Prof. Kitila Mkumbo: Serikali za Mtaa hazishauri Serikali Kuu badala yake zinapokea maelekezo kutoka Serikali Kuu

Prof. Kitila Mkumbo: Serikali za Mtaa hazishauri Serikali Kuu badala yake zinapokea maelekezo kutoka Serikali Kuu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mbunge wa Ubungo, Kitila Mkumbo amesema serikali za mtaa hazishauri serikali kuu kama ilivyopangwa badala yake zinapokea maelekezo kutoka serikali kuu. Wananchi wanabaki kushangilia mafanikio ya serikali badala ya kuwa sehemu ya mafanikio ya serikali.

Mbunge ameyasema hayo bungeni ambapo amesema ushirikishwaji wa wananchi bado ni finyu na hivyo zinanyima uhuru wa serikali za mtaa.
 
Mbunge wa Ubungo, Kitila Mkumbo amesema serikali za mtaa hazishauri serikali kuu kama ilivyopangwa badala yake zinapokea maelekezo kutoka serikali kuu. Wananchi wanabaki kushangilia mafanikio ya serikali badala ya kuwa sehemu ya mafanikio ya serikali

Mbunge ameyasema hayo bungeni ambapo amesema ushirikishwaji wa wananchi bado ni finyu na hivyo zinanyima uhuru wa serikali za mtaa
SM nyingi bado ni tegemezi kimapato kutoka serikali kuu. Zinaishi kwa Ruzuku hiyo nguvu ya kushauri serikali kuu zitatoa wapi?
 
Marofesa wa bongo njaa tupu
Hili lilipora ubunge
 
Mbunge wa Ubungo, Kitila Mkumbo amesema serikali za mtaa hazishauri serikali kuu kama ilivyopangwa badala yake zinapokea maelekezo kutoka serikali kuu. Wananchi wanabaki kushangilia mafanikio ya serikali badala ya kuwa sehemu ya mafanikio ya serikali.

Mbunge ameyasema hayo bungeni ambapo amesema ushirikishwaji wa wananchi bado ni finyu na hivyo zinanyima uhuru wa serikali za mtaa.
Good point. Tangu ameachwa kwenye baraza la mawaziri amekuwa akifanya kazi nzuri kuliko alipokuwa waziri.
 
Ni sawa na Tz ishauri USA...

Ukiwa huna hela hakuna jambo utashauria,,, lazima usikilize watoa hela...

Katiba itatakiwa iweke vizuri hilo swala pia
 
Muulize Bashe, leo kaambiwa matreka yake yanakatika katikati, sijui kama alitoka maelezo au hata yeye hakuwa anajua hilo maana ni suti na V8 top!!!!!
 
Mbunge wa Ubungo, Kitila Mkumbo amesema serikali za mtaa hazishauri serikali kuu kama ilivyopangwa badala yake zinapokea maelekezo kutoka serikali kuu. Wananchi wanabaki kushangilia mafanikio ya serikali badala ya kuwa sehemu ya mafanikio ya serikali.

Mbunge ameyasema hayo bungeni ambapo amesema ushirikishwaji wa wananchi bado ni finyu na hivyo zinanyima uhuru wa serikali za mtaa.
Hii inatokana na incompetence ya mamlaka za serikali za mitaa.

Pia muundo hauko sawa,Mkurugenzi hakutakiwa kuwa muajiriwa wa serikali kuu.
 
Unadhani Nini kibadilike kwenye serikali za Mitaa hasa kimuundo?
Wakurugenzi waajiriwe na Baraza la madiwani..

Pili vigezo vya mtu kuwa diwani vipitiwe upya na tatu wananchi wapewe nguvu ya kuondoa diwani yeyote bila kusubiria uchaguzi kwa ku sign petition ya kura kadhaa zenu tunaanza mchakato,mshindi wa pili anachukua nafasi bila kuingia kwenye uchaguzi mwingine..

Pili uwakilishi uhusishe vyama vya hiari kama NGOs,makundi maslahi nk..

Kwa sababu uzoefu unaonyesha Baraza la madiwani haliwezi kabisa kuisimamia Halmashauri ndio maana wizi na ujenzi wa miradi chini ya kiwango na inefficiency ni kubwa kweyutoaji huduma achilia mbali maamuzi ya kisenge kisenge yasiyojali maslahi ya umma..

Hii ndio inasababisha Serikali kuu iwe inaonekana iko in charge moja kwa moja.

Na jambo jingine kila Halmashauri ijitegemee.Hii ya kuchukua pesa za Ubungo kupeleka Lindi haikubaliki ,inalea uzembe.
 
Wakurugenzi waajiriwe na Baraza la madiwani..
Kwasasa Sheria inayounda mamlaka ya serikali za Mitaa, inawapa Madiwani mamlaka ya kinidhamu kwa Watumishi wa umma.

Suala hili limekuwa Ni kero sana has katika nchi yet ambayo watu wengi tunaishi kwa Unafiki na CHUKI.

Kutokana na suala hili, mpaka sasa Kuna mapendekezo kuwa badala ya Madiwani kuwa na mamlaka ya kinidhamu kwa Watumishi wa umma, Ni Bora Jambo hili likawa kwenye mamlaka ya Tume ya Utumishi mkoa.
Pili vigezo vya mtu kuwa diwani vipitiwe upya
Vipitiwe upya na Nani?

Wananchi wetu wakoje, maana isije kuwa unaweka vigezo ambavyo sasa itabidi Wananchi waanze kutafuta watu kutoka nje ya maeneo yao kuja kuwa Viongozi kitu ambacho siyo demokrasia.
Demokrasia Ni kuchagua mtu unayempenda na unaridhika naye hata kama Ni hajui kusoma Wala kuandika.
tatu wananchi wapewe nguvu ya kuondoa diwani yeyote bila kusubiria uchaguzi kwa ku sign petition ya kura kadhaa zenu tunaanza mchakato,mshindi wa pili anachukua nafasi bila kuingia kwenye uchaguzi mwingine..
Siasa zinazohusisha watu wengi, Ni rahisi kuwa manipulated.

Tunashiriki VICOBA na SACCOS zinazoongozwa kidemokrasia na tunaliona hili. Siyo Jambo rahisi kuweka msimamo was pamoja kwenye taasisi za watu wengi wenye itikadi, hisia na imani tofauti.
Pili uwakilishi uhusishe vyama vya hiari kama NGOs,makundi maslahi nk.
Kwa sababu uzoefu unaonyesha Baraza la madiwani haliwezi kabisa kuisimamia Halmashauri ndio maana wizi na ujenzi wa miradi chini ya kiwango na inefficiency ni kubwa kweyutoaji huduma achilia mbali maamuzi ya kisenge kisenge yasiyojali maslahi ya umma..

Hii ndio inasababisha Serikali kuu iwe inaonekana iko in charge moja kwa moja.

Na jambo jingine kila Halmashauri ijitegemee.Hii ya kuchukua pesa za Ubungo kupeleka Lindi haikubaliki ,inalea uzembe.
Suala la miradi kuwa chini ya kiwango sidhani kama issue ni Madiwani.

Issue kubwa hapa Ni SIASA ZA MASLAHI.
 
Back
Top Bottom