Poor customer services, nini chanzo?

rpg

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2007
Posts
3,620
Reaction score
1,478
Kama mtanzania, kama binadamu, ni lazima nihitaji huduma mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Ili kuyapata haya lazima nizifuate mahala huduma hizi zilipo iwe ofisi za serikali na zisizo za serikali, ofisi za huduma, mahotelini, mahospitalini, bank, nk. Katika watoa huduma kumi wa kitanzania, zaidi ya 75% hutarithika jinsi ambavyo wana toa huduma kwako kama mteja. Wengine huongea kama umewalazimisha vile, wengine huwa wako busy na mambo mengine wakati ukiwaeleza shida zako, wengine lugha za ukali, nk. Mbaya zaidi utekelezaji wa kile unachokihitaji hata kama unakilipia huwa ni wa kusukuma sana na pengine usifanyike kabisa. Waweza ambiwa uje baada ya siku kadhaa, lakini ukirudi hakuna kilichofanyika. Mbaya zaidi mzaha huu unafanyiwa bila kujali umetoka mamia ya kilometer kwa ajili ya jambo hilo.

Nini chanzo? Mishahara mdogo? Uvivu? Ubabe na dharau?

Je hali hii inaathiri vipi uchumi wetu?

Watanzania tubadilike! It begins with me!
 
Chanzo ni uvivu, ubabe na dharau.......
 
KUGEGEDWA NA WAKUBWA

we customer service personel atapata wapi
jeuri, dharau, kiburi mbele ya mteja?

si anajua hata ukienda kwa bosi hafanywi chochote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…