Prof. Shivji: Wamasai wasiondolewe Ngorongoro

Prof. Shivji: Wamasai wasiondolewe Ngorongoro

Hasira za kukosa uteuzi. Kule Zanzibar kuna waliokosa ulaji nao wanampinga Mwinyi asilete wawekezaji.

Yajayo YANAHUZUNISHA!.
Alishawahi kuteuliwa wapi na katika nini? Si kila mtu mtumwa wa teuzi, acha kumdhalilisha mwanataaluma huyu nguli. Amekuwa consistent muda wote wa maisha yake katika taaluma
 
kuondolewa kwa wamasai ngorongoro kuna tija hiyo ni busara wakaondolewa kwa kuwa tuna ardhi ya kutosha tu tz na kwa nn wang'ang'anie hifadhini

Kwani wanatolewa wamasai au watu wote wanaoishi kwenye hifadhi?
Mambo ya mwaka 1958 ndo yatuzuie kufanya kitu positive leo. Hata huko Handeni wanapopelekwa mwaka 2070 pakaonekana pana madini watatole
 
Kwa uhai wa ngorongoro miaka 20 ijayo, hakuna budi wamasai kuondoka tena kwa amani kabisa, kasi yao ya kuongezeka ni kubwa alafu eneo wanaloishi haliongezeki tusisahau hilo, wakati ni sasa ili tusilaumiane baadae
 
Kwa uhai wa ngorongoro miaka 20 ijayo, hakuna budi wamasai kuondoka tena kwa amani kabisa, kasi yao ya kuongezeka ni kubwa alafu eneo wanaloishi haliongezeki tusisahau hilo, wakati ni sasa ili tusilaumiane baadae
Ikumbukwe pia kuwa Hawa Wamasai wamesambaa maeneo mengine ya nchi. Kama yalivyo makabila mengine.

Pia kuhama huku kuonekane sawa tu na walihamishwa kutoka maeneo ya maji, yoevu, barabara, etc
 
Wamasai hawana haki milki ya Ngorongoro, kama wao walivyo na haki ya kuishi pale na watanzania wengine wasio wamasai (kwa makabila Yao) wana haki pia ya kuishi na kuendesha shughuli zao Ngorongoro na sehemu nyingine ndani ya mipaka ya nchi. Ili mradi wafate utaratibu na kuheshimu sheria za nchi na mamlaka zake...

hivyo isiwe kwa maasai pekee bali watanzania wote wapate fursa ya kuishi ngorongoro... na waheshimiwe...
 
Hasira za kukosa uteuzi. Kule Zanzibar kuna waliokosa ulaji nao wanampinga Mwinyi asilete wawekezaji.

Yajayo YANAHUZUNISHA!.
Ardhi ni mali ya nani?
Je, mdhamini ana powers za kukuondoa kwenye mkopo kwa manufaa yake binafsi?
Je, mdhamini wa passpoti ya kusafiria ana weza kukwapua passipoti yako kwa matumizi yake?
Je, mdhamini kwenye mchakato wa ajira anaweza kukuondoa kazini kwa maslahi yake?
Kama hapana mbona mdhamini wa ardhi (rais) ana uwezo wa kufanya chochote kwenye ardhi bila mashauriano au ridhaa ya anayemdhamini?

ARDHI NI MALI YA NANI??
 
Ardhi ni mali ya nani?
Je, mdhamini ana powers za kukuondoa kwenye mkopo kwa manufaa yake binafsi?
Je, mdhamini wa passpoti ya kusafiria ana weza kukwapua passipoti yako kwa matumizi yake?
Je, mdhamini kwenye mchakato wa ajira anaweza kukuondoa kazini kwa maslahi yake?
Kama hapana mbona mdhamini wa ardhi (rais) ana uwezo wa kufanya chochote kwenye ardhi bila mashauriano au ridhaa ya anayemdhamini?

ARDHI NI MALI YA NANI??
Pro Shivji ni miongoni mwa watanzania wenye asili ya asia. Kwahiyo yeye hata ardhi ikifanywa shamba la bibi na wafugaji wa Kenya hana cha kupoteza, ili mradi ashapewa chake na watafuna mirungi.
 
Maskini Tz yangu imekuwa nchi ya mibwabwa! Hivi professa shivji kakosea wapi kushauri?
Halafu kuna yanayohusisha na uteuzi maskini.
Kwani OBC amewagawia watanzania wote au ni ile mtu anachukua lions share anagawa peremende kwa masikini>
Wamasai, Raia halali wa JMT wanaswagwa kama wanyama huku nyani nyingine zikishabikia eti (funika pua) "uhifadhi" . Wamasai ni wahifadhi wazuri kuliko binadamu yeyote. Wameishi na wanyama kwa karne nyingi, -- Hawali nyamapori, Lakini muarabu anahamishia wanyama uarabuni hovyo.
Wamasai hawalimi wala kuharibu mazingira kwa namna yoyote.

Walindeni waarabu tu baadaye mtawakumbuka hawa wamasai mnaowaswaga.

professor Shivji amefanya tafiti nyingi katika maeneo hayo asikilizwe!!
 
Namsikiliza Prof. Shivji kupitia ITV. Shortly anasema Wamasai walihamishiwa Ngorongoro kutokea Serengeti Mwaka 1958 na kuahidiwa kutohamishwa. Anasema tusiwe na haraka ya kuwatoa Wamasai. Muhimu kuangalia haya.

1. Je Kuna wasio Wamasai wangapi waliojaa ndani ya Ngorongoro.

2. Tujadili nao mustakabali wao.

Kwa ufupi amepinga jambo hili la kuwahamisha wamasai
 
Sikuhitaji kujenga hoja kwa hilo tapeli la kibagachori. Anaendaga na upepo.
Mkuu wewe una roho ya makaburu, hata kama ni ngozi nyeusi we ni kaburu tu. Unaubaguzi wa kunuka inafaa kuogopwa kama ukoma. Iweje wa Tanzania tubaguane kwa uhindi na uafrika?
 
Pro Shivji ni miongoni mwa watanzania wenye asili ya asia. Kwahiyo yeye hata ardhi ikifanywa shamba la bibi na wafugaji wa Kenya hana cha kupoteza, ili mradi ashapewa chake na watafuna mirungi.
Ardhi ikiwa yako na unajua ni yako huwezi kuruhusu matumizi ya ovyo kama hayo.
Ila kwa sasa yote yanatokea kwa sababu hakuna wa mdhamini hana uwezo wa kusimamia ardhi.

Tatizo mkipingwa kwa hoka mnakimbilia kuhakiki asili za watu... Very weak
 
..Prof.Issa Gulamhussein Shivji ni mbobezi ktk masuala ya sheria za ardhi hapa Tz.

..kutokana na utaalamu wake aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchunguzi ya Raisi kuhusu sheria za ardhi.

..Prof.Issa Shivji ametetea haki za ardhi za jamii nyingi hapa Tz hususani jamii ya wafugaji wa Kibarbaig waliohamishwa kwa nguvu serikali kutoka ktk ardhi yao ya asili maeneo ya Basuto.

..Hakuna msomi anayeweza kutafiti masuala ya ardhi na mapambano ya haki ardhi hapa Tz asikutane au asitaje kazi za Prof.Issa Shivji.

NB:

..kwa wanaohoji asili yake, Prof.Shivji ni mzaliwa wa Kilosa Morogoro.
 
Kutokuwa na mpango wa matumizi sahihi ya ardhi kutaendelea kuligharimu taifa hili.

Matumizi ya ardhi yanavyofanyika utafikiri ardhi hii tuliyonayo inazaliana.

Baada ya wamasai kuwekwa ngorongoro serikali ilitakiwa kuwa na namna ya kucontrol population hiyo hata kuwa wanahamishwa baadhi ili kuhakikisha population haiathiri uhifadhi. Wamasai hata kama hawatahamishwa Leo lazima Kuna siku watahamishwa au ngorongoro itabadilika kuwa makazi ya kawaida ya watu na si wanyama.

Hata huku nje tulipo ardhi inazidi kuadimika lakini hakuna maono ya matumizi ya ardhi, Serikali yenyewe wanafurahi kujenga majengo mengi ya chini badala ya gorofa, hatujui ardhi ya matumizi ya msingi na muhimu tunazidi kuimaliza. Mashamba yanapungua na makazi yanaongezeka Kuna siku tutakula tofali.
Huko serikalini hakuna hata mmoja mwenye mawazo ya aina hii, kama yupo, ameridhika tu kupata mshahara wake wa kila mwezi.
 
Pro Shivji ni miongoni mwa watanzania wenye asili ya asia. Kwahiyo yeye hata ardhi ikifanywa shamba la bibi na wafugaji wa Kenya hana cha kupoteza, ili mradi ashapewa chake na watafuna mirungi.
Haya uliyoweka hapa yanaudhi, kama ilivyo kwa mtu mwingine kusema wenye wajomba nje ya nchi hii hawana uchungu wowote na nchi wanayoiongoza sasa zaidi ya kuwakatia mapande wajomba zao!

Prof. Shivji anaweza kuwa anaipenda sana nchi hii na watu wanaoonewa kuliko wewe unayepigania kujaza tumbo lako.
 
Namsikiliza Prof. Shivji kupitia ITV. Shortly anasema Wamasai walihamishiwa Ngorongoro kutokea Serengeti Mwaka 1958 na kuahidiwa kutohamishwa. Anasema tusiwe na haraka ya kuwatoa Wamasai. Muhimu kuangalia haya.

1. Je Kuna wasio Wamasai wangapi waliojaa ndani ya Ngorongoro.

2. Tujadili nao mustakabali wao.

Kwa ufupi amepinga jambo hili la kuwahamisha wamasai

Watanzania wengi hawajui wachokiongea na sishangai waongeaji wengi ni wenyeji wa pwani ambao hawajui hali halisi ya ngorongoro sisi tuliokaa Arusha ndiyo tunajua
1. Tatizo sio watu bali ni mifugo hivyo huyu Professor anaongelea watu kama vile ndiyo tatizo la hasha tatizo kubwa ndugu zangu ni hao ng'ombe ambao ni karibu 1M kutangatanga mbungani
2. Wamassai ni waharibifu wa mazingira. Watanzania tujiulize imekuwaje Wamassai wanasomba ng'ombe kutokea Mondoli mpaka Lindi! wamejaa bagamoyo, morogoro na Tanga na migogoro mingi ni ya kwao. Monduli nendeni mkaone jangwa lililo letwa na wafugaji hawa!.
3. Wamassai wamekuwa kama wafanyakazi wa watu wamassai wenye pesa na wafanyabiashara wanawapa ng'ombe wao wawafugie na wengine wanatoka mpaka Kenya na wengine ni viongozi serikalini
4. Mabadiliko ya mazingira yanayoendelea Dunia tatizo la malisho ya mifugo litaendelea hivyo ni bora watolewe sasa na sio baadae
5. Umefika muda wa kuwa na mifugo ya kisasa hivyo sio tu wanatolewa lakini wanaenda kuelekezwa ufugaji wa kibiashara na sio kufuga ili kuongeza wake pekee. Utamaduni huu wa sasa hauna tija kwa nchi. Watoto ni lazima wasome sio kushinda kucha kuchunga ng'ombe ambao nusu wanakaa mpaka wanakufa bila faida yoyote. Ngombe wa kimassai ni bei rahisi kuliko mbuzi wa South Afrika kwasababu wamekondo balaa.

Mimi binafsi na rafiki zangu tuna heka 62 kidomole pale Bagamoyo kila siku ni kugombana na hawa wamassai. Hawana faida yeyote wanaoleta kwa jamii zaidi ya ugomvi, uharibifu wa mazingira na kuendeleza ulimbukeni. Hatuwezi kutunza kabila kama vile nao ni utalii kama wanyama hii sio sawa. Hawa wana haki kama watanzania wengine na tuache tabia ya kuwadekeza badala yake tuwaulize. Kwanini watoto hawaendi shule, tutawapaje hospitali za kisasa katikati ya mbuga? je wakianza kuliwa na wanyama pori tuanze kuuwa wanyama mbugani? au tutume polisi akazuie tembo mbugani!. Wamassai watolewe na kama Professor yupo serious akakae nao kule mwezi mmoja tuone kama atapona

Hata USA kuna mbuga ambazo watu hawaruhusiwi kujenga.
 
Namsikiliza Prof. Shivji kupitia ITV. Shortly anasema Wamasai walihamishiwa Ngorongoro kutokea Serengeti Mwaka 1958 na kuahidiwa kutohamishwa. Anasema tusiwe na haraka ya kuwatoa Wamasai. Muhimu kuangalia haya.

1. Je Kuna wasio Wamasai wangapi waliojaa ndani ya Ngorongoro.

2. Tujadili nao mustakabali wao.

Kwa ufupi amepinga jambo hili la kuwahamisha wamasai
Siwapendi watu wanaojaribu kupotosha ukweli wa Loliondo kama Prof Shivji! Ila walioweka fikra wanaiona nuru!

1. Wajerumani walitawala 1881 hadi 1919: walilinda ushoroba wa Loliondo wa sqkm 4000, hakukuwa na wakazi wala wafugaji. Walitunga sheria za wanyamapori na misitu 1908, 1911, 1912.

2. Waingereza walitawala 1919 hadi 1961: walilinda ushoroba wa sqkm 4000 wa Loliondo na hakukuwa na wakazi wala wafugaji. Walitunga sheria ya Pori Tengefu la Loliondo 1951.

3. Baada ya Uhuru 1961 hadi sasa - madai Loliondo ni eneo sqkm 4000 ni la Waamasai. Isemwe umiliki wao ulianzia lini na walilipataje hilo eneo. Ukizingatia taarifa za watawala walivyoikuta na kuiacha Tanganyika zipo.
 
Haya uliyoweka hapa yanaudhi, kama ilivyo kwa mtu mwingine kusema wenye wajomba nje ya nchi hii hawana uchungu wowote na nchi wanayoiongoza sasa zaidi ya kuwakatia mapande wajomba zao!

Prof. Shivji anaweza kuwa anaipenda sana nchi hii na watu wanaoonewa kuliko wewe unayepigania kujaza tumbo lako.
Wewe ni mkenya, kwahiyo swala la ardhi ya Tanzania halikuhusu na hata kama likikuhusu ni kwa faida yako na mabwanyenye wako. Watu kama kina prof Shivji unaowaona wazalendo unakuta wana familia Tanzania na India, so anajua lolote likitokea Tanzania yeye anaenda zake India na kuishi sawa na raia wao wengine. So mtu wa aina hii hawezi kuwa na uchungu na chochote hata kama Tanzania nzima itavamiwa na wageni kwa faida ya nchi zao yeye ataona sawa tu maana hana cha kupoteza. Hawa wamasai wsngekuwa wana asili ya mkoa wa katikati ya Tanzania kama vile Dodoma, Morogoro nk usingesikia kelele unazosikia sasa, lkn kwa vile ni wa mpakani na kuhamishwa kwao kutaathiri mipango ya mabwanyenye ya nchi jirani ambayo yalikuwa yanatumia ardhi yetu kwa faida yao, ndo maana umeona hili swala limekuzwa kisiasa na kidiplomasia. Watu wangapi wamevunjiwa majumba yao na kuachwa bila makazi huko Kimara na kwengine, prof Shivji alikuwa wapi? Mbona hakuwasemea? Hata hivyo serikali imeshaamua, kwahiyo prof Shivji na genge lake wawashauri hao waliomtuma wahamishie mifugo yao katika nchi nyingine kama vile Uganda, Sudan, Ethiopia, Somalia nk kama wataweza kufanya hivyo.
 
Wewe ni mkenya, kwahiyo swala la ardhi ya Tanzania halikuhusu na hata kama likikuhusu ni kwa faida yako na mabwanyenye wako
Mbona unatabia ya kipuuzi namna hii, ya kupachika watu uraia usiowahusu kwa vile tu hawakubaliani na wewe? Sasa sisi tutajuaje kwamba wewe siyo mwarabu?

Mtu kama Prof. Shivji, maisha yake aliyoishi Tanzania na kufanya aliyofanya Tanzania halafu unam'steriotype' kama unavyofanya inaonyesha dhahiri wewe ni mpuuzi.

Kama hao watu wa mipakani ni wageni toka nchi za nje, utamlaumi vipi Shivji badala ya kuilaumu serikali iliyoshindwa kusimamia kazi ya kulinda mipaka ya nchi yake. Inaonyesha wazi uwezo wako wa kupambanua mambo ulivyo mdogo sana, kiasi kwamba unachoona rahisi kufanya ni kupachika watu wasiohusika na uraia usiowahusu. Hii haitasaidia chochote.
 
je wakianza kuliwa na wanyama pori tuanze kuuwa wanyama mbugani? au tutume polisi akazuie tembo mbugani!. Wamassai watolewe na kama Professor yupo serious akakae nao kule mwezi mmoja tuone kama atapona
Kama kawaida yako, umejichanganya sana katika uliyoandika kwenye bandiko lako hilo.
Yamo mazuri uliyoongelea, lakini unachanganya na kumlaumu Prof. kana kwamba yeye hayo mazuri kwa wamasai hayakubali. Unachanganya kwa sababu huelewi anachokisimamia Prof. kama alivyojieleza katika barua yake.

Hata hivyo ngoja nikufahamishe. hayo mabaya yanayotokana na wamasai ilaumu serikali. Kama watoto wao hawaendi shule, serikali inawajibu wa kuhakikisha watoto wote wa nchi hii wanapata elimu. Wazazi ni lazima waelimishwe na serikali juu ya umuhimu wa elimu kwa watoto wao.
Kama wamasai wanafanya uhalifu kwa wananchi wengine, ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa kila raia anafuata sheria kama inavyotakiwa bila ya kumwonea au kumpendelea yeyote.
Wamasai ni binaadam kama walivyo binaadam wengine, kwa hiyo hakuna sababu ya kusema hawawezi kufuata sheria zlizopo.
 
Back
Top Bottom