Pongezi za pekee kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Abubakar Kunenge

Pongezi za pekee kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Abubakar Kunenge

Masokotz

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
3,713
Reaction score
6,121
Kwanza nianze kwa kusema kwamba mimi ni mdau mkubwa sana wa maendeleo ya jiji la Dar na binafsi ninatamni sana Dar es Salaam liwe jiji la kisasa kabisa.

Leo naandika waraka huu kumpa pongezi zangu za dhati kabisa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Ndugu Kunenge kwa namna ulivohakikisha kwamba hauwabugudhi Watanzania walipokuwa wanampokea Jemadari Lissu. Sitaki kufikiri kwamba MSIBA wa MZEE MKAPA umechangia hili hapana,Nataka kuamni kabisa kwamba wewe unazo hekima na busara za kiutawala na kwamba yaliyotokea jana ni udhihirisho wa kuzaliwa kwa Dar es Salaam Mpya.

Nakukaribisha sana Kigamboni uje kusimamia Miradi maana huyu Boss wako wa Zamani huku sis hatumtaki tunataka wewe uje maana wewe sasa ndo mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.Ile kasi mnayoonesha ya kukamilisha hiki kipande cha Barabara hapa Mnadani ni nzuri sana,Wahimize wakandarasi wafanye kazi usiku na mchana ila uje utuzindulie hii rounda about hapa ambayo Boss wako wa zamani alishindwa kuitengeneza kwa miaka mitano.

Vile vile uje huku Kigamboni uangalie namna ya kufanya kwenye hii barabara ya Kutoka Tungi-Mnadani kupitia Kisota mpaka Mjimwema ambayo naona inawekewa lami lakini wakandarasi wanafanya kazi kivivu sana Ili uwachangamshe wafanye kazi kwa bidii.

Hapa kwenye Bonde la maji wote walipojenga na ambapo hapapitiki wakati wa mvua naamini kabisa unaweza kupafanyia jambo ili pawe bora zaidi.

Vile nikukumbueshe tu kwamba Lile eneo la Manispaa liliko karibu na barabara njia ya kwenda ofisi ya mkuu wa wilya na mkurugenzi litolewe kwa wananchi kwa mkataba wajenge Majengo ya Biashara kwa mkataba na Manispaa ili Wana Kigamboni tuwe na Shopping centere ya Kisasa Pale.Kama Pesa Ipo Mnaweza kujenga Stand Kubwa ya Kisasa Kabisa Pale pamoja na Masoko na Ofisi space.ili kusogeza huduma huku kati.Cha muhimu ni kuhakikisha kwamba kunakuwa na huduma za muhimu kama umeme maji na internet yenye kasi.Mkifanya hivyo Na hakika Geza Ulole itakuwa Centre ya Kigamboni

Pia Hili Daraja la Kwenda Mbutu naona Kazi inaenda vizuri ila spidi ya Kazi ni ndogo sana,Wekeni Mipango ya Kuiwekea hii barabara ya Dege Mbutu Lami kabisa ili sisi wana kigambini tuendelee kufurahia maendeleo.Huku Kimbiji nako Msitusahau bwana,hata sisi ni watanzania Pia

Kwa kuwa ulikuwa katibu tawala najua mengi tayari ulikuwa unayafahamu ili nitaurahi sana ukija Kigamboni kutusalimia wanakigamboni maana hapa ndipo JIJI jipya la Dar-Satelite city litakapojengwa na Tunataka wewe uje uongozi njia.

Hongera sana Kunenge kwa kuonesha hekima ya kiuongozi.

Kizito S.

Kimbiji-Kigamboni
 
Mimi kipekee kwa kweli ningependa nimshukuru kwa hii hali ya hewa ya dar es salaam tangu aingie ni kaubarid flan kakibabe kwa sasa nadhani yule mtangulizi wake alikua anakula hela ya baridi wata tunaangamia na joto ya hajali kabisa nawasilisha
 
Mimi kipekee kwa kweli ningependa nimshukuru kwa hii hali ya hewa ya dar es salaam tangu aingie ni kaubarid flan kakibabe kwa sasa nadhani yule mtangulizi wake alikua anakula hela ya baridi wata tunaangamia na joto ya hajali kabisa nawasilisha
Yani jiji lemetulia,wakazi wa jiji wametulia,Polisi hawachukui rushwa hovyo hovyo,Mambo sasa hatoi mikwara ya ajabu ajabu.Yaani hata unajisikia RAHA kuwa mkazi wa Dar es Salaam
 
😂😂 yaan nyie majamaa mkiweza kutenganisha dini na ujinga mtaish kwa amani sana hapa kwenya duniya
Ila Mkuu Dini na Imani,na Imani ni maisha.Abubakar Kunenge ni mcha Mungu hilo halina Mjadala.sio swala la waislamu kuchanganya dini na sijui nini.Ni swala la ukweli jinsi ulivo.
 
Msimtafutie mwenzenu kufukuzwa kazi. Pongezi nyingine zinamchulia mtu. Kuweni wakubwa (kiakili) jamani.
Mkuu,Hawawezi kumtoa kama anafanya kazi nzuri,Huyu jamaa ni Kiongozi mwenye utulivu wa kiakili na kihisia sio kama Mtangulizi wake
 
Mkuu,Hawawezi kumtoa kama anafanya kazi nzuri,Huyu jamaa ni Kiongozi mwenye utulivu wa kiakili na kihisia sio kama Mtangulizi wake
Dahhh, mpeni muda wakuu[emoji3]. ni mapema sana kuanza kumsifia maana with time binadamu anabadilika
 
Yaani naimagine kipindi hiki cha msiba sijui kungekuwa na video ngapi huyo YouTube na instagram zikimwonyesha Makonda akiwa busy na kuandaa,yaani....
 
Unapongeza kwa CDM kuzuiliwa kwenye msiba wa Mkapa?......! Acha mambo kama haya wewe. Lakini baadaye ohh daraja la Mbutu spidi ndogo.

Sasa unampongezea nini Kunenge? Watz bwana.
 
Unapongeza kwa CDM kuzuiliwa kwenye msiba wa Mkapa?......! Acha mambo kama haya wewe. Lakini baadaye ohh daraja la Mbutu spidi ndogo...Sasa unampongezea nini Kunenge? Watz bwana.
Nani kawazuia Bana?Hilo la msiba lilikuwa swala logistic tu wala msilete porojo.Hayo niliyoeleza ni maeneo anatakiwa afanyie kazi kama hupendi potezea.Halafu acha kuingiza Utanzania wangu kwenye Upuuzi wako
 
Yaani mkoa wa baridiiiii umetulia na umekuwa wak starabu sana yaani mpaka SIro anaongelea fujo Masasi sio Dar.Duuu maisha yanaenda kasi sana aisee sio mchezo.Big up mkuu wa mkoa mpya nimekukubali .Makonda akirudi kuwa mkuu wa mkoa aende zake Dodoma
 
Back
Top Bottom