Prefect wa darasa la 6B mbona hata wewe unatajwa

Prefect wa darasa la 6B mbona hata wewe unatajwa

View attachment 919957

Ni pale prefect wa shule ya Dodo alipoomba majina ya wanafunzi wote wanaoachia hewa chafu darasani. Anasema amechoshwa na tabia ya wachache wanao haribu hali ya hewa darasani.

Kuna wengi hasa wale ambao wanaomba mwalimu atoke waendelee kucheza. Wao shuleni wanakuja ku social ndiyo hao walikuwa front line kumpa prefect majina. Prefect anasema hata mwenyewe yamemshangaza ma confi waliyokuja nayo jamaa.

Huku nyuma tuna list yetu, hawa ni watu wanaokaa na prefect upande mmoja. Wanasema mbona prefect pia huwa anachafua hali ya hewa? Sasa nani atamfunga paka kengele? Hii list yetu tuipeleke wapi?
"Konki konki konki..master"
 
UZURI MAJINA YA WATAJWA SHURTI YATAJWE MBELE,WASEME NIPO MWALIMU!!


af ndo mwalimu aseme nimewasamehe,au atandandike!!

JE ATARUKA JINA ?
HATASOMA JINA LA KIRANJA?
 
Wasambaa wana msemo wao unasema "Mishi ya Mbazi izashia"....kila mtu ajitetee mwenyewe sasa!!
 
Ndiyo maana BWANA YESU alisema hivi; "itoe kwanza "boriti" iliyo kwenye jicho lako ndipo utaona vema kukitoa "kibanzi" kilicho kwenye jicho la mwenzako".

Huyu "Prefect" ni Mkristo na anajua vizuri sana hayo maandiko lakini kwa sababu ya hicho cheo alichopewa kimempumbaza macho, haoni wala hasikii.
 
Back
Top Bottom