Prof. Shivji apinga sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema

Haki zipi anazo mpiga kura tupe mfano.
1. Haki ya kupiga kura
2. Haki ya kupigiwa kura
3. Haki ya kudai haki kama anaona haki yake inapokonywa
4. Kama Dr Batilda angefungua kesi/angelalamika labda tungekuwa tunakuwa tunajadili kitu kingine lakini (third party)! Hapa labda kama utangeleta sheria inayosema hivyo kwamba akionewa huyu mwenye haki ya kulalamika ani yule mwingine na si aliyeonewa.
 
Mkuu Ritz hebu waache kina EMT watushushie nondo za kisheria hapa bana. Mwenzio nakaribia kukamata LLB kwa nondo nazozisoma hapa.

Ubishani wa kisiasa tuufuate na tuufanyie kwenye mathread ya kina TUNTEMEKE na Masalia yao.

Mkuu Asprin,
Nipo nao hawa toka kule Great Thinkers. Nafyonza elimu tu hapa.
 
Last edited by a moderator:
Mpiga kura atakosaje kuwa na maslahi katika chaguzi za nchini mwake bana?

Nyani!

Nimeisoma mara 2 hukumu ya Mahakama ya rufaa kwenye "concurrence" iliyosainiwa na Jaji Nathalia Kimaro;hukumu hii haijatengua wala kufuta kutumika kwa kesi ya Chadiel Mgonja(1980)kwenye kesi za Uchaguzi hapo baadae!

Lkn Mahakama ya Rufaa imeona kuwa walalamikaji kwenye kesi ya Lema-Arusha WAMESHINDWA KUTHIBITISHA MAHAKAMANI ni vipi haki zao za msingi kama wapiga kura zilikiukwa!!

TUSICHANGANYE MAMBO:ktk Kesi ya LEMA wapiga kura hawa walikuwa wanalalamika kuwa Lema alimtukana Mama Batlida lkn wao wameshindwa kuthibitisha mahakamani matusi ya Lema kwa Mama Batlida ni kivipi yaliaathiri uchaguzi huo na ni vipi yaliwaathiri wao wenyewe kumchagua Mbunge wampendae?

Ni kweli ktk hukmu yao majaji wote 3 hamna aliyaendika "dissent"lkn hii haina maana kuwa kesi ya Mgonjwa haitatumika tena kwenye kesi za wapiga kura wakikimbilia mahakamani!

Kesi hii ya Lema haikuwa ya uchaguzi bali ni ya kashfa na hawa wapiga kura wametupotezea muda tu!Kesi ya Mgonja si iliamriwa kwenye ground ya baadhi ya wapiga kura halali kuzuiliwa kupiga kura?
 
Watu wa Chadema wametoka wapi? Si muijadili hiyo sheria tu bila kuweka siasa kama magwiji ya sheria hapa JF akina EMT walivyofanya?

Wengine kusoma na ku like inatosha!

umetazama mbali sana ndugu yangu
 
Last edited by a moderator:
Hawa wapiga kura pamoja na mambo mengine walilalamika kuwa Lema alitumia maneno machafu(matusi) kwa mgombea wao ndo maana akashindwa. Sasa mbona hakuna mahali ambapo Batilda alilalamika kwa tume kutukanwa achilia mbali kujakuthibitish hayo malalamiko mahakamani.

Pili waliofungua kesi ya arusha hakuna uthibitisho mahakamani kuwa ni wapiga kura wa Arusha mjini, ndo maana mahakama imepigilia nyundo kwa kila mpiga kura kufupinga ushindi wa mtu.

Kumbuka mahakama imesema uthibitisho wa kuwa wale walalamikaji wa tatu ni wapiga kura wa arusha mjini, wakili wao alitakiwa alete barua ya uthibitisho kutoa Tume ya Uchaguzi ikitamka hivyo. kwa tafsiri ya harakaharaka kesi ilifunguliwa na watu baki wasio wapiga kura wa arusha mjini
 

Mkuu ukiangalia kwa undani utaona tatizo lipo kwenye sheria yenyewe kwani sheria haionyeshi ni wapi ambapo mpiga kura haki yake ikikiukwa anahaki iko tu general tena inaonyesha mpiga kura yeyote bila kuzingatia hata kama alipiga kura au la au alijiandikishia wapi0 Maoni yangu hii sheria iangaliwe ili iboreshwe.
 
Nimeyakuza na kuyapaka rangi maneno yako hapo juu ili kuonyesha msisitizo.. infact hizo ndio sifa zako kwa sababu huoni hata hoja iliyopo nyumba ya wanaopinga hukumu hii.. umeshindwa kuona jinsi mahakama ilivyopinda sheria(bila kujali uzuri au ubaya wa sheria husika) na umeshindwa kuona hata mawakili na wanasheria waliobobea wanapotoa matamshi kwaba"""" HAPA MAHAKAMA IMETUNGA SHERIA MPYA""""

Huoni kwamba kazi ya kutunga sheria sio ya mahakama bali kazi yake ni kutafsiri sheria iliyotungwa na bunge....... unaendekeza mapenzi/chuki kuliko mantiki na umepofushwa na ushabiki kiasi cha kutoona ukweli ulio wazi... pambana kwa hoja neno kwa neno na sio kukimbilia kuzikashifu sheria zilizopo bila kutoa ushauri wa jinsi tutakavyoziondoa katika maoni ya katiba ijayo..
 

Mkuu vipi kesi ya Mgoja mwaka 1980?
 
Prof.Shivji na Stolla yawezekana hawajaisoma hukumu vyema. Kabla ya yote,Mahakama ilijiridhisha kama Warufaniwa walikuwa wapiga kura waliandikishwa kisheria.Hapakuwa na ushahidi kulingana na Sheria ya Ushahidi. Kadi za wapiga kura hazikuwasilishwa kama ushahidi.Hivyo,hawakuwa wapiga kura waliosajiliwa(registered voters).Hapo ndipo Lema alipoibukia kidedea.
 
Kwa makusudi kabisa sitajadili maudhui ya hukumu ya Lema ingawa nimepitia nakala yake.Niseme wazi kuwa nina wasiwasi na nia ya gazeti la Mwananchi kuendelea kufuatilia uhalali ama ubatili wa hukumu ya Lema kisheria.

Nia yao ya wazi ni kuuza gazeti ili kupata faida kwa stori zinazoonekana zina mvuto kwa wananchi. Mtindo wa wanahabari kutafuta wanataaluma kupata maoni yao kuhalalisha matamanio na mitazamo yao haufurahishi na hauvumiliki. Habari husika ina upungufu kwa kuwa imekiuka moja ya miiko ya taaluma habari kwa kutoweka maoni ya wanasheria wengine wanaoridhishwa na hukumu husika mbali na wakili wetu Kimogoro.

Swali:Baada ya Lema kuvuliwa ubunge wake, April,''Mwananchi'' walitafuta maoni ya Shivji na wengine?Baada ya ile hukumu ya Mnyika, walitaka maoni ya wabobezi wa sheria? Na ile ya Igunga je? Vipi kuhusu ile ya Sumbawanga?

Labda niwaulize ''Mwananchi'':ule mwendelezo wa habari na makala za ''kikombe cha babu wa Loliondo'' umefikia wap?Tusingependa kuletewa tamthilia tena maana kwa hakika yapo masuala mengine ya msingi kujadili.

 
sijasoma sheria hata moja ila hapo ndipo kwenye hoja ya msingi kabisa.
 
Reactions: EMT

Well said Mkuu, lazima tujiuliza maswali hayo kama mgombea mwenyewe angefungua hii kesi hapo ingekuwa applied kuwa haki zake zimeadhiriwa kwani alidhalilishwa lakini akaja mjomba wake akadai kuwa haki zangu zimeadhiriwa kwakuwa ni tegemeo lake hapana hapo pana ukakasi wanasheria watu wanapaswa kusugua vichwa tena.
 
Mimi siyo Great Thinker kama Gaijin, EMT, au Bu'yaka :becky: lakini hiki anachosema Shivji hata kule kwenye jukwaa la hawa ma Great Thinkers nilikisema.

Mpiga kura atakosaje kuwa na maslahi katika chaguzi za nchini mwake bana?


naoma kujuzwa kilichosemwa kwenye kesi ni kuwa mpiga kura hana maslai katika uchaguzi wa nchi yake au yale matusi ndio hayakuwaathiri wapiga kura na hivyo kukosa haki kisheria ya kufungua kesi. na haswa ikizingatiwa kuwa walishinda kupeleka ushahidi wa matusi hayo kama yalkikuwepo au la?
 

Kimogoro amesema sheria hampi haki mwanchi kumshitaki mtoa rushwa kwenye uchaguzi akaulizwa na mwananchi vipi mpiga kura anaweza kumshitaki akasema ngoja ariew sheria ha ha pana tatizo kwenyesheria yenyewe.
 

Shivji amechemka sana kwenye hili hukumu ya CAT hainyimi wapiga kura haki ya kushtaki au kupinga matokeo ila imeweka vigezo lazima mpiga kura awe ameadhirika na athibitishe ameadhirika vipi kabla hajafungua kesi,kwa hiyo haki ya kupinga ipo ila sio kil mtu bila sababu THERE IS NO ROOM FOR BUSY BODIES IN COURT OF LAW
 
Walichokifanya mahakama ya rufaa ni kuidhibitisha kauli ya kisheria "NO ROOM FOR BUSY BODIES" mpiga kura hajanyimwa haki ya kupinga matokeo ila awe ameadhirika moja kwa moja na aweze kuthibitisha hilo
 
Ningemuona Shivji wa maana kama angeanzisha mjadala kwanza kwa hukumu ya jaji Rwakibarila,
ya kutoa hukumu wrong ya kumzuia Lema kushiriki siasa,je ilikuwa sahihi?kwa nini hakuanza na
hili kwanza,Jibu ni:MNAFIKI"
 

UMEMALIZA KILA KITU.SHIVJI Anazeeka vibaya baada ya kutoswa na JK ujumbe wa katiba mpya.
 
tunawasubiri wanasheria mliobobea sheria niliyosoma ni kidogo sana nika ilikuwa yakunilinda kwenye mikataba tu na ufanyaji wa kazi sehemu mbalimbali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…