Prof. Kitila Mkumbo ataka bajeti ieleze namna inavyoshughulikia mfumuko wa bei

Prof. Kitila Mkumbo ataka bajeti ieleze namna inavyoshughulikia mfumuko wa bei

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mbunge wa Ubungo akichangia katika bunge la Bajeti leo amesema ongezeko la bei linaloendelea mtaani sio la kawaida. Amesema ongezeko lililopo sio makosa ya serikali hata hivyo ni muhimu kwa serikali kuchukua hatua za dharura kudhibiti ongezeko hilo

Ameshauri wizara ya fedha kuja na hatua rasmi ili ziwepo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23. Aidha amesema katika tozo zilizopo serikali ikubali kuondoa walau Tsh 300 katika mafuta ili wananchi wapate unafuu na kuhusu miradi inayoendelea serikali inaweza kukopa ili kui-finance miradi hiyo badala ya kutegemea kodi na tozo ambazo zinawaongezea wananchi ugumu wa maisha

“Naweza kushauri tukachukua Sh. 300 mpaka 400, tukaondoa kwa muda mfupi tukitarajia Julai au Agosti, hali itarudi kawaida. Tukifanya hivyo tutampunguzia mwananchi ukali wa maisha. Hizo fedha zinazopungua kwenye miradi ya maendeleo, Serikali yetu inakopesheka, ikope ili miradi ya maendeleo isisimame,” amesema Prof. Mkumbo.
 
Watu mna moyo.
Hata maoni ya Kitila mnayasikiliza?
 
Mama endelea kushikilia hapo. Ongeza na tozo kutembea barabarani.

Tunataka kufikia 2025 tukapige kura wote tukiwa tuna akili timamu.
Ccm uwa hawahitaji kura zetu masandarusi yapo 🤣
 
Mama endelea kushikilia hapo na ongeza na tozo a kutembea barabarani.

Tunataka kufikia 2025 tukapige kura wote tukiwa tuna akili timamu.

😂🤣😐🤣😐🤣🤣🤣🤣
 
Mbunge wa Ubungo akichangia katika bunge la Bajeti leo amesema ongezeko la bei linaloendelea mtaani sio la kawaida. Amesema ongezeko lililopo sio makosa ya serikali hata hivyo ni muhimu kwa serikali kuchukua hatua za dharura kudhibiti ongezeko hilo

Ameshauri wizara ya fedha kuja na hatua rasmi ili ziwepo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23. Aidha amesema katika tozo zilizopo serikali ikubali kuondoa walau Tsh 300 katika mafuta ili wananchi wapate unafuu na kuhusu miradi inayoendelea serikali inaweza kukopa ili kui-finance miradi hiyo badala ya kutegemea kodi na tozo ambazo zinawaongezea wananchi ugumu wa maisha

“Naweza kushauri tukachukua Sh. 300 mpaka 400, tukaondoa kwa muda mfupi tukitarajia Julai au Agosti, hali itarudi kawaida. Tukifanya hivyo tutampunguzia mwananchi ukali wa maisha. Hizo fedha zinazopungua kwenye miradi ya maendeleo, Serikali yetu inakopesheka, ikope ili miradi ya maendeleo isisimame,” amesema Prof. Mkumbo.
Safi sana
 
Back
Top Bottom