Prof. Shivji apinga sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema

Hivi, ni hoja hiyo tu ndio imemrudisha Lema jimboni? vipi hoja zingine. Shivj na wengine je, Lema alipaswa asishinde rufaa? kwa hizo hoja zenu?
 

Let's start this thought experiment.

Say kuna mtu mwanachama wa FUC, mkazi na mpiga kura wa Chake Chake Pemba. Alikuwa na access na high level strategic meetings za FUC huko Chake Chake Pemba.

Katika hizo strategic meetings, candidate wa ubunge wa FUC Muleba katoa mchongo wa kushinda kwa kuhonga wahesabu kura wote strategy limeshapangwa, documents zipo, ma bank transfers yapo. Piga ua galagaza lazima ashinde ubunge Muleba ili aende ku introduce sheria fulani to an unsuspecting parliament ili kuruhusu takeover fulani katika biashara ya mafuta kwa WaIran. Huyu mtu ana documents za alliance na hawa waIran wamuendeshe kama remote control, awapatie parliamentary access to information.

Uchaguzi unapita, huyu mgombea wa FUC anashinda Muleba, kwa rushwa. Ushahidi wote huyu mjumbe wa FUC wa Chake Chake anao, anaweza kuuwakilisha mahakamani.

Nafsi yake inamsuta kwani anaelewa ubunge hawajashinda kihalali, na zaidi ya hapo mbunge hana nia nzuri na nchi kuna a conspiracy inaandaliwa.

Huyu mjumbe wa FUC asiwezeshwe kuchallenge ubunge wa huyu mbunge wa Muleba kwa sababu tu si mpiga kura wa Muleba?

Au si mgombea aliyeshindwa Muleba?

This scenario may read like a hyperbole from an overly excited mind, but it is actually very plausible under our current conditions.
 
hii mada mlkua mnajadili lakin toka mlipoanza tumia hii lugha ya kitumwa mmeharibu mambo...
 
Hawa majaji pamoja na mawakili wa Lema wanataka kutuambia kuwa ubunge ni ajira.ndio maana wanajikita kwenye hoja kwamba wajibu rufani wathibitishe ni jinsi gani walivyoathirika wao binafsi.Hii si kweli kabisa ubunge ni uakilishi wa eneo fulani ambapo mtu atakayechaguliwa kwa mujibu wa sheria.Ni mkataba kati ya wananchi wa eneo hilo na mbunge(social contract) sasa kama maneno ya kibaguzi na kashfa yalitolewa na mkatarufaa na kusikiwa na wajibu rufaa na maneno hayo ni kinyume na sheria ya uchaguzi kwa nini wakose locus standi?hayo maneno yaliwaathiri moja kwa moja wajibu rufaa kwa sababu matakwa yao yalikuwa wampate kiongozi aliyetokana na free and fair election. kwa kuwa maneno yaliotumika yalimuwezesha mkatarufaa kushinda uchaguzi huo basi haukuwa fair kwa sababu baadhi ya watu wakiwemo wajibu rufaa walikuwa prejudiced.kwa kuwa uotcomes ya matokeo yalikuwa na effect kwa wajibu rufaa kuona kuwa wanampata kiongozi aliyechaguliwa kwa kufuata sheria ya uchanguzi, na kwa kuwa maneno hayo yalikuwa kinyume na sheria hiyo na yakaweza kusababisha baadhi ya wapiga kura kuyaamini na kumpa ushindi hivyo basi wajibu rufaa walikuwa na locus standi
 

Hili ni moja ya mapungufu ya katiba yetu, "mpiga kura ana haki ya kupinga matokea only kama haki yake ya kupiga kura ilivurugwa" mfano alikataliwa kupiga kura kwa sababu si za kisheria nk. Katiba hii mbovu inavuka mipaka na CCM waliweka mwanya huo na kuingiza nchi katika gharama za kipuuzi
Watu wengi tunapinga vitu kutokana na ushabiki, ni malezi tuliyopewa na CCM
 

1. Mimi nimeelewa kuwa katika kesi hii mgombea mwenyewe ndiye aliyepaswa kulalamika na si wapiga kura wake kama ilivyo pia kwamba kama wapiga kura wana kitu wanakilalamikia labda hawakutendewa haki ni jukumu lao kufungua kesi na si jukumu la mtu mwingine (third party), mfano mgombea kulalamika.
2. Tuchukulie mimi nimekutukana vibaya wewe. Halafu mtu mwingine aliyesikia yeye mwenyewe afungue kesi ya kunishitaki kuwa nimekutukana na aliyetukanwa wala haoni tatizo. Je, mahakama hapo ungetaka imsikilize nani: aliyetukanwa na yeye haoni tatizo lotote au aliyesikia na ambaye hakutukanwa?
3. Tukumbuke pia kuwa kesi hii si ya jinai na hivyo utaratibu wake wa kufungua na kuendesha mashtaka ni tofauti na ule wa kesi ya jinai.
 

Kama unaingiza neno "mkataba" si ujue third party hawana chao kwenye mkataba unless mkataba unasema hivyo?
 
...Watu wengi tunapinga vitu kutokana na ushabiki...

1. inabid ufikirie lema angekuwa wa ccm au cuf unge-comment unavyo comment sasa? maana leo ni wa cdm kesho inaweza kuwa wa ccm 2. tusio na vyama interest iko kwenye namna bora zaid ya kushughulika na chaguz na kesi zake baadae 3. hata kama majaj wa kuheshmika sana ndo wametoa huo uamuz na ujadiliwe tu. tunajua wao pia ni binadam kama sie na tunajuaje kama hawakuwa influenced na chochote?
 
Kama unaingiza neno "mkataba" si ujue third party hawana chao kwenye mkataba unless mkataba unasema hivyo?
kwenye social contract ni tofauti kidogo na ordinary contract mkuu kwani ni mkataba kati ya wananchi na mtawala hivyo hawa wapiga kura sio third part bali ni sehemu kabisa ya mkataba
 

Ulevi wa kisiasa ni kama huo hapo juu!
 

Mkuu, big up.
 
Ulevi wa kisiasa ni kama huo hapo juu!

Only in Tanzania, mwanasheria mmoja anaweza kumwambia mwanasheria mwengine asiangalie kesi kwa misingi ya taaluma ya sheria bali siasa.

Na only in Tanzania, jambo hilo litaonekana ni poa tu na msemaji ni "jembe" sana
 
Only in Tanzania, mwanasheria mmoja anaweza kumwambia mwanasheria mwengine asiangalie kesi kwa misingi ya taaluma ya sheria bali siasa.

hata mim hii imenishangaza zaid. sikutegemea jembe lisu angesema hvo alivosema. eti suala litazamwe ki-Tz zaid. utafikir tz 2ko so different from the rest na hii ni genetically. anazid kuniaminisha kuwa prof shivji yuko right. nimesoma mwananch la leo
 

Ebwana upo sahihi kabisa, katika uelewa wangu mpiga kura anaweza kufungua kwasababu flani au anapo jiskia siungi hoja ya shivji.
 
Mpiga kura hana Locus stand ya kuchalenge hapo, lakini pia mahakama imetoa sababu za hukumu kua hakuna athari zozote zilizompata mpiga kura katika madai ya msingi ya kesi waliyofungua. mahakama kuu imesimama kwenye haki haijayumba katika kutoa maamuzi katika shauri hili.
 
Unalinganisha udiwani na ubunge?

Nyani Ngabu, ubunge, udiwani na urais vyote vinahusika na upigaji kura. Haki ya mpiga kura inatofautiana kulingana na ama anapiga kura ya urais, ubunge au udiwani. Maana yangu ni kuwa haki ya mpiga kura inategemea na eneo analotoka. Mpigakura aliejiandikisha Chakechake anaweza kupiga kura kumchagua rais mahali popote nchini (Ngara, Kintinku, Ishinabulandi n.k) lakini hawezi kupiga kura kumchagua mbunge nje ya jimbo lake la uchaguzi na hawezi kupiga kura ya kumchagua diwani nje ya kata aliyojiandikisha.

By the same token; there must be a limitation on the right of the registered voter to appeal against the election results.
 
Kwanza inabidi ieleweke unaenda kupinga uchaguzi wa aina gani.

Na pili, kama una compelling evidence kwa nini usiweze?

Nyani Ngabu, hata kama mjuaji ana "compelling evidence" ya election violations Musoma Mjini, yeye akiwa mpigakura wa Kanyenye Tabora haki zake zinazohusiana na uchaguzi (iwe ya ubunge au udiwani) Musoma Mjini zitakuwa zimekiukwaje?
 
Nasikitika kumfananisha shivji na mchungaji(mwl Prof. wa sheria) wa kanisa anayeaminika kwa mafundisho,maombezi na ushauri(elimu ya sheria) kwa waumini(wananchi) wake na sasa amekengeuka(corrupt) na kuwafanya waumini wamkimbie(mimi kuacha kuhudhuria workshop zake popote pale) na kuanzisha harakati za kumpinga kwa kuacha misingi ya sheria na kuanza kufanya siasa.............the deady thought .....kweli kuzeeka kwingine mzigo....nawkilisha.
 
Sawa kabisa mkuu ni haki yako kufungua mashtaka lakini umbumbumbu wa sheria ndio uliowaangusha hao wakata rufaa CA vielelezo je????vithibitisho je????VILIVYOATHIRI mgombea wako asishinde utavionyesha pale mahakamani???????unavyoo????teh,teh,teh SHERIA ISIKIE TU.
 
hii mada mlkua mnajadili lakin toka mlipoanza tumia hii lugha ya kitumwa mmeharibu mambo...

Hata wewe umetumia maandishi ya watu, kama hutaki kujichanganya anzisha maandishi ya kwetu na wala usitumie teknolojia za watu tujue unamaanisha unachoandika.

Mtu unatumia alphabet ya Kirumi, internet ya Kimarekani, computer/simu nina hakika si ya Kitanzania etc etc halafu unabinua pua kuhusu "lugha ya kitumwa"?

Kiswahili chenyewe ni lugha iliyotumika katika biashara ya kitumwa kipande chetu, kuliko kiingereza, na kimejaa maneno ya kiarabu, kwa minajili hii hata wewe nawe hujafanya chochote zaidi ya huyo unayemuamini.

Hizo sheria zenyewe tumerithi za Muingereza, halafu kelele nyyingi lugha ya kitumwa wakati hata ukiandika kiswahili ni lugha iliyotohoa sana kwa watu, hatuna maandishi yetu na sheria zenyewe tumezirithi kwa msingi wa common law za Uingereza na mfumo mzima wa serikali umedesa kwenye Westminster system, kila unapoangalia tumedesa.

Wewe unalalmikia lugha?

Unazunguka harijojo ka guluguja aso uti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…