Kuna watu wamesema vyema hapo juu, mimi ni mgeni lakini nimeguswa na tatizo la dada yetu.
Ni kweli kwamba kukosa choo (coinstipation) na tumbo kujaa gas (dyspepsia and ) ni matatizo ya kawaida kwa wajawazito.
Ni kweli pia kama walivyoeleza wengine kwamba hii kwa kiasi kikubwa husababishwa na kichocheo kiitwacho 'progesterone' ambacho huzalishwa kwa wingi mama anapokuwa mja mzito. Kazi ya kichocheo hiki ni kulifanya tumbo la uzazi (uterus) li-relax ili mimba isitoke (kinazuia uterine contractions).
Lakini zaidi ya effect yake kwenye tumbo la uzazi, pia hufanya relaxation ya misuli mingine mwilini hasa ile misuli laini (smooth muscles). Kati ya misuli inayoathiriwa na kichocheo hiki ni ile ya utumbo na ya mlango (cardiac sphincter) unaotenganisha tumbo na njia ya juu ya kupitisha chakula (oesophagus).
Kinachotokea utumbo uki-relax unasababisha kudorora kwa utembeaji wa utumbo (bowel movements) na hivyo kusababisha yale mabaki ya chakula ambayo yamegeuzwa kuwa uchafu (feaces) yachelewe kutolewa nje ya mwili. Hivyo mtu anaweza kuchelewa kupata choo na hivyo anakuwa coinstipated.
Ile sehemu ya mlango nayo (cardiac sphincter) iki-relax kutokana na effect ya progesterone, gas iliyoko tumboni hupanda juu kwenye oesophagus (anapata kama aina fulani ya gatro-eosophageal reflux) na kusababisha kiungulia (heartburn).
Matibabu
Kwa coistipation ajitahidi kuwa active kwa kufanya mazoezi kama kutembea, kuogelea nk., anywe maji mengi, atumie matunda ya kutosha kama mapapai, hata maparachichi na mboga mboga pia. Iron supplements pia zinaweza kusababisha coinstipation hivyo muone daktari wako ajue namna ya kukusaidia kama kukupa dawa ambazo zina kiasi kidogo cha iron.
Kwa heartburn na dyspepsia anaweza
1) Kufanya marekebisho kwenye mfumo wake wa maisha (life-style modification) kama
a) kula chakula kidogo kidogo mara nyingi, sio kingi kwa wakati mmoja,
b) asile chakula usiku sana, akichelewa mwisho saa 2.,
c) atumie mto wakati wa kulala ikiwezekana kitanda kinyanyuliwe kichwani kuzuia gas isipande juu.
d) Atumie chewing gums zinasaidia kupunguza acid,
e) aepuke vyakula vinavyoongeza uzalishaji wa acid kama maharage, pilipili na spicy foods nyingine.
2) kutumia dawa zinazopunguza acid au uzalishaji wake kama
a) cimetidine na ranitidine ambazo hazina matatizo pia kwenye ujauzito na hazileti coinstipation
b) Magnesium trisilicate ambayo pia ni salama kwa mama mjamzito ingawa dawa hii inaweza kusababisha coinstipation. Isitumiwe kwa zaidi ya wiki. Muone daktari bingwa wa akina mama in-case tatizo litaendelea.
Asitumie dawa iitwayo Omeprazole (ingawa hutumiwa pia kupunguza acid kwa wasio wajawazito) kwani imeonyesha kuleta madhara kwa mtoto hata kifo kwenye utafiti uliofanywa kwa wanyama.
Matatizo yakizidi muone specialist wako.