Power Mabula: Mtu aliyetikisa enzi zake!

Huyu jamaa nimemkumbuka alikuwa ana nguvu za kimiujiza. Yeye mwenyewe aliwahi kufanya mkutano wa injili, mji mdogo wa Sirari Tarime mnamo 2003, kwa wiki 1 hivi. Alitusimulia alikuwa na irizi kibao na kila irizi ina kazi yake. Yale mambo alikuwa anafanya yote yalikuwa changa la macho. Aliamua kuokoka na sasa hivi anahubiri na kuponya watu.
 

The guy is alive yet; kwa sasa ana-hubiri INJILI na wakati mwingine uwa anatangaza vipindi fulanifulani KISS FM Mwanza.

Kweli huyu jamaa alikuwa na uwezo mkubwa wa kufanya maajabu, alikuwa ana uwezo wa kubeba kwa meno mifuko mitano yenye simenti na pia kuzuia pikipiki zisiondoke kwa kutumia kope za macho. Anayetakaya kimuona wasiliana na Kiss FM Mwanza atapata habari zake
 
Duh! umenikumbusha mbali kweli enzi za shule ya msingi.
Pia kulikuwa na profesa mmoja wa kihindi anakupa ndizi waila halafu anapasua tumbo live na kutoa ndizi iliyoliwa sijui walikuwa wanatudanganyaje? mazingaombwe ya zawadi za biskuts, chupi na vitu kibao watoto mnapewa duh kazi kweli
 
Thread kama hii ni nzuri sana, unakumbuka matukio na enzi za wakati huo, namkumbuka pia Power Jabir Computer a.k.a Kababayee ulikuwa ukiambiwa atakuja shuleni chunga sana kalamu na vitabu, mtu akikuibia anaviuza japo apate shilingi 5 ya kuingilia kwenye maonesho na nyimbo zake zile ''misumri nilalielalie'' watu ''lalia''
 
Siku zoote mimi nilijua jamaa ni myth tu! Bora umeeuliza for the benefit ya wengi...


The Following User Says Thank You to Steve Dii For This Useful Post:

Asha D (Today)​
 
Hapana X-P hakua mtu wa msoma alikua msukuma, naskia alikuja kuokoka yeye na mwingine alikua anaitwa power Mwasekaga kitu kama hicho.
Hawa jamaa walitakiwa wawekwe kwenye kipindi cha Believe it or No cha AXN.
 
mimi nilimshuhudia kigoma akifanya vitu vyake mfano kunywa chupa
mbili za orange squash bila ku-dilute, gari kupita kifuani, kuvutana na watu
"walioshiba", kuzuia pikipiki isiondoke kwa kuivuta kwa meno n.k.
aidha nakumbuka kila alipokuwa anaanza tukio alikuwa anasisitiza kwamba zake
sio nguvu za giza bali ni za asili hivyo alikuwa anawasihi "watazamaji" wasimjaribu
kwani watamuua bure.

ni wakati wa kuvutana kamba alikuwa anapita miungoni mwa
waliojitokeza na kuwaondoa baadhi ya watu bila maelezo!
 
Umenikumbusha enzi za mapawa na maprofesa (wanamazingaombwe). Power Mabula was one of my favourite, kulikuwa na power mwingine anaitwa Power Ngeta, huyu akija tulikuwa tunaimba "Power! Ngeta! Super! Kibongeeee!" Sijui yuko wapi naye huyu.

Kuna dogo tulikuwa tuko naye darasani alikuwa ni fundi wa kutengeneza mihuri (inayogongwa mkononi kama unatoka nje mara moja na utarudi), basi wale maprofesa wakija dogo naye anatengeza na kutugongea mikononi watu wanaotaka kuingia bila kulipia. Baadae ukitoka unampa shilingi 5 au unamnunulia vipande vya mihogo. Tulikuwa tunainjoi sana maisha yale.
 

Ahsante kwa kunikumbusha wimbo wa Power Ngeta! Mid 80 hizo. Power Iranda,Power Mwanakulya jitu lishibalo.
 

Duh,hii sikuwahi kuisikia.
 
Bila kumsahau Profesa EYESO! (A.S.O) na mazingaombwe yake, miaka ya '80s alizungukia karibu shule zote za wakati huo
 
Power Mabula, huyu jamaa yupo hapa Mwanza anatangaza kwa radio kiss fm na Living water fm. Yaan jamaa aktangaza ana maufundi flan hv. Yale ya eeehi bado tupo hewani eeh tena kwa sana........,yani yale mambo ya long tym.
 
Kulikuwa na PAWA SAVIMBI, JAFAR VURU MROMA , MBWA MWITU (RIP).......Siku hizi huu mchezo haupo tena......kila mtu sharobaro

...we bwana umenifanya nicheke kweli peke yangu! Kila mtu Sharobaro, huh?..........teh teh teh! :biggrin1: :biggrin1:

 
mmenikumbusha power Mketa super Kibonge wa kule kwetu Mtwara.. Duh huyu jamaa alishatujaza uwanjwa wa Umoja pale karibu primaries zote za pale mtwara kipindi hicho kiingilio sumni
 
Kuna simulizi kule kwao Bariadi alikozaliwa kwamba alizaliwa shambani wakati mama yake anafanya kazi za shamba. Siku hiyo mvua kubwa sana ilinyesha na ikamnyeshea lakini hakudhurika na hiyo mvua. Mama yake alipomfikisha nyumbani babu yake alimtemea mate mdomoni na kumwambia utakuwa miamba kati ya miamba na hakuna atakayekushinda nguvu. Basi inawezekana hako kazee kalimfanyia vitu fulani hivi ndo maana akawa hivyo, si unajua tena mambo ya akina Mwanamalundi kule Usukumani!!!

Ila jamaa kweli alikuwa na nguvu za ajabu niliwahi kumshuhudia miaka ya 1980 huko Mwanza anavuta pikipiki 250 XL kwa kutumia nywele, anavunja msumari wa inchi 6 kwa mikono kama anavunja ukuni.

Lakini pia enzi hizo na ma-power uchwara walikuwapo, siku moja shuleni kwetu akaja power uchwara mmoja utafikiri ana utapiamlo eti naye akaitisha mijamaa 10 iliyoshiba akafunga kamba mikono yake na kila upande zikakaa njemba 5 kidogo zimnyofoe mikono (almanusura kifua kichanike), wanafunzi mbavu hatukuwa nazo siku hiyo.

Kwa kweli enzi hizo ilikuwa raha! Pamoja na maisha kuwa magumu (Ingawa haya ya Mkwer'e yamezidi kipimo) lakini tulikuwa tunaburudika wala huwaziii kama kuna ugumu wa maisha!!!!
 
Hapana X-P hakua mtu wa msoma alikua msukuma, naskia alikuja kuokoka yeye na mwingine alikua anaitwa power Mwasekaga kitu kama hicho.
Hawa jamaa walitakiwa wawekwe kwenye kipindi cha Believe it or No cha AXN.
Ahsante Mamushka kwa kusahihisha, mambo yenyewe ya siku nyingi tena, nshaanza na kusahau.
 






Naombeni mnikukmbushe, hivi mzee mwinamila alikua nani vilee, hilo jina nalikumbuka.
 
mmenikumbusha power Mketa super Kibonge wa kule kwetu Mtwara.. Duh huyu jamaa alishatujaza uwanjwa wa Umoja pale karibu primaries zote za pale mtwara kipindi hicho kiingilio sumni

Sumni? mh zamani sana itakua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…