John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Black Rhino ambaye ni mdogo wa Profesa Jay amezungumzia kuhusu maendeleo ya kaka yake ambaye amelazwa Muhimbili.
Joseph Haule au Jay ambaye ni mwanasiasa na msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, alikuwa yuko sawa, alienda Bukoba akafanya shoo fresh tu na kudrive kurudi Dar na kuendelea na mishe zake.
“Akiwa yupo Bukoba kwa ajili ya shoo alianza kulalamika kuwa hajisikii vizuri lakini kwa kuwa alikuwa ameshachukua hela ya watu akaamua kufanya shoo na kuondoka kurudi Dar.
“Alipofika hapa (Dar), ikawa kama wiki hivi, analalamika hajisikii vizuri, anaenda hospitali anapewa dawa na kuendelea na maisha, lakini siku kama ya saba hivi tangu atoke safari akasema hajisikii vizuri akaomba tumpelekea hospitali.
“Hivyo, kuhusu anasumbuliwa na nini hilo ni suala la kwake binafsi siwezi kuliingilia au kulizungumzia hadharani.
“Hizo taarifa zinazoendelea mitandaoni siyo za kweli na imetusikitisha sana familia.
“Ukiwa unapitia kitu kama hiki kisha unaona mitandaoni watu wanaongea mambo ambayo siyo ya kweli, imetusikitisha sana kwa kuwa kuna watu hawana ubinaadamu.
“Siyo uungwana kuona mwenzako anaumwa kisha unaanza kusambaza taarifa ambazo siyo za kweli, hao watu ni wahuni au siyo wastaarabu wanaosambaza hizo taarifa, kuna hatua za kisheria zimeanza kuchukuliwa kuhusu uwongo wanaosambaza mitandaoni.
“Watanzania wapunguze hofu, Jay anaendelea vizuri, japo brother alikuwa anaumwa, yaani anaumwa sana lakini kwa sasa kuna nafuu, tuwekeze nguvu kuendelea kumuombea ili anyanyuke na kuweza kutoka hospitali.
“Nilipokuwa kwake mara ya mwisho alinisikilizisha kazi zake na kuna moja alitaka kufanya kazi na Zuchu, akaniambia nimpe ushauri,” anasema Rhino ambaye naye pia ni msanii wa Bongo Fleva.
Joseph Haule au Jay ambaye ni mwanasiasa na msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, alikuwa yuko sawa, alienda Bukoba akafanya shoo fresh tu na kudrive kurudi Dar na kuendelea na mishe zake.
“Akiwa yupo Bukoba kwa ajili ya shoo alianza kulalamika kuwa hajisikii vizuri lakini kwa kuwa alikuwa ameshachukua hela ya watu akaamua kufanya shoo na kuondoka kurudi Dar.
“Alipofika hapa (Dar), ikawa kama wiki hivi, analalamika hajisikii vizuri, anaenda hospitali anapewa dawa na kuendelea na maisha, lakini siku kama ya saba hivi tangu atoke safari akasema hajisikii vizuri akaomba tumpelekea hospitali.
“Hivyo, kuhusu anasumbuliwa na nini hilo ni suala la kwake binafsi siwezi kuliingilia au kulizungumzia hadharani.
“Hizo taarifa zinazoendelea mitandaoni siyo za kweli na imetusikitisha sana familia.
“Ukiwa unapitia kitu kama hiki kisha unaona mitandaoni watu wanaongea mambo ambayo siyo ya kweli, imetusikitisha sana kwa kuwa kuna watu hawana ubinaadamu.
“Siyo uungwana kuona mwenzako anaumwa kisha unaanza kusambaza taarifa ambazo siyo za kweli, hao watu ni wahuni au siyo wastaarabu wanaosambaza hizo taarifa, kuna hatua za kisheria zimeanza kuchukuliwa kuhusu uwongo wanaosambaza mitandaoni.
“Watanzania wapunguze hofu, Jay anaendelea vizuri, japo brother alikuwa anaumwa, yaani anaumwa sana lakini kwa sasa kuna nafuu, tuwekeze nguvu kuendelea kumuombea ili anyanyuke na kuweza kutoka hospitali.
“Nilipokuwa kwake mara ya mwisho alinisikilizisha kazi zake na kuna moja alitaka kufanya kazi na Zuchu, akaniambia nimpe ushauri,” anasema Rhino ambaye naye pia ni msanii wa Bongo Fleva.