongoza kwa mwaka huu wa ripoti ilipotoka na sio mwaka ule wa utafiti.
Tujifunze kutofautisha Tafiti na Ripoti.
Mfano inawezekana kabisa ukafanyika utafiti wa literacy levels za nchi za Africa Mashariki kutokana na Tanzania kuwa na population kubwa, Tanzania tunaweza kujikuta ndio tunaongoza kwa low literacy levels kwasababu kipindi cha Mkapa na Kikwete elimu ililipiwa. Sasa kipindi cha Magufuli anatoa elimu bure. Ripoti hiyo ikitoka na kuonyesha Tanzania ndio tunaongoza kwa vilaza, nani atazomewa?. Atakayezomewa ni Magufuli!. Na rais Magufuli akizomewa kwa vile yeye anatoa elimu bure, hivyo aibuke na kukanusha ripoti hiyo kwa kusema hao vilaza kwenye ripoti hiyo ni vilaza wa Mkapa na Kikwete, yeye hana vilaza kwasababu anatoa elimu bure?.
Ripoti ya Tanzania kuwa nchi kinara kupinguza umasikini uliotopea ni ripoti ya mwaka huu 2019, pongezi ni kwa Magufuli.
P
Vivyo hivyo japo utafiti umenywa kwa kipindi kilichopita, Tanzania ndio imeongoza kwa mwaka huu wa ripoti ilipotoka na sio mwaka ule wa utafiti.
Tujifunze kutofautisha Tafiti na Ripoti.
Wanabodi,
Naendelea kusisitiza kwenye mazuri, tupongeze, kwenye mabaya tukosoe,kwenye maovu tulaani, kwenye mapungufu tushauri na kutoa mapendekezo.
Leo nilikuwa napitia ripoti ya Benki ya Dunia(WB) kuhusu hatua ambazo zimechukuliwa na nchi mbalimbali kupunguza umasikini uliotopea, I was surprised kukuta Tanzania ndio nchi ya kwanza inayoongoza duniani kwa kupiga hatua kubwa zaidi kuondoa umasikini uliotopea, hivyo japo data ni miaka iliyopita, lakini ripoti ni mwaka huu!, hapa tunajadili ripoti ya 2019 na sio data ni za lini, hivyo Rais Magufuli na serikali yake ya Awamu ya Tano, wanastahili pongezi za dhati kwa kufanya maajabu makubwa kabisa katika vita dhidi ya umasikini uliotopea kwa kupiga hatua kubwa zaidi kupunguza idadi ya familia zilizokuwa zinaishi chini ya kipato cha dola moja kwa siku.
Hata Hivyo, Ripoti ambayo ni ya mwaka huu 2019 imeonyesha data za Tanzania kuongoza kwa kupungunguza umasikini uliotopea, zilikusanywa katika kipindi cha miaka 10 tangu 2000 hadi 2011 ila haikusema in details, Tanzania imefanya nini katika kupunguza umasikini huo, naomba tuisome ripoti hii kwa kanuni ya "the end justify the means, kwasababu kwa sasa Tanzania ni Tanzania ya Magufuli, na Tanzania ndio inayoongoza kwa kupunguza umasikini, regardless ni kipindi cha nani umasikini huo ulipungua, as long as ripoti ndio imetoka sasa na Tanzania tunaongoza, then ni haki na halali kabisa pongezi hizi ziende kwa Magufuli na awamu yake ya tano, ila pia kwa vile najua kuna kazi nzuri inayofanywa na TASAF, kwenye ule mpango wa kunusuru kaya masikini, huku MKURABITA, ukirasimisha rasilimali na biashara za wanyonge, na hatua nyingine mbalimbali zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano katika kupunguza umasikini na kuinua kipato.
Wajameni, taarifa hii ni kwa mujibu wa datas za kuaminini za WB, maana humu jf kumezuka mtindo wa kubeza tuu kila kizuri kinachofanywa na awamu hii. Kwa vile mimi sio mchumi, hata ule ukuaji wa uchumi wa taifa wa zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ulikuwa unanitatiza kwa sababu nikiangalia hali halisi huku mitaani mambo yanakuwa ni magumu sana, na kujiuliza huo ukuaji wa uchumi wa zaidi asilimia 7% unamfaidia nani, ni mpaka mchumi wetu Number 1 aliponifafanulia ndipo nikaelewa.
Hivyo hata bandiko hili, kama familia yako sii miongoni mwa kaya zinazoishi kwa kipato cha chini ya dola 1 kwa siku, unaweza usielewe kuwa Rais Magufuli na awamu yake ya tano, wanafanya mambo makubwa mazuri ya kuleta maendeleo kwa taifa letu.
Hongera rana rais Magufuli na kikosi kazi chako cha awamu ya 5, inawezekana kabisa sisi Watanzania, tusione, lakini kama World Bank wameona, dunia imeona, wasioona sasa wataonyeshwa.
Na kwa vile mwaka ujao ni mwaka wa uchaguzi mkuu, kuna wanasiasa ambao watapanda jukwaani na kujinadi kuwamkituchagua tutafanya hiki na hiki na hiki, lakini kuna wengine, watapanda jukwaani sio tuu kusema, bali kuonyesha walichofanya, hivyo naomba kuwaandaa watu kisaikolojia, usije kufika muda huo, watu ambao hawana chochote cha kuonyesha kuwa wamefanya, watakatakiwa kupanda kilingeni na watu wenye good track records za waliyoyafanya, kisha wasio na kitu wakaamua kuweka tena mpira kwapani, nashauri tuu, lets save time, money and resources, kama Watanzania tunachotaka ni maendeleo, na maendeleo hayo yanapatikana, yanaonekanika, then kwa nini tusiwaache tuu tuendelee tuu bila kufanya ....
naomba nisimalizie watu wasije kuniparura bure humu.
Maendeleo haya mazuri ya vita dhidi ya umasikini pia yamezungumzwa kwenye ripoti hii ya UNDP
Dodoma. Poverty in Tanzania has decreased from 64 per cent in 2015 to 47.4 per cent in 2017, according to the 2017 Tanzania Human Development (THDR). The government in collaboration with the Economic and Social Research Foundation and UNDP yesterday unveiled the HDR in a ceremony officiated by...
www.jamiiforums.com
Nawatakia maandalizi mema ya kuingia 2020!.
Paskali
Pascal Mayalla Walioko mitaani na wananchi ndo wanajua wenyewe kama umasikini ume wapungukia au umezidi.
Graduates ndio wanajua kama kazi zipo bwerere unachagua.
Na walioko kazini wanajua kama mshahara unakidhi mahitaji.
Na hata Wakuu wa nchi wanajua pia kuwa mazingira waloweka biashara zinakua na kodi itaongezeka . Naamini wanajua ukweli
Mfano mimi nilikua na biashara turnover yangu kabla ya 2015 ilikua 3.5 bilion kwa mwaka
Si haba tulikua tunaenda vizuri sasa 2019 biashara imeshuka by 50% na sababu kubwa ni kufa kwa secta binafsi za ujenzi , real estate na uwekezaji ambazo ndio source ya biashara yetu.
Sasa imebidi kuweka masharti kwa wafanya kazi tuwapunguze au wakubali kubaki ila mishahara tunapunguza kwa 50% tukitegemea mambo yatabadilika baada ya Awamu ya Tano.
Tatizo la awamu hii sio ukosefu wa haki democrasiana utawala bora tu lakini hata sera za uchumi ni mbovu na zitaleta matatizo in future.
Hivo utamu wa chakula aujuaye ni mpishi
Rais Magufuli anapopewaga Salaam za pongezi kwa Uhuru na Jamhuri, huwa anapongezewa nini?. Kwani Uhuru kaleta yeye?. Hapa hatuzungumzii data collected lini, inazungumziwa ni ripoti ya mwaka huu.
Pongezi ni kwa Magufuli na awamu yake.
P
Wanabodi,
Naendelea kusisitiza kwenye mazuri, tupongeze, kwenye mabaya tukosoe,kwenye maovu tulaani, kwenye mapungufu tushauri na kutoa mapendekezo.
Leo nilikuwa napitia ripoti ya Benki ya Dunia(WB) kuhusu hatua ambazo zimechukuliwa na nchi mbalimbali kupunguza umasikini uliotopea, I was surprised kukuta Tanzania ndio nchi ya kwanza inayoongoza duniani kwa kupiga hatua kubwa zaidi kuondoa umasikini uliotopea, hivyo japo data ni miaka iliyopita, lakini ripoti ni mwaka huu!, hapa tunajadili ripoti ya 2019 na sio data ni za lini, hivyo Rais Magufuli na serikali yake ya Awamu ya Tano, wanastahili pongezi za dhati kwa kufanya maajabu makubwa kabisa katika vita dhidi ya umasikini uliotopea kwa kupiga hatua kubwa zaidi kupunguza idadi ya familia zilizokuwa zinaishi chini ya kipato cha dola moja kwa siku.
Hata Hivyo, Ripoti ambayo ni ya mwaka huu 2019 imeonyesha data za Tanzania kuongoza kwa kupungunguza umasikini uliotopea, zilikusanywa katika kipindi cha miaka 10 tangu 2000 hadi 2011 ila haikusema in details, Tanzania imefanya nini katika kupunguza umasikini huo, naomba tuisome ripoti hii kwa kanuni ya "the end justify the means, kwasababu kwa sasa Tanzania ni Tanzania ya Magufuli, na Tanzania ndio inayoongoza kwa kupunguza umasikini, regardless ni kipindi cha nani umasikini huo ulipungua, as long as ripoti ndio imetoka sasa na Tanzania tunaongoza, then ni haki na halali kabisa pongezi hizi ziende kwa Magufuli na awamu yake ya tano, ila pia kwa vile najua kuna kazi nzuri inayofanywa na TASAF, kwenye ule mpango wa kunusuru kaya masikini, huku MKURABITA, ukirasimisha rasilimali na biashara za wanyonge, na hatua nyingine mbalimbali zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano katika kupunguza umasikini na kuinua kipato.
Wajameni, taarifa hii ni kwa mujibu wa datas za kuaminini za WB, maana humu jf kumezuka mtindo wa kubeza tuu kila kizuri kinachofanywa na awamu hii. Kwa vile mimi sio mchumi, hata ule ukuaji wa uchumi wa taifa wa zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ulikuwa unanitatiza kwa sababu nikiangalia hali halisi huku mitaani mambo yanakuwa ni magumu sana, na kujiuliza huo ukuaji wa uchumi wa zaidi asilimia 7% unamfaidia nani, ni mpaka mchumi wetu Number 1 aliponifafanulia ndipo nikaelewa.
Hivyo hata bandiko hili, kama familia yako sii miongoni mwa kaya zinazoishi kwa kipato cha chini ya dola 1 kwa siku, unaweza usielewe kuwa Rais Magufuli na awamu yake ya tano, wanafanya mambo makubwa mazuri ya kuleta maendeleo kwa taifa letu.
Hongera rana rais Magufuli na kikosi kazi chako cha awamu ya 5, inawezekana kabisa sisi Watanzania, tusione, lakini kama World Bank wameona, dunia imeona, wasioona sasa wataonyeshwa.
Na kwa vile mwaka ujao ni mwaka wa uchaguzi mkuu, kuna wanasiasa ambao watapanda jukwaani na kujinadi kuwamkituchagua tutafanya hiki na hiki na hiki, lakini kuna wengine, watapanda jukwaani sio tuu kusema, bali kuonyesha walichofanya, hivyo naomba kuwaandaa watu kisaikolojia, usije kufika muda huo, watu ambao hawana chochote cha kuonyesha kuwa wamefanya, watakatakiwa kupanda kilingeni na watu wenye good track records za waliyoyafanya, kisha wasio na kitu wakaamua kuweka tena mpira kwapani, nashauri tuu, lets save time, money and resources, kama Watanzania tunachotaka ni maendeleo, na maendeleo hayo yanapatikana, yanaonekanika, then kwa nini tusiwaache tuu tuendelee tuu bila kufanya ....
naomba nisimalizie watu wasije kuniparura bure humu.
Maendeleo haya mazuri ya vita dhidi ya umasikini pia yamezungumzwa kwenye ripoti hii ya UNDP
Dodoma. Poverty in Tanzania has decreased from 64 per cent in 2015 to 47.4 per cent in 2017, according to the 2017 Tanzania Human Development (THDR). The government in collaboration with the Economic and Social Research Foundation and UNDP yesterday unveiled the HDR in a ceremony officiated by...
www.jamiiforums.com
Nawatakia maandalizi mema ya kuingia 2020!.
Paskali
Watanzania tujifunze kusoma ni ripoti ya lini!. Ripoti hii ni Ripoti ya mwaka 2019 regardless data zilikuwa collected lini, validity ya ripoti yoyote ni the date of publication of the report na sio dates of data collection, hivyo as of now, Tanzania ndio inaongoza kwa kupunguza umasikini uliotopea kwa mwaka huu 2019!.
P
Validity ya ripoti ni date of publication na sio data zilikuwa collected lini??!!...kweli???!...unachoweza kuipongeza serikali (kama kweli kipo cha kupongeza) ni kwa kuwezesha ripoti kutolewa. Lakini hata hivyo sio wao walioitoa, kwahiyo kwa kifupi hapo hakuna cha kupongeza.
Kiukweli kunahitajika elimu kwa Watanzania kusoma ripoti. Mwaka 2000-2011 was the data collection period, unaweza kukuta kwa data hizo, kwa mwaka huo, wala Tanzania haikuongoza. Date of publication ndio hii ya Dec, 2019. Hii maana yake Tanzania ndio inayoongoza sasa kwa ripoti ya mwaka huu.
Mimi nina watoto 10!. Tukifanya research ya members wa jf wenye watoto wengi kwa mwaka huu wa 2019, naweza kuongoza. Ikichapishwa Ripoti ya "Wana JF Wenye Watoto Wengi 2019", jina langu likaongoza. Ukiangalia niliwapa lini, huwezi kuja na hoja kuwa tangu 2015 tayari nilikuwa na watoto 10, hivyo hiyo rekodi ni 2015!. Ripoti ikitoka mwaka huu, mimi nikaongoza kuwa na watoto wengi, haijalishi walizaliwa lini, bingwa wenu nitakuwa ni mimi, unless aje mwenye watoto 11!.
Sasa katika ripoti ya mwaka huu ya WB kuhusu kiwango cha kupungua umasikini duniani, Tanzania ndio tumeongoza sio kwa nchi za East Africa, Sio kwa nchi za Bara la Africa, bali tumeongoza kwa dunia nzima!. Haijalisi data zilikuwa collected lini, bali ripoti ndio imechapishwa sasa na ni ripoti ya mwaka huu!.
P
Ingawa mfano wako hauendani lakini tuchukue tu huo huo. Hao watoto ni wako na ni kweli utashinda lakini ukweli ni kwamba tokea wamezaliwa wewe ndo baba yao, yaani wewe ndo uliwazaa. Tofauti na hiyo ripoti ni kwamba data zilikusanywa kipindi cha mtu mwingine na zimetolewa kipindi kingine. Mfano wangekusanya data kipindi kile ukakutwa na watoto kumi halafu pengine ukafariki watoto hao wakaishi na mjomba. Je, wakitoa hiyo takwimu watasema mjomba ana watoto kumi au watasema wewe mwaka fulani ulikuwa na watoto kumi??!
Rais Magufuli anapopewaga Salaam za pongezi kwa Uhuru na Jamhuri, huwa anapongezewa nini?. Kwani Uhuru kaleta yeye?. Hapa hatuzungumzii data collected lini, inazungumziwa ni ripoti ya mwaka huu.
Pongezi ni kwa Magufuli na awamu yake.
P
Naunga mkono hoja, tunaipongeza serikali ya awamu ya tano iliyo chini ya Rais Magufuli kwa kupunguza umaskini ktk kipindi cha kuanzia mwaka 2000 hadi 2011.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.