Prof. Kitila Mkumbo: Kazi ya Serikali sio Kugawa Hela, Serikali inaajiri Watu 5 kati ya 100

Prof. Kitila Mkumbo: Kazi ya Serikali sio Kugawa Hela, Serikali inaajiri Watu 5 kati ya 100

Ndugu zangu.
Shibe siyo jambo baya, lakini mlevi akishiba hupata nguvu ya kuongea lolote
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amesema Kazi ya Serikali si kugawa Fedha bali ni kutengeneza mazingira ya kupata Fedha na ili kupata Fedha inaamanisha Watu wafanye kazi na kazi zinatoka kwenye biashara.

Ameongeza kuwa "Kazi zinatoka wapi? Wengi wataongelea Serikalini au kwenye mashirika ya Umma lakini mimi nasema kazi zinatoka kwenye Biashara. Ni kweli Serikali inaajiri lakini watu kidogo sana katika watu 100 wanaoajiriwa Tanzania kila siku, Serikali inaajiri watu 5 tu, waliobaki wanaajiriwa na sekta binafsi na sekta binafsi maana yake nini ni biashara".

Akizungumza na CloudsTV leo Nov 29, 2023, amesema Serikali inachokiangalia ni kwa kiasi gani imechangamsha Biashara nchini na biashara hizo zimechamka zaidi wakati huu kulinganisha na miaka 20 iliyopita hata kama hazijafikia kiwango kinachotakiwa.

Kwa mujibu wa Kwa mujibu ripoti ya Taasisi ya Utafiti na Kupunguza Umasikini Tanzania (REPOA) ya 2019, takriban vijana 1,000,000 wanahitimu masomo kila mwaka kutoka Taasisi mbalimbali za Elimu nchini huku idadi ya ajira zinazozalishwa kutoka Serikalini na Sekta Binafsi ni 250,000 pekee.

Idadi hiyo ni sawa na Wastani wa Muhitimu Mmoja kutumia Miaka 5.5 kupata ajira nchini Tanzania
 
Huwa wanakera wanaposema wahitimu
Sasa kama tuna wahitimu kwanini wanapeleka wafanyakazi wa ndani kusafisha vyoo vyao na kunyanyaswa huko

Kwanini hawasemi tumepeleka wauguzi au engineers?
Hatuna elimu bali kukariri tu
Waliojaaliwa tena vichwa haswa ni wachache sana na hao wanapigwa vita kama yule mama alietangaza Zika wakati ule akatimuliwa na kupata kazi nje

Wapo ila tunataka watengengenezwe wengi kama hao la sivyo wafunge midomo
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amesema Kazi ya Serikali si kugawa Fedha bali ni kutengeneza mazingira ya kupata Fedha na ili kupata Fedha inaamanisha Watu wafanye kazi na kazi zinatoka kwenye biashara.

Ameongeza kuwa "Kazi zinatoka wapi? Wengi wataongelea Serikalini au kwenye mashirika ya Umma lakini mimi nasema kazi zinatoka kwenye Biashara. Ni kweli Serikali inaajiri lakini watu kidogo sana katika watu 100 wanaoajiriwa Tanzania kila siku, Serikali inaajiri watu 5 tu, waliobaki wanaajiriwa na sekta binafsi na sekta binafsi maana yake nini ni biashara".

Akizungumza na CloudsTV leo Nov 29, 2023, amesema Serikali inachokiangalia ni kwa kiasi gani imechangamsha Biashara nchini na biashara hizo zimechamka zaidi wakati huu kulinganisha na miaka 20 iliyopita hata kama hazijafikia kiwango kinachotakiwa.

Kwa mujibu wa Kwa mujibu ripoti ya Taasisi ya Utafiti na Kupunguza Umasikini Tanzania (REPOA) ya 2019, takriban vijana 1,000,000 wanahitimu masomo kila mwaka kutoka Taasisi mbalimbali za Elimu nchini huku idadi ya ajira zinazozalishwa kutoka Serikalini na Sekta Binafsi ni 250,000 pekee.

Idadi hiyo ni sawa na Wastani wa Muhitimu Mmoja kutumia Miaka 5.5 kupata ajira nchini Tanzania
Mpuuzi apuuzwe mwanzoni.
Zile ajira milioni 3 mlisema mtatoa ilikuwa ni milioni 3 kwa watanganyika milioni 300?
 
Kama anajua hivyo wapunguze kodi, tozo, ushuru na ada kwenye biashara sasa.
Waachane pia na V8, badala yake waanze kutumia IST kupunguza matumizi mabaya ya hela.
 
Sawa hilo liko wazi na ingekuwa yema ikaeleweka hivyo lakini mbona mazingira ya kujiajiri kwa Tanzania ni magumu kupitiliza sio rafiki ukisema uanzishe biashara yako utakumbana na urasimu wa hali ya juu na tozo pamoja na kodi kiasi kwamba kama huna ujasiri lazıma ukate tamaa. Hawa wanasiasa hasa mawaziri wamezoea porojo kila wapatapo jukwaa la kupiga porojo zoo kama hapa Kitila anavyoendeleza porojo anaongelea vijana kujiajiri bila kuwa na mazingira rafiki kwa vijana kufanya hivyo.
 
Back
Top Bottom