Poor Ali Kiba, kama hujui kiingereza ni vema kuongea lugha yako tu

Nimetoka kusikiliza, Yesu na Maria uwiiii anaongelea nini huyu mwanaume? Kwa kweli ndio msanii anayejiita mkubwa anasema hayo?

Hata kwa kiswahili bado angeshangaza tu.

Hajui ndio wakati wa kujiuza hapo, mtu atake kujua zaidi na kazi kumjia. Nani kweli atataka kusogea nae... duh!!!!
 
Ni kama alikuwa anatengeneza sentensi ya kiswahili kichwani halafu anatafsiri kwa sauti kwa kiingereza.
Hayo yalinikuta enzi hizo za morning talk shuleni. Miaka hiyo nilionekana nakijua kweli.
 
..haha!!kweli Hii Lugha Ililetwa na meli,there is no way mtu unaweza ukaongea Ivo,hata basics Hana
 
Acha ujinga, chakwako kikojee? Alichoongea hicho kinatosha ilimradi kimeeleweka ndio la msingi,usitake watu waongee kama waingereza, hata mzungu aliejifunza kiswahili usitegemee ataongea kama mswahili mwenye lugha yake, ata chapia and that's normal.
 
Kaongea lugha mbaya ipi ambayo haijaeleweka?Mbona kaongea simple English na well understood.
Katika hadhira ile angeongea Kiswahili unahisi nani angemsikia?
Think harder
 
Acha ujinga, chakwako kikojee? Alichoongea hicho kinatosha ilimradi kimeeleweka ndio la msingi,usitake watu waongee kama waingereza, hata mzungu aliejifunza kiswahili usitegemee ataongea kama mswahili mwenye lugha yake, ata chapia and that's normal.
kuchapia kawaida sana, tatizo la kiba MAJIVUNO anajiona king afu kujieleza hajui sio kwa kiswahili wala kingereza ndipo hapo tunaposhangaa king of F.ckngEverything
anashindwaje lugha[emoji780][emoji780][emoji780]
 
Hivi tatizo ni hao wanaokosea kuongea kiingereza hadi tunaona aibu au tatizo ni sie tunaoona aibu? Maana mbona wazungu wakiongea kiswahili na wanakosea sana tu lakini mbona hatuoni aibu kwa kukosea kwao?

Tatizo ni mitazamo yetu tu katika hiyo lugha na si kingine,maana tatizo hili lipo kwenye kiingereza tu na si lugha zengine.
 
Seriously the guy has really tried. Am sure if we put you on a clear spotlight it might be challenging for you to put up a technical dialogue in this colonial language.

Yes, he should have spoken in swahili, a language he does command but we must also ask few questions to ascertain that line of thought.

1. Who were the audience?
2. What was the interview language?
3. Were there interpreters available to make swahili palatable to the audience?

Tusihukumu bila kujitafakari katika hili
 
Kiingereza janga la taifa. Hata Magufuli ana Ph.D lakini Kiingereza cha manati.
 
Jamani amejitahidi ingawa "you know" nyingi.kujiamini kumeongezeka interview zake za zamani na hii ya sasa ame imrove kiasi fulani.ipo siku ataweza tu. Msimvunje moyo
 
Lkn yeye kibakuli si wa kitambo kny fani mpk akashirikishwa na rkelly (mnavyosema) inakuaje kalugha haka ka malkia kamtoe jasho jamani kuna mkono wa mtu si bure [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Harmonize alisemwa humu kwa kuongea kiswahili USA.

huyu akasema naongea lugha ya malkia.

au alizimiwa kiingereza na Sallam?
 
Harmonize alisemwa humu kwa kuongea kiswahili USA.

huyu akasema naongea lugha ya malkia.

au alizimiwa kiingereza na Sallam?
Ndiyo maana mie nasema tatizo lipo kwa wanaokosoa wenzao ila hawajajijua.
 
Kukosea ni kaz rahisi sna lkn kuwa sehem fulan ni kaz kubwa zaid I have learn we have alot to learn
 
Kama English ngumu mi natoa offer ya kufundisha kijerumani bure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…