Prof. Kabudi kuanza na Katiba Mpya

Prof. Kabudi kuanza na Katiba Mpya

Anko magu alishasema kabisa kipaumbele chake sio katiba mpya.
Anataka tanzania ya magufuli iwe ya viwanda na sio ya katiba mpya. Na uzuri alishasema hakuna wa kumpangia sasa sijui prof. ataendelezaje huo mchakato wa katiba mpya katika mazingira kama haya.
 
Thubutu.
Anajaribu kutikisa kiberiti cha Magufuli.
Kama hataonywa basi atatumbuliwa haraka sana. Hizo hoja za katiba mpya Magufuli alishasema hazitaki kabisa kuzisikia kwa sababu sio wakati wake na hazina maana kwake.
Huyu Prof. Alikuwa mpaka anatoa mapovu kuitetea katiba inayopendekezwa nadhani anaweza kuipigania
 
Naona prof. naye anataka kumjaribu mtukufu....
Inaelekea hajamsoma vizuri bado, atafanywa kama nape sasa hivi
 
Tunaanzia na tulipoishia.Tunasubiri kura ya maoni tu YES au NO!
Hapana. Kabudi ni miongoni mwa watu waliopinga vikali uchakachuaji wa rasimu ya 2 ya Warioba uliyofanywa na BMK chini ya hayati siťta.

Nakumbuka Palamagamba Kabudi aliwahi kurusha kijembe kwa serikali ya JK akisema "inashupaa" badala ya "kuduwa".
 
Kama akipata chansi inarudi ya warioba
Haahahahhaha mkuu mie nadoubt maana kma polepole kaikana hadharani na kitila mkumbo pia sioni wapi kabudi ataing'ang'ania!!!! I can picture him sayin KATIBA MPYA SIO AJENDA YA SASA WANANCHI WANATALA MAJI NA UMEME

anyway time will tell
 
Hapana. Kabudi ni miongoni mwa watu waliopinga vikali uchakachuaji wa rasimu ya 2 ya Warioba uliyofanywa na BMK chini ya hayati siťta.

Nakumbuka Palamagamba Kabudi aliwahi kurusha kijembe kwa serikali ya JK akisema "inashupaa" badala ya "kuduwa".
Mkuu ina maana kabudi alifight sana kwa ajili ya rasimu ya warioba kuliko polepole??? Ila leo hii polepoe mbona ametusaliti how can we rrust kabudi
 
Hapana. Kabudi ni miongoni mwa watu waliopinga vikali uchakachuaji wa rasimu ya 2 ya Warioba uliyofanywa na BMK chini ya hayati siťta.

Nakumbuka Palamagamba Kabudi aliwahi kurusha kijembe kwa serikali ya JK akisema "inashupaa" badala ya "kuduwa".
Tehehe tehe.Wengi wape,mchakato ulikfikia kwenye kura ya maoni.Tuikubali katiba pendekezwa au tuikatae
 
Hata nyie mnaweza kuikata katiba pendekezwa kwa kutumia makali yenu tukaendelea na katiba iliopo
Tukiikataa katiba pendekezwa na kuendeleaa na ya sasa AMA kuikubali katiba pendekezwa ni sawa na BURE. Hatujafanya kitu.
 
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuwa mchakato wa Katiba mpya uko pale pale.

Prof. Kabudi amesema hayo wakati alipokutana na Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge, amesema kuwa hajakutana na viongozi wake kuzungumzia suala la Katiba Mpya, ingawa anajua mambo mengine kuhusu mchakato huo ambao wakati wa maandalizi yake alikuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Amesema kuwa mchakato wa Katiba mpya uko pale pale hivyo pindi mchakato huo utakapo kamilika kwenye ofisi yake atauwasilisha kwenye kamati hiyo.

Aidha, Prof. Kabudi ameongeza kuwa ana muda mfupi katika wizara hiyo na kwamba, hajapata muda wa kukutana na mabosi wake akiwamo Waziri Mkuu, ili wazungumzie suala la Katiba Mpya.

Hata hivyo, amesema kuwa mchakato huo unahitaji umakini mkubwa hivyo atafanya kazi kulingana na utaratibu wa kisheria ili liwe na mwanzo na mwisho mzuri.

Chanzo: Dar24
Huyu hajitambui anajisemea tu, ndio mapropesa wetu! SIMSHANGAI KAMWE!
 
Kabudi, kitila, polepole..... Nawasubiri Sana hawa watu itakapofika saula la serikali 3
 
Back
Top Bottom