PROF. MUKANDALA M/KITI BODI NECTA: Mbona Kimya?

PROF. MUKANDALA M/KITI BODI NECTA: Mbona Kimya?

M24 Headquarters-Kigali

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2012
Posts
8,199
Reaction score
8,186
Wakati taifa linaelea juu juu kwa matokeo ya Kidato cha 4 ya mwaka 2012 nilitegemea Mwenyekiti huyu wa bodi ya NECTA aseme lolote but sijamsikia akiongea lolote au ndo bora liende? Wewe ni msomi, mtawala & Mtafiti mzuri sana unaheshimika Tanzania na Duniani kote kwa machapisho yako (Vitabu, Makala ktk Majarida ya Wasomi) lakini mbona upo kimya pamoja uozo ambayo taasisi yako unayoongoza bodi yake (NECTA) imetuhumiwa?
 
necta hawausiki ata kidogo tatizo ni serikali ya ccm mkuu hao akina prof rwekaza na dr ndalichako wanaonewa tu serikali yenyewe wanajua kua necta wanaonewa.
 
Wakuu katika hili siami hata kidogo kama tatizo ni Baraza la Mitihani. Namfahamu Prof Mukandala kiongozi wetu hapa Mlimani yuko makini sana katika utendaji wake. Sidhani kama Prof Mukandala angeweza kuruhusu Bodi anayoiongoza ifanye madudu kiasi hicho anachotaka kutuaminisha Lukuvi. Hapo ni dhahiri kuwa Kawambwa yuko taabani wizara imemshinda kabisa kuisimamia sasa anatafuta pa kupumulia kwa kutaka kuchafua majina ya watu wengine.

Prof Mukandala tunaimani kubwa sana na wewe tunaomba uvunje ukimya ili jina lako tukufu linaloheshimiwa ndani na nje ya nchi lisichafuliwe na huyo Kawa Mbwa ambaye ameshindwa kuongoza kila Wizara aliyopangiwa. Sijui kwa nini Mh Rais amemuacha muda mrefu hapa Elimu ambako ameiharibu kabisa
 
Prof Mukandala kwa nini Bodi yako haimuwajibishi Katibu Mtendaji maana umma umechanganyikiwa au kuna siri gani kuhusu hiyo kauli ya Lukuvi mbona NECTA wote Katibu ma Mwenyekiti wa Bodi mko kimya sana? Tunataka kujua ukweli wa mambo na aliyehusika kuleta usumbufu huuawajibishwe
 
ki ukweli hata mi na sikitishwa sana na suala la necta kukaa kimya kiasi hk. mbaya zaidi kuna tetec kwamba body ya miko imesha tangaza muda ambao wanafunz wanao taka kujiunga na vyuo vikuu wafanye aplication za mikopo hiyo huku wakiwa hawajui kama wame faulu ama wame feli... hili li 2acha njia panda watu weng hasa sisg ambao ndo 2me maliz 4m six mawaka huu. kwanza atuna tempo wala nin wazaz wata 2elewaje na kutu amini kiac cha ku2 ruhusu kufanya aplicmtio kabla ya kujua matokeo husika.. serikali mna boa bhanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa! kama 2me feli wote tuambieni2...... 2mesha zoea maumiv co 2ta yapokea cya kwe2........!
 
Wakati taifa linaelea juu juu kwa matokeo ya Kidato cha 4 ya mwaka 2012 nilitegemea Mwenyekiti huyu wa bodi ya NECTA aseme lolote but sijamsikia akiongea lolote au ndo bora liende? Wewe ni msomi, mtawala & Mtafiti mzuri sana unaheshimika Tanzania na Duniani kote kwa machapisho yako (Vitabu, Makala ktk Majarida ya Wasomi) lakini mbona upo kimya pamoja uozo ambayo taasisi yako unayoongoza bodi yake (NECTA) imetuhumiwa?

Kwa bahati nzuri alinifundisha pia darasani....Nakumbuka aliipenda sana definition ya Harold Dwight Lasswell kuwa Politics is who gets what, when, and how.

BACK TO THE TOPIC, Kwa muktadha huo yeye pia ni muhanga wa maagizo ya wanasiasa. Wewe ukitaka kujua nguvu ya siasa ni pale Mulugo anapokuwa bosi wa Mukandala.....yaani huwa natamani hata kulia...
 
Back
Top Bottom