Prof. Sospeter Muhongo agawa chakula cha Dharura kwa Waathirika wa Mafuriko

Prof. Sospeter Muhongo agawa chakula cha Dharura kwa Waathirika wa Mafuriko

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
MHE. SOSPTER MUHONGO AGAWA CHAKULA CHA DHARURA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO

Leo, Jumanne, 4.4.2023, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo ametembelea Kijiji cha Kusenyi, Kata ya Suguti kwa malengo yafuatayo:
1. Kutoa pole kwa waathirika wa mafuriko ya juzi na jana
2. Kushuhudia uharibifu uliotokana na mafuriko hayo
3. Kugawa chakula cha dharura

Chakula alichogawa Mbunge huyo:
1. Magunia 25 ya Mahindi, kila gunia lenye Kilo 108
2. Maharage Kilo 100

Vitongoji vilivyoathirika sana
1. Kitongoji cha Nyabweke, Kaya 26 zimeathirika sana
2. Kitongoji cha Kwikuyu, Kaya 24 zimeathirika sana

Tathmini inaendelea kufanywa:
Wakati taathimini ya uharibifu uliotokana na mafuriko hayo ikiendelea kufanywa, Mbunge huyo amebaini yafuatayo:

1. Baadhi ya nyumba zimebomoka na kuanguka
2. Baadhi ya nyumba zimepasuka hazifai kutumika
3. Baadhi ya Kaya, Chakula chao kilichotunzwa majumbani kimeharibika na kingine kimesombwa na maji
4. Kuku na Bata wamesombwa na Maji
5. Tope ni nyingi sehemu za makazi ya watu

Tunategemewa kupata tathmini kamili ndani ya wiki hii.

Kilichosababisha maafa haya:
Wananchi, kwa uzoefu wao, wamebaini sababu kuu mbili:
1. Ujenzi wa barabara ya lami ya km 5, haukuzingatia uwekaji wa njia za kutosha kupitisha maji kwenda ziwani (Ziwa Victoria)
2. Wakulima wa Mpunga, n.k. walioko sehemu ya juu ya Kijiji cha Kusenyi wameweka miundombinu yao ya kilimo inayozuia maji kutitirika kwenye mikondo inayoelekea ziwani.

OMBI KUTOKA KIJIJINI KUSENYI

Waathirika wa mafuriko ya Kijijini Kusenyi wanaomba tuwasaidie:
1. Chakula
2. Vifaa vya ujenzi (tathmini itaainisha idadi)
3. Ujenzi wa miundombinu mikubwa ya kutiririsha maji ziwani.

Michango ipelekewe kwa: DC Wilaya ya Musoma; +255 756 088 624

Picha za hapa zinaonesha matukio mbalimbali ya Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mhe. Prof Sospeter Muhongo akiwa na:
1. Waathirika wa mafuriko Kijijini Kusenyi, Kata ya Suguti
2. Viongozi 3 kutoka Kijijini Kusenyi wakipokea magunia 25 ya mahindi (Kilo 108), na gunia 1 la maharage la kilo 100.

TAFADHALI SANA TUJITOKEZE KUWASAIDIA WAATHIRIKA WA MAFURIKO YA KIJIJINI KUSENYI

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumanne, 4.4.2023
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-04-04 at 18.29.44.jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-04 at 18.29.44.jpeg
    123.3 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-04-04 at 18.29.45(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-04 at 18.29.45(1).jpeg
    158.1 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-04-04 at 18.29.45(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-04 at 18.29.45(2).jpeg
    178.7 KB · Views: 2
Huyu mwamba namkubali sana! Kimyaaa, hana shobo na mtu. Akitoa fact zake za kisomi na mjingamjinga mmoja akatokea na kumbishia ye anakausha kimya anaendelea na habari zake. Safi kabisa!
 
Back
Top Bottom