Prof. Mohamed Janabi Miongoni mwa Wagombea wa Ukurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika

Prof. Mohamed Janabi Miongoni mwa Wagombea wa Ukurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika

Wampe, sio tu kwa Heshima ya Marehemu Dr. Ndungulile, bali pia anaweza sana, na ni mtendaji halisi sio politician.
Labda hukusoma resumè ya Dr Ndugulile!! Kwanza yeye binafsi alikuwa anajitosheleza.

Aliji involve kabla na shughuli nyingi za WHO kama 6-7 years before. Kwa hiyo hata waliokuwa wanamuuza ki-diplomasia hawakuwa na ugumu.

Sasa huyu candidate wako utachukua zile clip zake za kukataza kula chapati ma magimbi ndiyo upeleke kwa wapiga kura wa WHO-Afro?
 
Labda hukusoma resumè ya Dr Ndugulile!! Kwanza yeye binafsi alikuwa anajitosheleza.

Aliji involve kabla na shughuli nyingi za WHO kama 6-7 years before. Kwa hiyo hata waliokuwa wanamuuza ki-diplomasia hawakuwa na ugumu.

Sasa huyu candidate wako utachukua zile clip zake za kukataza kula chapati ma magimbi ndiyo upeleke kwa wapiga kura wa WHO-Afro?
😀
 
Anaandika Zanzibar-ASP :-
Mara baada ya Rais Samia kutangaza kumpigia debe Professor Janabi ili kuiwakilisha Tanzania kwenye kinyang'anyiro cha ukurugenzi mkuu wa WHO kanda ya Afrika, watu wenye akili kubwa ikabidi waingie chimbo kufukua file lenye kubeba wasifu mbali mbali kumhusu Profesa Mohamed Janabi ili kuona ana kipi cha kielimu na kisayansi, na sasa imekuja kugundulika kuwa, kumbe mwamba hakuwahi kusomea udaktari bingwa wowote (Mmed) achilia mbali udaktari bingwa wa moyo (Cardiologist) na wala hana sifa zozote stahiki za kibingwa kutibu moyo.

Na kwa mifumo ya mamlaka za usimamizi wa fani ya utabibu hapa Tanzania (Medical Council of Tanganyika), daktari asiyekuwa na sifa za kibingwa za fani huzika haruhusiwi kutoa matibabu ya kibingwa moja kwa moja kwa mgonjwa, na kwa tafsiri ya moja kwa moja, Professor Janabi hakuwahi popote moja kwa moja kutibu kibingwa moyo, na kama aliwahi kufanya hivyo anastahili kushtakiwa kwenye baraza la madaktari kwa kutenda kosa la kimaadili katika fani ya udaktari.

Hapa chini nimeambanisha wasifu wa Professor Janabi wa kidaktari unaotambulika na mamlaka za usimamizi wa taaluma ya udaktari hapa Tanzania (MCT).

Mwisho kabisa, MCT wanatakiwa kutoa maelezo kwa umma, kwa hicho ulichowahi kusomea Professor Jababi (Masters of tropical health) ambacho hakina sifa yoyote ya udaktari bingwa wa moyo (maana mhitimu yoyote wa fani ya afya anaweza kusomea), kinampaje sifa mhusika kuwa daktari bingwa wa moyo?

NOTE:
Daktari bingwa mbombezi (kama daktari bingwa wa moyo) yoyote mwenye sifa stahiki za kutambulika na baraza la madaktari la Tanganyika (MCT) ni lazima utambulisho wake kwenye ukurasa rasmi wa MCT (Professional Profile status) usomeke SUPER SPECIALIST DOCTOR. Kwa Professor Janabi hakuna hicho kitu.


Cc imhotep , bagamoyo, DR Mambo Jambo
Hii ni kweli 💯...
Kila siku anauzungumzia moyo kama kausomea vile kumbe kilaza fulani!
 
PROFESA Mohamed Janabi, jina lake limetangazwa rasmi kuwa miongoni mwa wagombea watano katika kuwania nafasi ya Mkurugenzi wa Kanda ajaye wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa Kanda ya Afrika.

Prof. Janabi, ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) anawania kiti hicho pamoja na wenzake miongoni mwao kutoka nchi za Afrika Magharibi.

Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, limetoa taarifa hiyo. Majina ya wagombea hao ambayo yatafanyiwa mchakato wa Uchaguzi Mei 18, mwaka huu, yaliwasilishwa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk. Tedros Adhanom Ghebreyesus.

Soma Pia: Rais Samia ampendekeza Profesa Janabi kuwa Mkurugenzi wa WHO-Afrika

Nchi wanachama yaliwasilishwa majina hayo kwa kiongozi huyo, leo, Machi 14, 2025 huku nchi tano ikiwamo Tanzania na nyingine nne Ivory Coast; Togo; Niger na Guinea pia wakifanya hivyo.

Wagombea kutoka nchi zingine ni Dk. N'da Konan Michel Yao kutoka Ivory Coast; Dk. Dramé Mohammed Lamine (Guinea); Dk. Boureim Hama Sambo (Niger); na Pr Mijiyawa Moustafa wa Togo.
Mbona jina la Kasim Majaliwa limekatwa au alipomaliza chuo hakwenda VETA?
 
CV ya Prof Janabi imekaa vizuri kuliko washindani wake. Anayo nafasi kubwa kuwa mshindi wa nafasi husika huko WHO.
 
CV ya Prof Janabi imekaa vizuri kuliko washindani wake. Anayo nafasi kubwa kuwa mshindi wa nafasi husika huko WHO.
Unaifahamu basic educational requirement ya kazi ya Director-WHO AFRO?
 
Tunashauri wagombea wote wa nafasi hizi,Moja ya kigezo cha kufanya interview,kiwe, mgombea kupimwa afya yake na wapimwe na wataalam wa WHO.
Kabisa

Apimwe afya barabara huyo Profesa

Tanzania tusigeuze ofisi za WHO kama sehemu ya wadi ya wagonjwa

Profesa Janabi apimwe afya barabara

WHO wasisitize wagombea wote kupimwa afya zao na independent medical practitioners

Walio physically fit tu ndio wagombee kuepukq kurudia rudia chaguzi au mtu kutwa kushinda hospital kwa matibabu
 
CV ya Prof Janabi imekaa vizuri kuliko washindani wake. Anayo nafasi kubwa kuwa mshindi wa nafasi husika huko WHO.
Swala ni afya yake iko fit? Ndugulile pia CV yake ilikuwa vizuri lakini afya ilikuwa mgogoro
 
Kabisa

Apimwe afya barabara huyo Profesa

Tanzania tusigeuze ofisi za WHO kama sehemu ya wadi ya wagonjwa

Profesa Janabi apinwe afya barabara

WHO wasisitize wagombea wote kupimwa afya zao na independent medical practitioners

Walio physically fit tu ndio wagombee kuepukq kurudia rudia chaguzi au mtu kutwa kushinda hospital kwa matibabu
Kwa utaratibu huu,Janabi,atakwepa Interview
 
Kitakachomponza huyu ni affiliation yake na Watawala! Ukiangalia comments, Marehemu alipokelewa na watanzania Kwa ujumla wake sababu alikua na integrity ya kipekee! Hilo halina ubishi hata kidogo!
Sioni Lucas akimpigia kampeni sijajua kwanini mana anawajua watu wote sifa na sifu wao. Sioni Akienda kushinda kama na Mama Jenista ataemda pia kumnandi, akanza na on behalf of myself
Aah hahahaaa !
 
Hakuna uchawa kule! Hatoboi
Uchawa upo Francaphone watamchagua kati ya nchi zinazozungumza kifarasa.
Pili wagombea wote wanatokea Africa Magharibi ni wazi nchi za West Africa zitapigia kurs kwa watu wao.
 
Back
Top Bottom