Prof. Lipumba na nadharia ya "cash economy"

Prof. Lipumba na nadharia ya "cash economy"

JERRY

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2009
Posts
630
Reaction score
502
Juzi mtalaamu wa Uchumi na Mwenyekiti wa CUF Prof. I.Lipumba alitoa darsa la uchumi na jinsi gani Tanzania inaweza kutoka hapa tulipo kutokana na sera mbovu za CCM. Lakini mi japo sio mchumi napata shaka na namna yy prof.na CUF yake watavyoweza kutekeleza sera hii ya kuwapa watu hela kama ni on monthly basis sijui? maana sikuwepo.

Nchi kama za scandinavia, italy na kwingineko hii sera ilikuwepo huko nyuma ila kwa sasa haitumiki kwani ime- prove failure na hii ni kutokana na mazingira ya sasa ya uchumi wa dunia "GLOBAL ECONOMY". Mi nilizani angeleza namna CUF itavyoweza kutengeneza mazingira/fursa bora ili kumwezesha hata mtu wa chini kabisa kutumia fursa hizo kujitengenezea maisha bora, kama tunavyoona kwa nchi ya Rwanda sasa ivi.

Pengine wachumi watusaidie ktk hili, vinginevyo mimi naona kama hii ni NADHARIA zaidi na pengine kauli ya kisiasa, ni kitu kisichowezekana kabisa ktk mazingira ya sasa Tanzania
 
juzi mtalaamu wa uchumi na mwenyekiti wa cuf prof. I.lipumba alitoa darsa la uchumi na jinsi gani tanzania inaweza kutoka hapa tulipo kutokana na sera mbovu za ccm.
Lakini mi japo sio mchumi napata shaka na namna yy prof.na cuf yake watavyoweza kutekeleza sera hii ya kuwapa watu hela kama ni on monthly basis sijui? Maana sikuwepo.
Nchi kama za scandinavia, italy na kwingineko hii sera ilikuwepo huko nyuma ila kwa sasa haitumiki kwani ime- prove failure na hii ni kutokana na mazingira ya sasa ya uchumi wa dunia "global economy".
Mi nilizani angeleza namna cuf itavyoweza kutengeneza mazingira/fursa bora ili kumwezesha hata mtu wa chini kabisa kutumia fursa hizo kujitengenezea maisha bora, kama tunavyoona kwa nchi ya rwanda sasa ivi.
Pengine wachumi watusaidie ktk hili, vinginevyo mimi naona kama hii ni nadharia zaidi na pengine kauli ya kisiasa, ni kitu kisichowezekana kabisa ktk mazingira ya sasa tanzania
kwa nchi yenye utajiri kama tz tukiondoa ufisadi na maliasili ikitumika sawa inawezeka
kwa mfano gas ilio vumbuliwa tz pamoja na uwezekano mkubwa wa kupatikana mafuta na pia utajiri wa madini basi hili linawezekana bila ya shida
  • kuwait mtoto akizaliwa tu anawekewa $ 40,000 kwenye account yake, na wasiokuwa na kazi above 18 wanapata posho sawa na mshahara wa chini,eleimu mpaka chuo kikuu bure, afya bure,umeme bei poa,petrol na gas ya nyumbani kama bure,wazee wanapewa penseni ya kutosha
  • saudia pia hali ni kama hio
  • uae raia wake wana enjoy uchumi wa nchi yao, afya bure, elimu kwa wasio kuwa na uwezo bure,mafuta na gas kama bure , wazee wanalipwa penseni ya kutosha
  • hali nio pale libya alipokuwa ghadafi
  • venezuela pia kuna kuwezeshwa kwa raia ndio maana kumundoa chavez ni kazi kubwa
  • hata uingereza huna kazi basi unapata posho ya bure na nyumba
sera hii inaweezekana tu kama ubinafsi utaondoka na watu kuweka maslahi ya umma na taifa mbele
cha kwanza ni kufanya ajira kwa wingi
kila mmoja alipe kodi
 
kuna kipindi lipumba aliwaahidi wananchi wa kusini akiingia maadarakni atawaruhusu kulima pamba wakati inajulika mikoa ya kusini ilizuiliwa kulima pamba kutokana na mdudud aitwaye red ball worm aliyeko msumbiji jamaa ni heri arudi chuoni akafundishe
 
Me nadhani inawezekana kabisa. Kwa maana ukiangalia kiuhalisia sisi kama nchi tuna rasilimali ambazo zikifanyiwa matumizi sahihi kwa maana zikiwekezwa katika namna sahihi basi tunaweza kutengeneza kipato cha uhakika. Tatizo pesa inakwenda mahala au maeneo ambayo mrejesho wa productivity ni sifuri. Kwa staili hii tutaishi maisha haya haya miaka yote kwa maana hakuna jipya kiukweli. Ila naamini tukianza kujihoji tunaelekea wapi na kubadili mfumo wa maisha tutaweza kufika mbali.
 
Back
Top Bottom