Prof Kabudi: Kati ya pesa na heshima ya nchi yetu, tutasimamia heshima. Tuko tayari kuwasikiliza na kujadiliana kwa heshima

Issue sio misaada issue ni vikwazo vingine. Bidhaa zetu tutauza wapi nk Tusije kuwa Zimbabwe
 
Hatujalazimishwa kupokea misaada! Acha kupokea msaada muone cha mtema kuni!
 
Mpuuzi tu hana maana yoyote. Misaada mnapenda sana kila Head of state akija mnaomba misaada. Hata hio aid ya EU for Covid mlificha, serikali haina uwazi kabisa.
 

Alikuwa anamjibu nani - tena kupitia local press briefing? Kuna hoja rasmi iliyofikishwa kwake kwa ajili ya kujibiwa na yeye?
 
Utu haukanyagi demokrasia, utu unaheshimu haki za raia, utu unalinda maisha ya binadamu, utu hauzibi pumzi ya mwezio, utu unatoa uwanja sawa wa mashindano, utu hauna uoga bali husimamia na kusimama na kweli daima!
 
Lazima ifike mahali tufanye mambo kwa kujiamini bhana, Prof Kabudi usiyumbishwe na kelele za wapiga makofi wa Mabeberu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Kazi kazi tu hakuna kucheka na beberu wala ndugu yake na beberu.
Ila ya mbogamboga tu.
 
Upuuzi mwingine wa karne hii!eti watasimsmia heshima,sio fedha,Mwalimu mwenyewe,alipopinduliwa na jeshi,aliwakimbilia hao hao wazungu kuomba msaada,
Jibuni hoja,heshima ipo wapi,wakati mlipokea pesa za corona,mkapiga kimya,hata wananchi hsmkuwaambia,harafu mnajigamba tunajenga nchi kwa pesa ya ndani,Kama mlikuwa hamzihitaji,mngezirudisha,ufichoni mpunga mnapokea,majukwaani,mnapayuka mabeberu Hawa hawatutakii mema,
 
Lazima ifike mahali tufanye mambo kwa kujiamini bhana, Prof Kabudi usiyumbishwe na kelele za wapiga makofi wa Mabeberu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Kazi kazi tu hakuna kucheka na beberu wala ndugu yake na beberu.
Ngoja wapige BAN dawa za Ukimwi tu kwa miezi japo 6 tu...Tutaheshimiana!
 
Jinga kabisa wewe
Kwani uongo hawakuchota mali zetu na kupeleka kwao?

Kama walibeba hadi kichwa cha Mkwawa, sembuse madini?

Wamebeba hadi masalia ya mijusi halafu nyie mpo mnakata mauno kuwasifia.

Wana husika sana katika underdevelopment of Africa hao vikaragosi wenu.
 
Niliipenda ila kwa bahati mbaya NJAAKALI hakumwelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…