Prof. Shivji apinga sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema

Prof. Shivji apinga sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema

Wanasheria tufahamisheni ni haki zipi ambazo anazo mpiga kura kwenye uchaguzi.
 
Binafsi nnaona mpiga kura haki anayo, ila kwa kesi ya lema, ni hoja gani mpiga kura anakuja nazo?
hapo ndo penye tatizo, mpiga kira anatakiwa aje na hoja zinazomgusa moja kwa moja.
 
Shivja anaijadili sheria ilivyo lakini hakuangalia sheria hiyo katika uchaguzi huo wanaopinga matokea waliathiriwaje na madai yao kitu ambacho mahakama imeegemea kutoa hukumu yake. Hao wapiga kura hawakutukanwa na Lema sasa wanasimamaje kudai haki mahakamani wakati aliyetukanwa hakulalamika wala kuwa mmoja wapo wa mashahidi. Pamoja na ugwiji wa sheria katika hali kachemka sana.

Nilitaka kuandika wazo hili, kwa kuwa umeshaandika basi napigia mstari. Hebu tu read btn the lines jamani, tusikurupuke na kipengele kimoja, hasa kwa wanasheria
 
Shivji yuko sahihi kwamba mpiga kura ana haki, lkn haki hiyo ataitumia pale ambapo anaona kuna jinsi flani hajatendewa haki.
Sasa hao wapiga kura ndio waliotukanwa? Locus stand yao ktk kesi hii iko wapi?
Sio kwa sababu ni mpiga kura basi ufungue kesi ktk mambo yasiyokugusa, that is not the law
 
Badala ya kuhangaika na Lema,Prof Shivji angezungumzia hukumu ya Mgombea binafsi iliyoamuliwa na mahakama ya Rufaa.
 
Mkuu msome vizuri Prof Shivji yeye anaelezea tafsiri za sheria wewe umejikita zaidi kwenye ushabiki wa kisiasa.

Ritz inaingia akilini mwako mfano nitukanwe na Honey K halafu wewe Ritz uende kumshtaki mahakamani? Mbaya zaidi hata kunishirikisha mtukanwa kama shahidi isifanyeke, kwanini nirukwe hivyo mtukwanwa mwenye haki na hata kama `sijaonyesha dhamira ya kufungua mashtaka dhidi ya mtusi?

Mambo haya tuweke kwanza ushabiki wa kiitikadi kando tujadili kisheria na hata kama taaluma ya kisheria imetupiga chenga, lakini ile kitu inaitwa common sense tu Shvji ameteleza kidogo.

Hoja ya kujenga utetezi tokana na kesi ya Mgonja ni dhaifu katika maana kwamba upembuzi wa sheria na tafsiri hubadilika tokana nawakati, ndio maana kuna mabadiliko ya sheria mara kwa mara licha ya kuongeza mpya kwani wakati ukuta, vinginevyo tusingekuwa na baraza la kudumu la kutunga sheria, maana serikali haijakamilika bila uwepo wa bunge ambao ni mmoja ya mhimili muhimu wa serikali, mhimili ambayo ndio chimbuko la kutathmini mabadiliko ya miundo ya sheria nchini.

Matumaini yangu makubwa umenielewa ingawa unaweza kuja na jibu ambalo kwa sababu zako unaweza ukalitoa kinyume cha uelewa wako, lol.

Enjoyo Holiday Ritz!
 
Kwa wale wanaofikiri kwamba huenda wale wanaCCM watatu watakata rufaa tena (kutaka jopo kubwa zaidi la Majaji rufaa) kupitia hukumu hiyo wasiwe na hofu kwani rufaa haitafanikiwa.

Hoja hiyo ya 'locus standi' ya warufaa -- yaani iwapo wana haki ya kufungua kesi kupinga matokeo ya uchaguzi halikuwa pekee ambalo mawakili wa lema waliliweka katika rufaa yao.

Hoja za kutokuwepo CD za uthibitisho wa matusi ya Lema kwa BB, au jaji wa Mahakama Kuu kukataa ushahidi wa wanachadema kwa sababu ulikuwa wa kishabiki lakini hapo hapo kukubali ule ushahidi wa wanaCCM kwa mfano hayakuguswa kabisa katika ruling ya jaji Kimaro na wenzake na hilo na mengine yanaweza kuibuliwa.

Kumbukeni Rufaa ambayo Azim dewji alimfungulia Dr kabaorou mwaka 1994/95 (yaani baada ya Kaborou kushinda kesi aliyomfungulia Premji katika Mahakama Kuu kupinga ushindi wake katika byelection ya Kigoma Mjini) Jaji Lugakingira (nadhani) aliibua suala la uraia wa Azim Premji kwani aliona suala hilo halikufafanuliwa vizuri (au tuseme lilikuwa wrongly decided upon) katika rufaa ya awali ya Dr Kaborou kupinga matokeo ya ubunge uliompa ubunge Premji.

 
Shivji ni binadamu kama wengine tukubali kuna sehemu anakosea, sawa mpiga kura anahaki ya kufungua kesi coz anamasilahi kwenye uchaguzi lkn suala hapa ni mwenendo wa uchaguzi uliadhiri vp haki ya mpiga kura!
 
Prof. Shivji si avae joho tu,
kwa nini kuongelea pembeni.
 
Kwa wale wanaofikiri kwamba huenda wale wanaCCM watatu watakata rufaa tena (kutaka jopo kubwa zaidi la Majaji rufaa) kupitia hukumu hiyo wasiwe na hofu kwani rufaa haitafanikiwa.

Hoja hiyo ya 'locus standi' ya warufaa -- yaani iwapo wana haki ya kufungua kesi kupinga matokeo ya uchaguzi halikuwa pekee ambalo mawakili wa lema waliliweka katika rufaa yao.

Hoja za kutokuwepo CD za uthibitisho wa matusi ya Lema kwa BB, au jaji wa Mahakama Kuu kukataa ushahidi wa wanachadema kwa sababu ulikuwa wa kishabiki lakini hapo hapo kukubali ule ushahidi wa wanaCCM kwa mfano hayakuguswa kabisa katika ruling ya jaji Kimaro na wenzake na hilo na mengine yanaweza kuibuliwa.

Kumbukeni Rufaa ambayo Azim dewji alimfungulia Dr kabaorou mwaka 1994/95 (yaani baada ya Kaborou kushinda kesi aliyomfungulia Premji katika Mahakama Kuu kupinga ushindi wake katika byelection ya Kigoma Mjini) Jaji Lugakingira (nadhani) aliibua suala la uraia wa Azim Premji kwani aliona suala hilo halikufafanuliwa vizuri (au tuseme lilikuwa wrongly decided upon) katika rufaa ya awali ya Dr Kaborou kupinga matokeo ya ubunge uliompa ubunge Premji.


Asante kwa kumbukumbu yako. Akina Mkanga hawatathubutu kukata rufaa tena kuna masuala mengine hayakuguswa na yanaweza kuibuliwa kama unavyosema.
 
Mkuu Ritz hebu waache kina EMT watushushie nondo za kisheria hapa bana. Mwenzio nakaribia kukamata LLB kwa nondo nazozisoma hapa.

Ubishani wa kisiasa tuufuate na tuufanyie kwenye mathread ya kina TUNTEMEKE na Masalia yao.
 
Last edited by a moderator:
I beg to differ. Parliament should always make law and the courts should interpret the law.

We should respect and observe the fundamental constitutional principles to avoid abuse.

Lord Denning was perhaps the greatest law-making judge of the last century and the most controversial.

His achievement was to shape the common law according to his own highly individual vision of society.

He stepped down from the House of Lords to a much more influential post - Master of the Rolls so that he could do his thing without interference.

During his 20 years as Master of the Rolls, he could choose his own cases and the judges who were to sit with him. So on most issues, he effectively had the last word.

But in seeking justice Lord Denning, considered himself entitled to get round - or even change - any rule of law that stood in his way. There was no need to wait for legislation.

"Parliament does it too late," he argued. "It may take years and years before a statute can be passed to amend a bad law.

"The judge ... should make the law correspond with the justice that the case requires."

Although he saw himself as champion of the underdog - the ordinary citizens, the consumers, the deserted wives - he supported employers against trade unions, education authorities against students, and the Home Office against immigrants.

But his 1982 book "What Next in the Law" was his downfall. In it, he seemed to suggest some black people were unsuitable to serve on juries.

Lord Denning's prejudices demonstrate the risks of letting one man dispense justice.

BBC News | UK | Denning: A life of law

Aren't some black people unsuitable to serve on juries?
 
1. Mahakama inaweza kutunga sheria kutokana na hukumu zake. Wakina shivji wakasome hukumu za judge Demining wa uingereza jinsi hukumu zake zilivhotengeneza sheria nyingi za jumuia ya madola. Kama kulikuwapo na hukumu ya 1980 inamaana haiwezi kutenguliwa tena?
2. Mahakama haikusema wapiga kura hawana haki ila hicho walichofungulia kesi ndio kina ulakini. Kumbuka wale wanaharakati waliofungua kesi ya kugomea malipo ya dowans mahakama ilisema wazi kuwa hawana haki kwa vile sio party to the contract. Lakini hao wanaharakati na watanzania wote ni walipa kodi na tuna haki wao hawakuliona hilo? Mahakama zimeweka utaratibu kuwa lazima uwe muadhirika au ufungue kesi kwa niaba ya mwadhirika kwa ridhaa yake. Au mtu ukiona jirani amewekewa X unaweza kwenda mahakamani kupinga kwa vile utapoteza jirani? Mwadhirika wa kesi hakwenda mahakamani na kesi ya kutukana kama ni kweli wangepaswa wapeleke polisi ili jamhuri imfungulie shitaka la jinai. Kama mwanachi anaweza kufungua mashitaka ya jinai basi hata wanachi wafungue kesi za watuhumiwa wa epa si wote ni waadhirika na tuna haki na kodi zetu?

Umenena vema kiongozi. Ni jambo ambalo haliwezekani kila mtu afungue kesi kisa ni mpiga kura. Ingekua kwamba Lema amechukua kadi yake ikasababisha asipige kura, au angetishwa kwa namna yoyote, hapo ana haki ya kufungua kesi na angeshinda. Lakini matusi ni personal attack, hayo hayo tunayoyaona matusi kwa wenzetu wa tamaduni zingine ni majina ya heshima sana-nenda Japan utakubaliana na mimi.
 
Shivji kaamua kuchafua hewa kwa makusudi kabisa na hii ni dhambi ambayo itamrudia tu.
Hii ni 2012 awareness ya binadamu inazidi kuongezeka kila sekunde inayopita.
Tutarajie kuna madudu mengi kutoka kwa watu wenye majina kama Shivji.

Shivji got point (social reason),but ni complete mbulula wa legal reason..na sio logic kusema eti hukumu ina makosa, sheria ni loop holes na logic ziko wazi kutumika to win..

Labda tukumbuke kesi ya lema haikufunguliwa chini ya ibara ya 26(2) ambayo inampa fursa raia yoyote kufungua shauri mahakaman yenye maslahi ya umma..na ipo wazi iyo kesi hata haina maslahi kwa umma wa watanzania.. Shivji naona angeingilia ile kesi ya dowans ambayo ilikua na maslahi 100% kwa umma..

Ila pia sijaona kwenye gazeti hawakuonesha what shivji think and why hiyo hukumu imetolewa hivyo anahisi kua jopo la majaji halikufikiria hicho anachosema but sio kweli they got iyo idea tht why walisema ile kesi ya mgonja was wrongly judged!
 
Kuna jimbo moja lilipingwa hapo dar es salaam kisa ni masanduku yalipotea.Pingamizi likatupiliwa mbali.Je ni hukumu gani ambayo haikuwa halali kati ya hii Lema na hiyo?
 
Mkuu Ritz hebu waache kina EMT watushushie nondo za kisheria hapa bana. Mwenzio nakaribia kukamata LLB kwa nondo nazozisoma hapa.

Ubishani wa kisiasa tuufuate na tuufanyie kwenye mathread ya kina TUNTEMEKE na Masalia yao.

Umenena mkuu.!
 
Last edited by a moderator:
#jaman WATANZANIA tuache kuishi kwa mazoéa,shvji ni shvji tu lakn ni BINADAMU kama walivo majjaji wale RUFANI!!!sio akisema fulan basi na ww hapo hapo NO!!
kumbuken JAJI anauwezo wa kufanya nn akiwa mahakaman,kwa namna gani na kwa maslahi gan!!!
kwa mtazamo wangu,HUKUMU haina kasoro maana ushaidi hautoshelezi toka mwanzo kule ARUSHA!!!
 
(Kutoka gazeti la mwananchi)
MWANAZUONI aliyebobea katika sheria, Profesa Issa Shivji na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Francis Stolla wamekosoa hukumu ya Mahakama ya Rufani, iliyomrejesha bungeni, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema.



Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi, wanasheria hao walisema hukumu hiyo iliyotolewa na majaji watatu wakiongozwa na Nathalia Kimaro, Salum Massati na Bernard Luanda, inapingana na sheria.


Hata hivyo, mmoja wa mawakili wa Lema, Method Kimomogoro amepinga madai hayo akisema wanaoipinga pengine hawajapata nafasi ya kuliangalia kwa undani suala la haki ya mpiga kura kupinga matokeo mahakamani.


Profesa Shivji kwa upande wake alieleza kushangazwa na maelezo ya Mahakama ya Rufani kuwa mpiga kura hana haki ya kufungua kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi na kusema hiyo ni sawa na kutunga sheria mpya na si kutafsiri zilizopo.
Alisema Sheria ya Bunge ya Uchaguzi, Katiba ya nchi na Mahakama, vinampa haki mpiga kura kufungua kesi kupinga matokeo ya uchaguzi.....

1. Wanasheria kutofautiana ni kitu cha kawaida sana katika sheria (ni kama wanavyotofautiana wanafalsa na wanateolojia).

2. Ndio maana mtu anaweza kushinda kesi mahakama ya mwanzo mrufani akaja kushinda kwenye mahakama ya hakimu mkazi au ya wilaya na pengine kushindwa tena akienda mahakama kuu na kuendelea kushindwa akienda mahakama ya rufaa au kushinda.

3. Sheria zinatafsiriwa na ndio maana wanaotafsiri wanatofautiana pia. Ukisoma hukumu ya Jaji Mwalusanya kupinga hukumu ya kifo (Mahakama Kuu) na kuibadilisha kuwa kifungo cha maisha (sababu alizozitoa ni za msingi) na ukisoma pia jinsi Mahakama ya Rufaa ilivyopitia hukumu yake na kuichambua na kukubaliana naye kuwa hukumu ya kifo inapingana na haki za binadamu, ni ya kikatiri na haki ya kuishi lakini mahakama hiyohiyo iliyotambua hivyo ilisema kuendelea kuwa na hukumu hii si kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na bado ndivyo ilivyo hadi leo mpaka hapo tutakapoibadili kwenye Katiba Mpya (kama tutafanya hivyo).
 
Back
Top Bottom