Mandla Jr.
JF-Expert Member
- Dec 15, 2013
- 3,098
- 631
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetakiwa kuweka kando tofauti za kisiasa na kuunganisha nguvu zao, hasa katika kipindi hiki ambacho taifa lipo katika mchakato wa uundaji wa Katiba Mpya.
Wito huo umetolewa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba alipokuwa akifungua mkutano wa baraza kuu la chama hicho.
Kauli hiyo ya Lipumba inakuja kutokana na vuguvugu la mgogoro ulioibuka hivi karibuni ndani ya CHADEMA ambao ulisababisha aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zitto Kabwe kuvuliwa nafasi zake zote za uongozi.
Uamuzi huo pia ulimkumba aliyekuwa mjumbe wa Kamati kuu ya Chama icho Dk Kitila Mkumbo na Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Wito huo umetolewa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba alipokuwa akifungua mkutano wa baraza kuu la chama hicho.
Kauli hiyo ya Lipumba inakuja kutokana na vuguvugu la mgogoro ulioibuka hivi karibuni ndani ya CHADEMA ambao ulisababisha aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Zitto Kabwe kuvuliwa nafasi zake zote za uongozi.
Uamuzi huo pia ulimkumba aliyekuwa mjumbe wa Kamati kuu ya Chama icho Dk Kitila Mkumbo na Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.