Posta ni salama kutuma na kupokea mizigo kutoka nje ya nchi?

Posta ya Tz ni taasisi fulani hivi ya kijima, genge la vibaka na upuuzi mwingine mwingi.
Kimsingi taasisi, mashirika ya umma, wizara na idara zake kila kitu kinaendeshwa kijima. Bado wapo miaka ya 1970 na mbaya zaidi wana urasimu wa hali ya juu. Kuibadilisha Tanzania inahitaji operation kali sana. Watu hawajali na wanaenda kazini ili kuhesabiwa tu na siyo kufanya kazi.
 
Shirika limejaa wajanja wajanja wapigaji na hakuna hatua zinachukuliwa. Shida ya kuajiri kwa kujuana. Unakuta wafanyakazi wana undugu na mabosi wakubwa.

Huu uhuni huwezi upata kamwe huko DHL.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu acha kufananisha DHL na ushuzi wa mbuzi tafadhali

Sent using Unataka kujua ili iweje
 
GreatMkubwa,
System ya posta haifanyi Kazi yake ipasavyo tangu mwezi December so jaribu kwenda kuulizia posta husika maana kuna mdau aliwaibukia huko wakamwambia kwamba mzigo wanao shida haujaingizwa kwenye system yao
 
Wakurugenzi wote wa mashirika ya umma wamepewa vyeo kama fadhila tu aidha za ukada au walisaidia kwenye kampeni.

Au Kuwasaidia Watoto Wao Wasikae Jobless.

Ni Vieneo Vya Kisiasa Na Sehemu Zao Za Kula.

Hivyo Vihuduma Uchwara Wanavyotoa Ni Basi Tu Kuonesha Na Wao Wapo.
 
Kweli, nikiingia kule kwa Posta Tz naambiwa haupo kwny system[emoji26] inaboa sana, niliwaagizia watoto zawadi matata sana na nikawaahidi by Christmass watakuwa nazo saaasaaaa nimejieleza mpaka bas. Wanataka zawadi zao, inaboa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijawahi kupata tatizo kwa kutumia posta... Wana fanya vizuri kwa kweli.... Nimeagiza mingi sana na mingine ipo njiani, kuna mapungufu kidogo lakini sio tatizo kubwa sana
 
Mbaya zaidi hii kitu niliagiza kama zawadi ya Sikukuu kwa watoto...
niliwaagizia watoto zawadi matata sana na wakaziona picha na nikawaahidi by Christmass watakuwa nazo saaasaaaa nimejieleza mpaka bas. Wanataka zawadi zao, inaboa sana.
Dingi nimekuwa tapeli mbele ya watoto wangu[emoji25][emoji29][emoji29] GreatMkubwa,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu una bahati sana.... Mimi nilituma simu... Parcel ikafunguliwa simu ikaibiwa parcel ikafungwa tena.. Nawasiliana na posta Cape Town parcel imerudishwa lakini haina kitu ndani... Nikapewa documents nijaze kwa ajili ya investigation.... Mpaka leo mwaka wa Tano huu....
 
GreatMkubwa,

nilisha tandikwa hapo mzigo ulikaa miezi miwili na kuja kusainishwa na kulipa napewa mzigo umefunguliwa nilisikitika mno.posta lina wazee wengi alafu kazi wanavo chukulia kama hakuna biashara


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kama ni password vipi ibandikwe juu ya mzigo.Nijuavyo tracking no hutolewa kwaajili ya kukujulisha mzigo ulipofikia.Anyway kila la kher

Sent using Jamii Forums mobile app
Bro msaada wa kupeana mpaka Tracking number haupo... kuandikwa juu haimaanishi ndio nikupe namba.
Kuchukua mzigo unahtaji Tracking namba na ID yako.
Kwanza we nikupe hyo namba we nani??? Meneja wa Posta????

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna haja ya serikali kufumua uongozi wote na mfumo wote pale posta mana sio kwa ujinga huu...mzigo unaweza kuwasili hata wk lakini haufanyiwi process za kutoka ukienda kuulizia utaambiwa ndio umeingia leo,hapo ndio utafanyiwa mchakato na kupigwa tena kalenda ya kwenda kuchukua.

Toka tar 26.01 nimeambiwa niende tar 10 kuchukua hivi kweli? Tutafika kweli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa jamaa wa posta ni wezi sana. Mwezi uliopita nilipokea vimzigo v2 kiearphone na card reader. Upumbavu unaanzia wapi?
wananitumia meseji ndugu mteja fika ofisi ya posta dirisha namba c pia kumbuka kuja na 18800. Nikajiuliza kama vimzigo hivi havifiki hata kilo1 nalipishwa hivyo inakuwaje nikiagiza mikubwa kidogo?
 
18800 tsh au no ya mzigo?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…