Presha ya Urusi, Bilionea Abramovich kupokea ofa tatu wiki hii za kuiuza Chelsea

Presha ya Urusi, Bilionea Abramovich kupokea ofa tatu wiki hii za kuiuza Chelsea

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
NINTCHDBPICT000714893309.jpg

Mmiliki wa Klabu ya Chelsea, Roman Abramovich
Mmiliki wa Klabu ya Chelsea, Roman Abramovich anatarajiwa kushawishiwa kukubali kuiuza klabu hiyo, ikielezwa kuna ofa tatu zitatolewa wiki hii.

Kumekuwa na presha kubwa kwa bilionea huyo kuiuza Chelsea kutokana na ukaribu wake na Rais wa Urusi, Vladimir Putin ambaye anasakamwa kwa kuamua jeshi la nchi yake kuanzisha mashambulizi dhidi ya Ukraine, hivi karibuni, jambo ambalo linasababisha iaminike kuwa anamuunga mkono Putin katika mgogoro huo.

Licha ya uongozi wa Chelsea kutosema kuwa kuna mipango ya kuuzwa kwa klabu hiyo lakini bilionea wa Marekani, Todd Boehly na Hansjorg Wyss wa Switzerland ni kati ya wanaotaka kutuma maombi wiki hii.

Abramovich,ameshatangaza kukabidhi majukumu yake ya utendaji kwa Bodi ya Udhamini ya Chelsea licha ya kuwa anaendelea kuwa mmiliki na inaelezwa kuwa ana mpango wa kuuza jumba lake la kifahari lililopo England.

Pia soma
1. Tajiri Roman Abromavich akabidhi timu ya Chelsea kwa Bodi ya Wadhamini wa club hiyo
2. Bodi ya Wadhamini Chelsea FC yasita kubeba mikoba ya bilionea Roman Abramovich

Source: The Sun
 
atuachie team yetu, aende kwa Vladimir wakaandae team ya ushindi Ukraine [emoji1255] ..
 
Putin atawaponza wengi pamoja na wananchi wa Russia kwa ujumla. Sasa hivi ndege haziruki kuingia wala kutoka Russia na hata waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw. Sergey Lavrov alishindwa kusafiri kwenda nje ya nchi kufuatia marufuku waliyo wekewa.
 
Back
Top Bottom