Prof. Shivji apinga sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema


yap inawezekana kabisa. nakupa mfano mwingine kama ulivyosema unatoka jimbo la segerea ukafika kibakwe ukashuhudia live mgombea wa huko anatoa rushwa waziwazi, utanyamaza kisa si mgombea wa jimbo lako?. Kwa kifupi wanyonge hatuna haki tena. bora hata SHIVJI na wenzake wameliona hili na wajanja sasa hatupigi kura ng'o kwa sababu hata kama ukidhulumiwa huna pa kulalamika.
 

:becky: kweli mkuu babu kachemka
 
Hata kama Shivji yuko sahihi kuhusu haki ya mpiga kura, bado kesi husika ilikuwa ya kutunga na hawakuweza kuthibitisha madai yao! Pure CCM political games! Ni kupoteza wakati kujadili case zinazotungwa LUMUMBA!

Hayo sasa ni maneo ya ma-layman kama wewe, huna sababu ya kutuondoa katika msindi wa mada iliyoko hewani. Haijalishi kesi imetungwa LUMuMBA au hukumu imeandaliwa MTAA WA UFIPA KINDONI, hoja ya msingi ni Mpiga kura hana haki ya kupinga matokeo ya uchaguzi? na siyo kutuletea maneno ya vichwa visvyo na shule kama wewe.
 
Shivji kachemka kweli, coz haki ya kufungua kesi ya kupinga ushindi wa mbunge aliechaguliwa na umma na mtu ambaye haki zake si za mojakwa moja ingekuwa ni kuvunja haki za umma wa waliowengi. Ni mwathirika moja kwa moja ndie mwenye haki ya kufungua kesi
 

Yaani hapo wewe hujaelewa nini? ni wazi kuwa hukumu imemnyima haki mpiga kura. Hilo lingezingatiwa kwanza ni wazi matusi yale yalikuwa na effect kubwa tu katika mwenendo mzima wa uchaguzi na ndiyo maana tume ya uchaguzi katika sheria zake jambo mojawapo inalolisisitiza ni kufanya kampeni za kistaarabu kwa sababu wanajua madhara ya kampeni zisizo za kistaarabu.
 
 

EMT.
Mimi sio mtaalamu wa sheria lakini kwa jinsi nilivyofuatilia wataalamu wengi wa sheria wanachopinga ile statement ya "mpiga kura hana haki ya kufungua kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi"

Hata mimi naona ulakini katika hapo, mahakama ilipotumia statement kuamua rufanu ile imekuwa kama wametunga sheria mpya.
 
Reactions: EMT
Uliianza vizuri
nikasema leo Kiranga kapewa za mbavu

Sisi tuliobahatika kupata exposure kwa wenzetu ambako demokrasia imekomaa,
Hee kumbe upo exposed...

Mbona unawaibisha wenzako wakomavu wakisiasa na uchambuzi kama huu...
 

Hukumu ya Mgonja inaonekana kuwa ndio basis ya argument ya Prof Shivji. Je, hukumu hiyo ilikuwa sahihi? Na kama hakikuwa sahihi (kama walivyosema majaji kwenye kesi ya Lema) iendelee kutumika kwa sababu tu imekuwepo kwa miaka mingi sasa?

Pili, bado sijaelewa ni kwa vipi 'matusi' ya Lema yamewathiri wapiga kura/waleta mashitaka? Na maadam kesi hii inahusu uchaguzi wa mbunge wa Arusha Mjini, je, matokeo ya uchaguzi yangekuwa tofauti kama Lema hakusema hayo matusi?
 
Kama ni hivyo kwanini sheria itamke mpiga kura na si mwananchi yeyote? Je, mpiga kura ni yule tu aliyejindikisha kupiga kura? Kama raia amejiandikisha kupiga kura halafu hakupiga kura, kwa sababu nyingine zaidi ya safari za kikazi, ugonjwa au kuzuiliwa na taratibu za upigaji kura anakuwa na sifa za mpiga kura (mfano sikutaka tu kupiga kura)? Kwanini sheria ininyime haki ya kupiga kura popote na wakati huohuo inipe haki ya kupinga matokeo ya uchaguzi popote?
 

Wafungua kesi walishindwa kuthibitisha waliathirika vipi na madai ya matusi, pia mtukanwa hakuthibitisha kama alitukanwa kweli na hayo matusi yalimuathiri vipi katika uchaguzi! Hizi argument ndo zilipelekea mahakama ya rufaa kutoa uamuzi iliyotoa!
 
Mambo yameanza!!! but hata wakate tena rufaa but Lema is a winner!!! Kweli anaogopwa sana huyu mheshimiwa!! Hamtaki wanaarusha wawe na mwakilishi?
 

...kweli mkuu,maswali yako ni yamsingi sana...
 
hii inaonyesha ni jinsi gani hili linchi lina hali ngumu....semen msemavyo...cha msingi mweshimiwa lema yupo jimboni!!!
 
Japo mimi sio gwiji katika sheria kama Prof Shifji nadhani hayuko sahihi. Sheria inayoweza kutumiwa vibaya imepata tafsiri nzuri ili kukomesha matumizi yake vibaya. Sikubaliani kama mahakama ya rufani imetunga sheria mpya, ila imetafsiri sheria iliopo kwa namna chanya kuelekea kupata haki.
 
Hii thread ni muhimu sana kwa kujifunza.

Sisi ambao hatujui sheria nashauri tukae pembeni na kuwaacha wenye ujuzi watuelemishe.

Hili suala halina siasa ndani yake wala halina uhusiano na Lema kurudishiwa ubunge au kutokurudishiwa. Hii ni tafsiri kubwa zaidi ya siasa za CCM na CHADEMA.

Tusiivuruge kwa mapenzi ya vyama vya siasa na badala yake tuwaachie wanaojua kuliko sisi watuelemishe.
 
hii nchi hii inashangaza hii nani alisema hii nchi ina sheria,toka mwanzo kesi ilianza kinafiki na bahati nzuri imeisha kinafiki shame tanzania unaangamia kwa upumbavu wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…