Profesa Jay

Profesa Jay

Wadau wa muziki maarufu kama Bongo Fleva, mmesikia wimbo mpya wa Prof. J? Unaitwa KamiliGado.

Nahisi Profesa Jay ameanza 'kuzeeka' maana huo wimbo haudhihirishi 'uprofesa' wake. Ameamua kuimba, yeah, autotune and all that but melody ya wimbo ni ya kawaida sana. Mistari pia hain lolote jipya given that anarap kuhusu Mapenzi (atleast angeonesha uniqueness and creativity in rapping about love).

Kwasababu anajua wimbo wake ni mbovu na hivyo unahitaji promo ya ziada, ameamua kuufungulia website (mara ya kwanza kuona wimbo unafunguliwa website) www.kamiligado.com ilhali yeye kama msanii hana website ya kumtambulisha!

The only reason why his song is getting airplay, ni 'kulinda heshima'!

Ushauri wa bure: Nunua mashairi makali ama 'tundika daluga'!
True mkuu mwenyewa fan wake ila hapa big no
 
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni.. Prof.. Amebadilika kwenda sambamba na soko linavyoenda.. Kaja poa.. Mbona Snoop Dogg' anabadilika anaimba, anatumia auto.. tune.. Tumpe credit hapa..
 
angekomaa na style ile watu waliyompendea nayo angekuwa mmoja ya wanaharakati wakubwa bongo..lakini hii ya msanii mkubwa kama prof. jize kuwaiga akina diamond..yaani anatamani awe kama wao, inakera sana!!!! sifa kuu ya msanii wa hip hop ni msimamo! kila Msanii wa Hip HOP anawaza kuja kuwa C.E.O wa kamapuni flani mbeleni...lakini Jay Ukimwambia hata aandae Tamasha la watoto kuonyesha vipaji vyao Hajui A,B,C....IKOJE...Kachelewa ila bado ana nafasi ya kufanya kitu ila wakati wa kufanya Muziki hivi bila kufanuya Harakati za kujikomboa kama msanii umeshapita!!!!!
 
angekomaa na style ile watu waliyompendea nayo angekuwa mmoja ya wanaharakati wakubwa bongo..lakini hii ya msanii mkubwa kama prof. jize kuwaiga akina diamond..yaani anatamani awe kama wao, inakera sana!!!! sifa kuu ya msanii wa hip hop ni msimamo! kila Msanii wa Hip HOP anawaza kuja kuwa C.E.O wa kamapuni flani mbeleni...lakini Jay Ukimwambia hata aandae Tamasha la watoto kuonyesha vipaji vyao Hajui A,B,C....IKOJE...Kachelewa ila bado ana nafasi ya kufanya kitu ila wakati wa kufanya Muziki hivi bila kufanuya Harakati za kujikomboa kama msanii umeshapita!!!!!

Umeongea kitu cha msingi sana. Jay akiwa kama mkongwe watu walitegemea awe na kampuni yake anakuza wasanii lakini hatuwezi jua kwanini hajafanya hivi!
 
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni.. Prof.. Amebadilika kwenda sambamba na soko linavyoenda.. Kaja poa.. Mbona Snoop Dogg' anabadilika anaimba, anatumia auto.. tune.. Tumpe credit hapa..

Autotune ishapitwa na wakati alafu unasema anakwenda sambamba na soko. Ilibidi autotune itumike pale kwasababu kuna 'sauti' za kuimba sio ya Jay. Yake ya michano.

By the way, point yangu haikua hiyo bali ukiusikiliza huo wimbo melody yake si ya kuvutia. Na mashairi pia hayana jipya ukizingatia ni ya mapenzi nilitegemea kusikia vitu tofauti lakini ni yale yale. No credit for that
 
Tatizo la muziki ndio hilo. Mashabiki wanategemea kila siku utoe kitu kikali. We utakitoa wapi? Ukitoa kibaya watu wanakukataa utadhani hawakujui! Ndio maana hua nawaonea huruma wasanii wanaopata vihela badala ya kujijenga wanaendekeza starehe.
 
Prof Jay kasanda hana jipya wimbo wa mwisho mkali ni Hapo vipi? Hapo sawa 2009 baaaasiiii

hii sio kweli mazee unless u don' like his music or whatever.Ingawa tuna mitazamo tofauti tofauti lakini reality stands,obviously hii track kamili gado haiko kamili gado hata kidogo lakini huwezi ku-judge kua dude kasanda sikiliza na tazama vizuri track iliopita (haijapita hata 6 months tangu kua released) "kama ipo ipo(kupanda na kushuka)" then prove me wrong!!!
 
Profesa kaishiwa tukisema ukweri,labda kama ni kumuonea huruma...amefikia levo anawakopi kina Godzila na Diamond kubana pua!
 
Profesa kaishiwa tukisema ukweri,labda kama ni kumuonea huruma...amefikia levo anawakopi kina Godzila na Diamond kubana pua!

Wacha tuseme ukweli, hati wakituita ma'hater. Message sent
 
Sidhani kama kuna haja ya kulalamika juu ya wingi wa mashairi ya mapenzi. Binadamu tumeumbwa kupenda na siku zote ni mapenzi ndiyo yanayokimbiza ulimwengu, utake usitake. Ulitaka waimbe juu ya CCM na CHADEMA?

Kwa hiyo hapo umefika mwisho kabisa?
 
Tatizo lenu vigeu geu...Watatoa kali mtarudi kuwasifu humu humu jamvini...Kikubwa tu ni kwamba huwezi kum-judge mtu kwa wimbo mmoja tu, hata studies za evaluation hazielekezi hivyo ndugu zangu. It take a great deal of time to conclude whether someone is finished or not.

Great thinkers mnaniangusha...You are coming up with very cheap reasoning, light brains and corrupted minds.....Hii nchi itakwenda kweli jamani kama mnaojiita great thinkers mko hivi?

Personal grudges should not be entertained in this forum......They are not good indices of great thinking at all.
 
Tatizo lenu vigeu geu...Watatoa kali mtarudi kuwasifu humu humu jamvini...Kikubwa tu ni kwamba huwezi kum-judge mtu kwa wimbo mmoja tu, hata studies za evaluation hazielekezi hivyo ndugu zangu. It take a great deal of time to conclude whether someone is finished or not.

Great thinkers mnaniangusha...You are coming up with very cheap reasoning, light brains and corrupted minds.....Hii nchi itakwenda kweli jamani kama mnaojiita great thinkers mko hivi?

Personal grudges should not be entertained in this forum......They are not good indices of great thinking at all.

1. Kutoa wimbo mbovu ni sign ya kuishiwa.
2. Jay is a Bongo Fleva Legend that won't change.
3. Ofcourse akitoa wimbo mkali tutasifu kama vile tunavyoponda akitoa wimbo mbovu.
4. Personal grudges?? Did I mention anything personal about Jay? NO. I'm talking about his music here so may be you can call them 'Professional grudges', lol.
5. Take note son!
 
Naona tayari kuna kujaji kwa kupambanisha majina..hv ugumu uko wapi kuliko kumbeza kwanini usimshauri mtu katika positive way..kwanini usimpe courage?tena kwa mabango,vijembe,kukandia...why this damn?

Of course hii ngoma yake haiko artistic i.e haina creativity kitone(vocal)na kimaneno lakini katika simple logic tujiulize wimbo huu ukiwa mbaya pekee kwenye album yenye ngoma 10 kuna tatzo gani?ama ukiziangalia album zake zote 4/5 ni kweli nyimbo zote zililingana quality?ama huyo mkongwe Sugu na album zake 7/8 nyimbo zote zilibamba kisawa?

Yawezekana Jay kachoka lakini ni lazima tukakubali kwamba hii kachemka,tumshauri lakini bado kwa kipaji chake alichonacho na ukiangalia kazi zake siamini kama nyimbo mbili ama hata tatu zinatosha kuprove kuzeeka kwa Jay

Tuendelee kumfuatilia na mwisho tupate kusema ukweli wenyewe na si blabla hapa jamvini...wanazi tunaomba umakini wenu msipende kuongea kwa hisia kama wanamama.
 
Wadau wa muziki maarufu kama Bongo Fleva, mmesikia wimbo mpya wa Prof. J? Unaitwa KamiliGado.

Nahisi Profesa Jay ameanza 'kuzeeka' maana huo wimbo haudhihirishi 'uprofesa' wake. Ameamua kuimba, yeah, autotune and all that but melody ya wimbo ni ya kawaida sana. Mistari pia hain lolote jipya given that anarap kuhusu Mapenzi (atleast angeonesha uniqueness and creativity in rapping about love).

Kwasababu anajua wimbo wake ni mbovu na hivyo unahitaji promo ya ziada, ameamua kuufungulia website (mara ya kwanza kuona wimbo unafunguliwa website) www.kamiligado.com ilhali yeye kama msanii hana website ya kumtambulisha!

The only reason why his song is getting airplay, ni 'kulinda heshima'!

Ushauri wa bure: Nunua mashairi makali ama 'tundika daluga'!
hapana bwana huo ni mtazamo wako ila mm namwona jay bdo ni mkali na ule wimbo ni mkali. Mbona busta kabadilka bwana mambo yanabadilika ndugu tua mzigo wa mwiba
 
kwanza vionjo kaiba Nigeria ni vionjo vya kina Jo Martin.....Prof J jirudi baba,kuanza sio ujinga.
 
hapana bwana huo ni mtazamo wako ila mm namwona jay bdo ni mkali na ule wimbo ni mkali. Mbona busta kabadilka bwana mambo yanabadilika ndugu tua mzigo wa mwiba

Ni mtazamo wangu, mawazo yangu na yana'base kwenye weledi. Nimetoa sababu za ki'weledi. We una sababu ipi kuona kama si kweli? Ahsante
 
Back
Top Bottom