Prof. Kabudi ndio awe Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Apewe nafasi ya kukamilisha alichoanzisha

Prof. Kabudi ndio awe Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Apewe nafasi ya kukamilisha alichoanzisha

Kwa kuwa mchakato wa katiba mpya utaendelezwa panapo Majaliwa yake Mwenyezi Mungu mwaka ujao wa fedha 2023/2024 na tume maalumu itaundwa kufanikisha mchakato huo naona Prof.Kabudi atafaa sana kuwa Mwenyekiti wa bunge maalumu la Katiba.

Ni mwanasheria mzuri na mwenye uwezo mkubwa wa masuala ya katiba, anaifahamu vyema historia ya ukombozi wa nchi kabla na baada ya Uhuru, ni mzalendo wa kweli mwenye kuipenda Tanzania kwa dhati.

Ameshiriki kwa kiwango kikubwa kuandaa Rasimu ya Katiba ya Mzee Warioba hivyo kama mchakato wa katiba mpya utaendelezwa pale kwenye Rasmi ya Mzee Warioba basi Prof.Kabudi ndiye mtu sahihi wa kuendeleza mchakato huo na hata kama mchakato utaanza upya kabisa Prof.Kabudi ni mtu sahihi kwa uwezo na ujuzi wake katika masuala ya sheria na Katiba kutupatia katiba iliyo bora.

Ninaamini Prof.Kabudi ni mtu sahihi kabisa wa kutupatia katiba bora.
Kigeugeu hatufai hata bure
  1. Zile noah kwa kila mtanzania anasema siyo zetu
  2. Ile dawa ya madagascar alisema ni fake wakati wenyewe aliinywa na kuisifia
  3. Anasema ubunge alipewa na Mungu siyo wapigakura wake
 
Yani huyu Prof wa ovyo ndio asimamie katiba ya nchi...upuuzi yeye aendelee kubaki jalalani aliporudishwa
 
Kigeugeu hatufai hata bure
  1. Zile noah kwa kila mtanzania anasema siyo zetu
  2. Ile dawa ya madagascar alisema ni fake wakati wenyewe aliinywa na kuisifia
  3. Anasema ubunge alipewa na Mungu siyo wapigakura wake
Hoja namba tatu kama sio ushabiki basi omba toba na msamaha leo hii kwa Mungu. Kwa sababu ni Mungu mwenye kukirimu, kubariki na kutoa
 
Huyu amgeweza ila kwakuwa katiba mpya inagusa na maslahi ya watu lazima watampiga zengwe...
 
Kabudi hafai, ameyumba msimamo.

Mzee WARIOBA ndio chaguo sahihi.

Tumtumie vizuri Ili akamilishe mission yake na furaha yake iwe ya milele katika kurasa za kumbukumbu Kwa Taifa letu.

Bring back our WARIOBA 💪💪💪💪
 
Yaani umekuja kungwa Mkono hoja yako hapa JF , [emoji23][emoji23][emoji23].

Bora mngefanya veting huko huko na Kumuweka kuliko kutafuta maoni hapa.
 
Back
Top Bottom