Povu la mwanasiasa wa Kenya Miguna Miguna dhidi ya rais wa kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta

Povu la mwanasiasa wa Kenya Miguna Miguna dhidi ya rais wa kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta

smarte_r

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2013
Posts
4,564
Reaction score
12,014
Nitajitahidi kutafsiri kwa kiswahili ili iwe msaada kwa ndugu zangu watanzania ambao lugha ya kingereza sio rafiki kwao.

Miguna anasema,
Jomo Kenyatta (johnston kamau ngengi) alikuwa ni mtu mbaya kimuonekano ambaye jina na sura yake vinatakiwa kuondolewa kwenye masanamu, viwanja vya ndege, barabara, majengo na fedha ya kenya kwa kutumia sulphuric acid.

Anasema hakuwa tu mbaya kimaumbile bali hata kimaadili ambapo aliuwa watu wakubwa wa kenya wa enzi hizo waliokuwa na maono mazuri kwa taifa hilo.lakini pia aliipora kenya kwa kutumia mabavu.

Anasema jomo kenyatta alirejea kenya akitokea ulaya alikokuwa anafanya kazi za bustani kwa miaka 15 nchini scotland.

Anasema alipopata tu nafasi ya kuwa waziri mkuu wa kenya mwaka 1963,hakuwa akimiliki gari, nyumba wala ardhi. lakini miaka 15 baadaye baada ya kuwa waziri mkuu, alipora ardhi yenye ukubwa sawa na eneo lote la pwani ya kenya. uporaji ulimfanya kuwa mtu mwenye utajiri mkubwa africa.

Anasema laiti kama jomo kenyatta asingewauwa watu wenye maono makubwa wa nyakati hizo kama pio pinto gama, argwings kodhek, thomas Joseph mboya na JM kariuki, taifa la kenya lingekuwa katika nafasi kubwa ya kuwa taifa la kwanza kimaendeleo toka africa ktk karne ya 20.

Anasema Jomo Kenyatta alianzisha mauaji, ukabila na uporaji katika siasa za kenya.

Anahitimisha kwa kuweka hashtag

# DespotsMustFall akiwa na maana viongozi wanaotawala kimabavu lazima wadondoke.

IMG_20190602_123918.jpeg
IMG_20190602_123932.jpeg
FB_IMG_1559468341221.jpeg
 
Hivi Kenya kaika zile harakati za kuikomboa Afrika ilishiriki vipi.... ilitumia rasilimali yoyote kuhakikisha nchi nyingine zinakuwa huru......? au hawa jamaa wana asili ya ubinafsi kujiangalia wao wenyewe tuu ( MR.MYSELF) , wamelea viongozi gani katika Afrika hii kama ilivyokuwa Nyerere kuwalea na kuwafunza akina mandela, masire, Mugabe, Nk?

Ukipita mitaa mbali mbali Tanzania, mahospitali, mashule na huduma muhimu za kijamii zimepewa majina ya wapigania uhuru wa afrika ambao kwa nyia moja ama nyingine walipita mikononi mwa Nyerere hivi Kenya wana kitu cha namna hiyo ama wameita mitaa kulingana na vitu wanavyopenda kutumia kama KARIOBANGI, MIRAA nk?
 
Sasa Tz ina husu namna gani na mambo yenyu ya ukabila ya Kenya?
 
hakuna sehemu alipoitaja tanzania. acha kukurupuka ndg.
Hujaona hapo kuhusu kujuakizungu? And let me for the fact tell you we can speak it more than you can. Take a chill pill
 
Hujaona hapo kuhusu kujuakizungu? And let me for the fact tell you we can speak it more than you can. Take a chill pill
kuna baya lipi katika kutokujua kingereza?.
au nimefanya kosa kuitafasiri?.

kwani uongo?, ni kweli watanzania tunasumbuliwa sana na kingereza. mimi ni moja ya watz nisiyemudu kingereza na wala sijisikii vibaya. hata rais wetu magufuli ni mmoja wao pia.
 
kuna baya lipi katika kutokujua kingereza?.
au nimefanya kosa kuitafasiri?.

kwani uongo?, ni kweli watanzania tunasumbuliwa sana na kingereza. mimi ni moja ya watz nisiyemudu kingereza na wala sijisikii vibaya. hata rais wetu magufuli ni mmoja wao pia.
Sasa nani ana makosa wewe ulie taja Tz isipo husika au mimi. Uyo Miguna ana tuhusu namna gani?
 
Sasa nani ana makosa wewe ulie taja Tz isipo husika au mimi. Uyo Miguna ana tuhusu namna gani?
kwani kuna kosa gani kuleta mada inayohusu kenya kwenye jukwaa la kenya?.

au hujui kuwa hii mada ipo kenyaforum?. ulitaka niipeleke jukwaa la MMU?.
 
Back
Top Bottom