Prof. Kitila: Rais Samia Ametunza Amani, Usalama na Utulivu wa Nchi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, amesema kwamba Rais Samia Suluhu Hassan amefanikiwa kutunza hali ya usalama na amani nchini tangu alipoapishwa kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais awamu ya tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Mabibo, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, ambapo pia ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Prof. Kitila alisema, "Kazi ya kwanza ya Rais ni kuhakikisha kwamba nchi anayoiongoza ina amani, usalama na utulivu. Rais Samia amefaulu katika hili, ndiyo maana anaitwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania."

Alisisitiza kwamba Tanzania bado ina amani na utulivu, licha ya changamoto zinazoweza kutokea wakati wa mabadiliko ya uongozi. “Nchi zinapoondokewa na Mkuu wa Nchi huwa zinayumba, lakini Rais Samia amefanikiwa kuibakisha Tanzania kuwa salama,” aliongeza Prof. Kitila.
Your browser is not able to display this video.
 
 
Profesa uchwara huyo,hivyo ndivyo watu wanavyo aibika,hata ukijifanya msomi mwisho watu watakufahamu tu,ndio unaonekana umesoma lkn AKILI huna.
 
Profesa uchwara huyo,hivyo ndivyo watu wanavyo aibika,hata ukijifanya msomi mwisho watu watakufahamu tu,ndio unaonekana umesoma lkn AKILI huna.
Akiwa CHADEMA Profesa, akiama, Uchwara?
 
Wakati ww unakoroma usiku kitandani kwako na mkeo, watu wako doria uku nje na uko mipakani mwa nchi ili kukufanya wewe ukorome na mkeo raha mustarehe.
Si wanalipwa lakini kwani ni kazi ya kujitolea na watu waliomba wenyewe.
 
Ni lini Amani Tanzania ilitoweka?. Profesa chawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…