Prof. Shivji apinga sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema


Nakuongeza na LIKE tena" Nimekasirika sana leo kununua gazeti hili la kipuuzi na kukuta kilichoandikwa humo,lengo la Mwananchi ni mwendelezo wa habari zao za kujipeleka kaburini bila kujua,kwa kuwaza wanaweza kucheza na akili za watanzania kwa habari zinazouza gazeti lakini hazina mashiko yoyote,

Ni kwa nini hawakumhoji Shivji juu ya hukumu ya jaji Rwakibarila? na huyu Mzee kwa sababu amekuwa mnafiki sawa na lengo la aliyemhoji akajiingiza kwenye mkenge,Hivi suala la mtu kuitwa nyumba ndogo kuliathiri vipi haki ya mpiga kura na kumnyima ushindi mgombea wake,hata kama sijui sheria hapa Mzee Shivji amechemka.
 

Msomi Wangu Gaijin,

CA ililiona hilo na ndiyo maana ikatoa ufafanuzi huu:

" So a voter has no right to petition and challenge the election results where his rights were not infringed. Section 111(1) (a) of the Act reads:- 111(1) An election petition may be presented by one or more of the following persons, namely-: (a) a person who lawfully voted or had a right to vote at the election to which the election petition relates.

Currently the rule in Tanzania has been extended to cater for matters of public interest under Article 26(2) of the Constitution then a citizen of this country has locus standi to sue for the benefit of the society. And the test whether a litigation is of public interest depends on the nature of the relief sought and its effect. In Rev. Christopher Mtikila V Attorney General [1995J TLR 31 Lugakingira, J (as he was then) observed what a public interest litigation is.

He said:-
II In matters of public interest litigation this court will not deny standing to a genuine and bona fide litigant even where he has no personal interest in the matter." He went on the say :- II It is not the type of litigation which meant to satisfy the curiosity of the people, but it is a litigation which is instituted with a desire that the court would be able to give effective relief to the whole or a section of the society" In common law in order for one to succeed in an action, he must not only establish that his rights or interests were interfered with but must also show the injury he had suffered above the rest.

In The Attorney General v The Malawi Congress Party and
another, Civil Appeal No. 22 of 1996, the Malawian Supreme Court of Appeal provided the test for locus standi. It said:- II Locus Standi is a jurisdictional issue. It is a rule of equity that a person cannot maintain a suit or action unless he has an interest in the subject of lt; that is to say unless he stands in a sufficient close relation to it so as to give a right which requires prosecution or infringement of which he brings the action"

In our case the issue for consideration and decision is whether or not a registered voter under section 111(1)(a) of the Act has an absolute right to challenge the election result even where his rights were not infringed. We have given a deep thought to the matter. First, we wish to point out that election petitions are not in our view public interest litigation though they are matters of great public importance.

This is because the relief sought would not benefit the entire society as a whole. Second the petition was not brought under Article 26(2) of the Constitution which permits any person to bring a public interest litigation. The Article provides:-
26(2) Every person is entitled, subject to the procedure provided for by the law, to institute proceedings for the protection of the constitution and legality. Since an election petition is not a public interest litigation we do not read the section to have done away with the rule of locus standi.

We think in our view, section 111(1)(a) of the Act give rights to registered voter whose rights to vote have been interfered with or violated. In case violation effects the candidate it is for the candidate to challenge the election because his rights were violated. To give the section a broader interpretation that he has an absolute right to petition even where his rights were not interfered with is to defeat the well established principle of law of locus standi and indeed it does not sound well. We are not prepared to do so."
 
Nimesoma maelezo ya Prof. Shivdi kisha nikalinganisha hiyo sheria na hukumu ya Lema, bila kumumunya maneno Prof.Shivdi katika hili AMEPOTOKA KABISA.
Kwa sababu vifuatazo;

(1)Mpiga kura na mgombea hawana haki sawa kisheria katika uchaguzi. Haki za mgombea ni kubwa zaidi ya haki za mpiga kura
(eg.Sio kila mpiga kura ana haki ya kuwa mgombea lakini wagombea wote wana haki zote za mpiga kura)

(2)Haki ya mpiga kura ni kujiandikisha na kupiga kura tu, wakati mgombea ana haki zote za mpiga kura(Kujiandikisha na kupiga kura) Plus haki ya kupiga kampeni, kusimamia zoezi la upigaji kura, kuhesabu kura na kutangazwa matokeo nk.

(3)Hakuna haki yoyote ya mpiga kura(Kujiandikisha na kupiga kura) iliyoelezwa kuvunjwa katika uchaguzi ule katika kesi hii na wafungua kesi.

(4)Wafungua kesi walikosea sana walipoamua kubeba jukumu la mgombea(Kudai kudhalilishwa kwa mgombea wa CCM wakati wa *KAMPENI) wakati wao ni wapiga kura, hivyo wanakosa nguvu ya kisheria kudai na kuhoji haki isiyowahusu.

*KAMPENI ni jukumu na haki ya mgombea na chama chake tu na sio jukumu au haki ya msingi ya mpiga kura kisheria.
 
Mimi siyo Great Thinker kama Gaijin, EMT, au Bu'yaka :becky: lakini hiki anachosema Shivji hata kule kwenye jukwaa la hawa ma Great Thinkers nilikisema.Mpiga kura atakosaje kuwa na maslahi katika chaguzi za nchini mwake bana?
Nyani Ngabu et al. mimi sio mwanasheria, lakini nikiwa kama layman sitopenda mtu aende mahakamani kufungua shauri la kutengua matokeo ya uchaguzi ikiwa haki yake kama mpiga kura haikufinywa.

La sivyo na mpiga kura mwingine anaweza akaenda Mahakamani kupinga mpinga matokeo kutaka kufinya haki yake, na yeye akiwa kama mpiga kura.

Tukiruhusu kitu kama hicho, itakuwa gharama sana kwa serikali yetu, na zaidi; tunaingilia haki za wapiga kura wengine wengi ambao wanaona haki zao kama wapiga kura walizipata ipasavyo, na hivyo kutoamua kufungua kesi mahakamani.
 
Nadhani hao tunaowajua kuwa ni wanasheria waliobobea ndipo hapa hawapaangalii vizuri. Naomba waangalie maelezo yako kwa sawa sawa. Suala la kutumia maneno ya Kashifa haiwezi kuhathiri haki ya mpiga kura, bali inaweza kumuathiri mgombea na ndiye alitakiwa kulalamikiwa.

Kashifa anaweza kuielewa mkashifiwa maana ndiye anayejua ukweli wake yeye mwenyewe. Kwa mtu mwingine hawezi kujua kuwa mtu kakashifiwa maana huenda yaliyotamkwa ni ukweli na kwa hii naweza kusema kuwa huenda yanayotafsiriwa kuwa kashifa siyo kashifa ndiyo maana mgombea mwenyewe hakulalamika.

Majaji wa mahakama ya Rufaa walitumia hekima ya hali ya juu. Sikatai kuwa wanasheria wetu wanaotoa hoja za kukosoa hukumu siyo wasomi, la niwasomi haswa ila wanakosa component moja katika ubobeaji wao. Wanafalsafa kuna kitu wanaita Pragmatism katika elimu, kwa maana kuwa elimu anayoipata mtu imwezeshe kuendana na hali inayobadirika badirika na siyo kwa kuwa hukumu ilitolewa na itaendelea kuwa hivyo hivyo.

In pragmatic Philosophy they say that there is no absolute truth. Hebu tuwe tayari kubadilika kulingana na mabadiliko. Heri ya Mwaka Mpya
 
"Lakini Profesa Shivji aliitetea hukumu hiyo ya Mgonja akisema imekuwapo kwa zaidi ya miaka 30 sasa na kwamba kwa muda wote huo imekuwa ikifuatwa katika uamuzi wa mashauri mbalimbali, huku akisisitiza kuwa Mahakama haiwezi kuifuta kirahisi tu."

Mimi siyo mwanasheria, lakini kwa tafsiri rahisi tu, sidhani kama hii ni sahihi kama anavyosema Prof. Shivji!
 
Ni jambo zuri kulijadili ili hatimae tuwe na uelewa na kujua vitu ambavyo mwisho wa siku si kwa maslahi ya jamii fulani tuu bali taifa zima.

Hoja ya Shivji na wanasheria wengine ni ya msingi kama mahakama imeondoa au kuzuia haki ya mpiga kula kufungua kesi za uchaguzi.

Hoja nyingine ninavyoiona ni kama mpiga kura ana haki hiyo basi ni kwa wakati au mazingira gani au ni haki hisiyo na mipaka.

Nionavyo tutafika mahali tutakuwa na jibu juu ya suala hili ila Tuwe makini Shivji hapingi Lema kushinda ila ana concern na haki ya mpiga kula.
 
Reactions: EMT
Hivi hapa tatizo ni gazeti au ni Shivji?

Maamuzi ya kesi ya Lema yalikuwa na sura kuu mbili tu,

1) Waliathirika vipi na kile kilichodaiwa ni matusi? (Na hapa alistahili kusimama mtukanwaji sio vinginevyo)

2) Matusi hayo yaliathiri vipi mwenendo MZIMA wa uchaguzi?

Ninawasiwasi gazeti limepotosha maelezo ya Prof Issa Shivji makusudi.
 
Safi kamanda wanaopinga hukumu hii inawezekana hawajaisoma kwa makini, CA ilichokifuta ni kwa mpiga kura kuwa absolute rights of litigation in election matters. Lakini wanavyochangia ni as if CA imefuta kabisa haki ya mpiga kura kufungua kesi ya uchaguzi hata pale ambapo haki zake kama mpiga kura zimevunjwa
 
Reactions: EMT
Nakuunga mkono asilimia 100 kamanda.
 
Ndiyo hawahawa watatuabia tukubaliane na ushoga na kuutetea kisheria sababu tu UK wanafanya hivyo kutokkaka na sheria zao tunazozifuata pia katika maamuzi yetu.
 

Thanks GT, kwa maoni yangu msingi hasa wa uamuzi wa majaji wa mahakama ya rufaa kwa maoni yangu ulijikita kwenye hoja kuwa wajibu rufani hawakuthibitisha kuwa walikuwa wapiga kura halali kwa kujumuisha vielelezo.
 
EMT,

..lakini malalamiko dhidi ya Mgonja yalihusisha masuala ya rushwa.

..wakati hii ya Lema inahusisha matamshi aliyoyatoa wakati wa kampeni ambayo wapiga kura watatu wanaamini ni kashfa na wameathirika.

Wameathirika vipi mkuu????
Kumbuka hata anayedaiwa kutukanuwa hakuathirika na hakutaka hata kuwa shahidi kwenye hiyo kesi.


 

Hoja zilizorudisha Ubunge wa Lema ni hizi hapa
Hizi ndio hoja za Kisheria zilizorudisha Ubunge wa Lema - YouTube
 

Hata kama Shivji yuko sahihi kuhusu haki ya mpiga kura, bado kesi husika ilikuwa ya kutunga na hawakuweza kuthibitisha madai yao! Pure CCM political games! Ni kupoteza wakati kujadili case zinazotungwa LUMUMBA!
 
Hivi mpiga kura aliyejiandikisha kata ya segerea jimbo la ukonga, anayo haki ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge jimbo la Kibakwe, kwa kuwa alipita Mtera akakuta Simbachawene akimkashifu mpinzani wake katika kampeni? Kama ndivyo sheria zinavyotaka, itakuwa vurugu tupu.
 
Reactions: EMT
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…