Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

Zamani nilikuwa nikiona mtu anaitwa Profesa au Dr najua ana akili kwelikweli wakati huo nilikuwa sijakutana na hawa kina Kabudi. Ndio maana kumbe watu wenye pesa zao hawataki watoto wao wasome vyuo vya hapa Tanzania.
 
Ni wazi sasa Tanzania munaongozwa na genge la watu wahuni wachache, tayari matabaka yanatapakaa, ni matokeo ya uongozi mbovu zaidi na watakao umia ni wananchi maskini. Kabudi anajua future yake tayari na familia yake, yaani inasikitisha sana kwa viongozi wenye roho mbaya kama hawa.
 
Rudisheni billion 60 za watu. Mafisadi wakubwa nyie
 
Kama tuna nguvu ya kusimama wenyewe sioni haja ya kupiga kelele, tuonyeshe kwa vitendo.
 
Jamaa usee umemvaa vibaya,uyu si ndio yule alienda Madagascar na kurudi na vichupa vya dawa ya korona,jamaa hamna kitu ,akizungumza unahisi ni mtu anaefata jazba akipigiwa makofi ndio husidi kupoteza muelekea.

Jamaa amevuruga sana au hawa ndio watu wanaosaboteji utawala wa Magufuli,kabudi amevuruga vibaya mno ,hafai hata dakika moja kuwepo katika wizara na uwaziri huo.
 
Kama hatuhitaji urafiki wa "Mabeberu" sasa mbona tulikuwa tunapigania Zimbabwe wafanyiwe wepesi? Au hatujui sababu za Zimbabwe kufikia huko?
 
Africa ipate viongozi wengi zaidi wenye misimamo kamamagufuli tutafika mbali
 
Kabudi is a loughing stock in this Authoritarian ccm regime.
 
Loo, mkuu 'MLA PANYA SWANGA', nimekusoma vizuri sana. Una njia yako ya kipekee ya kueleza jambo na likaeleweka.

Hiyo mistari ya mwanzo juu ya biblia, ilitaka kunitoa kwenye reli, lakini ulivyoiunganisha kwa hoja uliyonuia kuieleza kiufundi kabisa, nilisimama vyema kwenye ile reli.

Hongera kwa kipaji chako hiki.
 
Huyu kabudi na wenzie wangekuwa watu wenye chembe hata ndogo ya aibu, asingethubutu kusema haya aliyosema kwenye mkutano huo.

Ni kama vile alikuwa anawahutubia watu wasiokuwa na akili kichwani; watu wasioweza kutambua kitu chochote.

Kabudi na Magufuli wanadhani wamewashikia waTanzania akili zao. Wanachowaza wao ndicho wanachodhani waTanzania wote na jamii yote ya kimataifa ndicho wanachopaswa kufikiri.

Wanadhani wanapochomekea aliyofanya Mwalimu, watu watawapa hadhi ya uzalendo wasiyoistahili. Aliyoyafanya Mwalimu na wanayoyafanya wao ni mambo tofauti kabisa.

Hawa watu mwisho wao utakuwa wa aibu kubwa.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…