Ianzishwe hii sheria ya mtu kuto-quote uzi mrefu. Sio wote wanatumia computer kuingia humu, wale wanaotumia simu wanapata shida sana.
Hii sheria ianzishwe ikiwezekana hata ban ya siku tatu ihusike.
Ku-quote uzi mzima ni kigezo kimojawapo cha uzi huo kutumika kama ushahidi pindi pale utakapouedit baada ya kujichanganya mwenyewe au pengine kudanganya.
Naunga mkono hilo, nadhani mods ni wataalamu wa haya mambo, hivyo kama wanaweza kumodify namna ya ku quote itapendeza. Ku quote kuna maana kubwa lakini mtu mwingine ana quote mwishoni hana hata ujumbe mrefu.. Mfano mtu ame quote chini anaishi neno "kweli kabisa". Km kutakuwa na maboresho ya ku quote mods itasaidia.